Spika na double standard yake kuhusu rostam

politiki

JF-Expert Member
Sep 2, 2010
2,376
1,507
spika anadai anasubiri barua kutoka kwa chama ili aweze kutambua kujiuzulu kwa Rostam na kwamba
barua ya rostam pekee haitoshi kutangaza kuthibitisha kujiuzuru kwake. lakini kwenye miaka ya 90, CUF ilishawahi
kumfukuza mbunge uanachama na kumuandikia spika wakati huo kama sikosei alikuwa msekwa kumtaarifu kuwa
kama sikosei mbunge huyo jina alikuwa anaitwa NAILA JIDAWI kuwa siyo tena mwanachama wao na hastahili kuwa
mbunge tena lakini spika alikataa kutambua barua ya chama na Naila jidawi akaendelea na ubunge wake. kuna utata hapa.

mwingine diwani wa chadema huko mbeya aliandika barua ya kujiuzulu kwa meya na baadaye aliandika barua nyingine
kufuta barua yake ya kwanza ya kujiuzulu lakini meya amekataa anadai kwa kuwa diwani alishaandika barua ya kujiuzulu
hiyo pekee inatosha na ktk hili haikusubiriwa barua ya kutoka kwa chama wala nini ? hii si double ya nguvu. inakuwaje
ndani ya nchi moja kuwe na sheria mbili tofauti na itafisiliwe kulingana na mazingira yaliyopo. naomba msaada wa ufafanuzi
jamani!.
 
wewe unatakaje? Rostam aendelee kuhudhuria vikao vya bunge??? hebu watanzania tubadilike...hivi unataka sisi tuache kufikiria mambo muhimu tuanze kujadili issue ya Rostam aliejiuzulu!!!!! will it make life different??/
 
Kwan huyo diwani wa chadema alikuwa chizi mpaka anajikanganya hivo?inaönekana huyo alishinda kwa upepo wa dr slaa,sawa na wale wa arusha,maskini cdm!....eti hata diwani anakitunishia msuri chama,ukishangaa ya musa....
 
mkuu RA kama ulimsoma vizuri MM Mwanakijiji amesema kuwa kafanya hivyo kukinusuru chama na sio nchi na ndio sasa inadhihirika hilo sasa kwa huyu mh makinda..
 
Barua ya Rostam Azizi ya kujuizulu iko kwenye ukarasa wa mbele (front page) ya Mwanahalisi -July 20, 2011. Kwa maneno mengine watanzania wapatao takribani elfu kumi waliosoma hili gazeti week hii wanajua reference number ya barua na contents zake zote. Spika Makinda mwenye access ya kila kitu anasema hajapata barua! Hivi ni kweli hajapata barua au hataki kupata hii barua? Na kama kweli haijafika kwake haoni umuhimu wa kutaka maelezo juu ya swala hili maana Rostam kakaririwa na vyombo vyote vya habari nchini (including TBC) akitangaza kujuzulu?

Why can't she lift her bam and ask what is going about a member of the parliment? Tabia ya viongozi wetu kusubiri kila kitu kiwe mezani inatia kinyaa. Takukuru hanyanyuki mpaka aletewe ushahidi? polisi hasogei mpaka apate usafiri, waziri (i.e Chikawe) hataki kuchunguza wizi mpaka aletewe ushahidi!

Kwa maoni yangu, kwa kiongozi yeyote kutojua nini kinachoendelea kwenye 'ulingo' wa kazi au ofisi yake ni uzembe na hafai kuwepo kwenye nafasi hiyo. Kwa spika kutokuwa na barua au kujuwa kujiuzulu kwa mbunge ni udhaifu usiokubalika na inaleta picha ya wasiwasi kuwa she doesnt know anything so how can she lead? Yaani mzazi unalala ndani huku hujui kama watoto wote wapo nyumbani au la!!! Pengine Spika angeacha kujifundisha namna ya kujibu hoja za serikali na kujikita zaidi kwenye kazi za bunge basi angekuwa amepata taarifa kamili juu ya kujiuzulu kwa mbunge. Awasiliane na KUBENEA. He knows something!
 
Barua ya Rostam Azizi ya kujuizulu iko kwenye ukarasa wa mbele (front page) ya Mwanahalisi -July 20, 2011. Kwa maneno mengine watanzania wapatao takribani elfu kumi waliosoma hili gazeti week hii wanajua reference number ya barua na contents zake zote. Spika Makinda mwenye access ya kila kitu anasema hajapata barua! Hivi ni kweli hajapata barua au hataki kupata hii barua? Na kama kweli haijafika kwake haoni umuhimu wa kutaka maelezo juu ya swala hili maana Rostam kakaririwa na vyombo vyote vya habari nchini (including TBC) akitangaza kujuzulu?

Why can't she lift her bam and ask what is going about a member of the parliment? Tabia ya viongozi wetu kusubiri kila kitu kiwe mezani inatia kinyaa. Takukuru hanyanyuki mpaka aletewe ushahidi? polisi hasogei mpaka apate usafiri, waziri (i.e Chikawe) hataki kuchunguza wizi mpaka aletewe ushahidi!

Kwa maoni yangu, kwa kiongozi yeyote kutojua nini kinachoendelea kwenye 'ulingo' wa kazi au ofisi yake ni uzembe na hafai kuwepo kwenye nafasi hiyo. Kwa spika kutokuwa na barua au kujuwa kujiuzulu kwa mbunge ni udhaifu usiokubalika na inaleta picha ya wasiwasi kuwa she doesnt know anything so how can she lead? Yaani mzazi unalala ndani huku hujui kama watoto wote wapo nyumbani au la!!! Pengine Spika angeacha kujifundisha namna ya kujibu hoja za serikali na kujikita zaidi kwenye kazi za bunge basi angekuwa amepata taarifa kamili juu ya kujiuzulu kwa mbunge. Awasiliane na KUBENEA. He knows something!
mheshimiwa spika ameshakiri kama amepokea barua kutoka kwa RA, utetezi wake mpya hivi sasa ni kuwa hajapokea barua kutoka kwa chama.
 
Back
Top Bottom