Spika Ndugai: Ajira ziwe zinazingatia usawa wa Kijografia

zandrano

JF-Expert Member
Jan 24, 2017
7,128
7,710
Spika ndugai alinena hiyo jana akiwa bungeni alitahadharisha sana kama taifa tuna hitaji ajira zinazo serikalini zizingatie uwiano ulio sawa yaani kimikoa, na hata Kidini.

Ametahadharisha endapo ajira zitaelemea kuajiri au hata kuteua watu wa aina mmoja kwa maana ya kimaeneo hata kiimani moja zaidi ni hatari sana kwa umoja na mshikamano wa taifa letu.

Nakubaliana nae asilimia 100 kuwa Taifa hili la Tanzania ni letu sote hivyo ni kweli na haipendezi na wala haifai, watu wa aina mmoja au kanda mmoja au hata wa aina mmoja ya imani ndio wawe wame hodhi nafasi zote za ajira au hata za kuteuliwa ktk nafasi za utumishi wa umma, jambo hilo lisipo angaliwa bila kuoneana aibu litaipasua Taifa letu siku za mbeleni, hivyo ni muhimu sana jambo hilo likazingatiwa ktk ajira na teuzi ili kuweka uwiano ulio sawa kwa mustakibali wa umoja wa taifa letu.

Ili kujenga na kuimarisha umoja na uzalendo ni muhimu ktk kuteua watumishi wa serikali uweke mseto wenye usawa mabao utawakilisha sura ya Taifa letu.

Kila mara kumekuwapo na manung'uniko ya watu wa Imani moja kuona wao wameminywa ktk nafasi za seriikalini na wengine wapo wengi zaidi kuliko wao, jambo hili sio zuri lazima litazamwe kwa nia njema, na jambo hili pia linahitaji utafiti.

Napendekeza kabla ya kutekeleza kila idara ya serikali yenyewe ifanye utafiti kwa watumishi wake wote ilio nao je?

Inazingatia Jografia ya nchi yetu? Je, kuna uwiano wa kiimani ktk nafasi mbalimbali?

Madhara ya kujaza kundi au aina ya watu fulani ktk utumishi wa umma ni hatari sana kwa umoja na uzalendo wa nchi yetu.

Asante Mhe. Spika kwa kutoa angalizo hilo la msingi na lenye nia njema ya kujenga ummoja wa nchi yetu. Ni matumaini yetu mamlaka za uteuzi na ajira zitalizingatia hilo.

UMOJA NI NGUVU, NCHI ITA JENGWA KWA UMOJA WETU NA SIO BAADHI YA WATU.

USHIRIKIANO WA WATU WOTE KTK KULIJENGA TAIFA LAO NI JAMBO MUHIMU SANA KWA UMOJA NA UIMARA WA NCHI, TUSIONEANE AIBU TUAMBIZANE UKWELI KWA MASILAHI YA TAIFA LETU.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Umenikumbusha, Doto biteko, merdard kalemani, Doto James, Dr Dorothy Gwajima, mganga mkuu wa serikali, mbunge wa Geita mjini aliyewahi kuwa naibu waziri wa maliadili na utalii, mkulu, anjelina mabula, DC siha, RC manyara wakati ule Mr mnyeti, RC Njombe wa sasa, wote hawa ni ukoo mmoja.
 
Si wanafanya interview, kama ilifanyika kwa usahihi,,hata wakipata wa ukanda mmoja sawa tu, si ni watanzania. Ndugai hana chembe ya kuaminika, si wa kumwamini. Hafai.
" Ajira za walimu na madaktari hakunaga interview"
 
Umenikumbusha, Doto biteko, merdard kalemani, Doto James, Dr Dorothy Gwajima, mganga mkuu wa serikali, mbunge wa Geita mjini aliyewahi kuwa naibu waziri wa maliadili na utalii, mkulu, anjelina mabula, DC siha, RC manyara wakati uke Mr mnyeti, Rc Njombe wa sasa, wote hawa ni ukoo mmoja
Kanda ya ziwa ina percent kubwa ya watu kuliko eneo lolote. Haiwezekani Wazanzibar na Wamakonde, ambao hawajazi uwanja wa Uhuru, wakawa wengi serikalini kuliko Wasukuma na Wajita.
 
Kanda ya ziwa ina percent kubwa ya watu kuliko eneo lolote. Haiwezekani Wazanzibar na Wamakonde wakawa wengi serikali kuliko Wasukuma na Wajita.
Nafasi za ualimu na udaktari zipo elfu sita, waombe,wanahitaji wapewe uwaziri tu?
 
Kanda ya ziwa ina percent kubwa ya watu kuliko eneo lolote. Haiwezekani Wazanzibar na Wamakonde, ambao hawajazi uwanja wa Uhuru, wakawa wengi serikalini kuliko Wasukuma na Wajita.
Idadi ya watu walioko kanda ya ziwa ni wafugaji,wachimbaji na wavuvi, ila ukuu wa mikoa, uDc,uwaziri wañahitaji.
 
Anazungumzia ajira kama vile zipo za kutosha, wakati ajira ni chache hata wanaopata huwa hawajulikani, hasa wakishagawia watoto wao, ndugu, na marafiki zao.
 
Imani inayooenda kulalamika lalamika inafahamika. Hata bila sababu hulalamika tu.
 
Umenikumbusha, Doto biteko, merdard kalemani, Doto James, Dr Dorothy Gwajima, mganga mkuu wa serikali, mbunge wa Geita mjini aliyewahi kuwa naibu waziri wa maliadili na utalii, mkulu, anjelina mabula, DC siha, RC manyara wakati ule Mr mnyeti, Rc Njombe wa sasa, wote hawa ni ukoo mmoja
Ivi uyu mnyeti sasaivi ni RC wa mkoa gani
 
Nafasi za ualimu na udaktari zipo elfu sita, waombe,wanahitaji wapewe uwaziri tu?
Uwiano wao lazima utakuwa na uwakilishi mwingi kwenye ajira za kawaida na uwaziri pia. Wachagga wote Kilimanjaro hawajazi Kishapu, I mean, Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu inalingana na mkoa wa Kilimanjaro, sasa Wachagga watakuaje wengi TRA kuliko Wasukuma?
 
Back
Top Bottom