Mwanza Press Club, tunaungana na wanahabari wote nchini kulaani kwa nguvu zote amri ya KIUKANDAMIZAJI iliyotolewa na Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, la kupiga marufuku kwa wandishi wa habari kufanya mahojiano na wabunge wanaosusia (wasiokubaliana) mwenendo wa uendeshaji wa bunge hilo.
Huo ni ukiukwaji mkubwa na uliovuka mipaka wa haki ya kutafuta, kupata na kutoa habari inayotolewa na Katiba ya Jamhuri.
Wandishi wa habari kufanya kazi za bunge na bunge kufanyakazi na wandishi wa habari sio HISANI, ni takwa la kikatiba na utawala bora. Mwandishi wa habari anao uhuru wa kutafuta habari mahala popote bila ya kuvunja sheria.
Bunge ni mkutano wa hadhara wa wawakilishi wa wananchi, hivyo ni lazima wananchi wapate habari ya yale yanayojadiliwa na wawakilishi wao kwasababu yanawahusu na yanahusu ustawi wao.
Spika anapaswa kutambua kuwa hata alipopiga marufuku kuonyeshwa kwa mijadala ya bunge moja kwa moja (live) wananchi hawakupendezwa na hatua hiyo na hivyo hatua yoyote inayozidi kulitia giza shughuli za bunge haliwezi kuungwa mkono.
Kama Spika anayo ajenda zake za siri ambazo hataki wananchi wazijue ni vema aseme kwa uwazi na azityekeleze nje ya bunge kwasababu bunge hilo ni la wananchi.
Tunamtaka Spika afute katazo hilo na kuwaachia uhuru wa kiutendaji wandishi wa habari na asijaribu kutufumba midomo na macho kama anavyowafanyia wabunge. - Mwenyekiti
Huo ni ukiukwaji mkubwa na uliovuka mipaka wa haki ya kutafuta, kupata na kutoa habari inayotolewa na Katiba ya Jamhuri.
Wandishi wa habari kufanya kazi za bunge na bunge kufanyakazi na wandishi wa habari sio HISANI, ni takwa la kikatiba na utawala bora. Mwandishi wa habari anao uhuru wa kutafuta habari mahala popote bila ya kuvunja sheria.
Bunge ni mkutano wa hadhara wa wawakilishi wa wananchi, hivyo ni lazima wananchi wapate habari ya yale yanayojadiliwa na wawakilishi wao kwasababu yanawahusu na yanahusu ustawi wao.
Spika anapaswa kutambua kuwa hata alipopiga marufuku kuonyeshwa kwa mijadala ya bunge moja kwa moja (live) wananchi hawakupendezwa na hatua hiyo na hivyo hatua yoyote inayozidi kulitia giza shughuli za bunge haliwezi kuungwa mkono.
Kama Spika anayo ajenda zake za siri ambazo hataki wananchi wazijue ni vema aseme kwa uwazi na azityekeleze nje ya bunge kwasababu bunge hilo ni la wananchi.
Tunamtaka Spika afute katazo hilo na kuwaachia uhuru wa kiutendaji wandishi wa habari na asijaribu kutufumba midomo na macho kama anavyowafanyia wabunge. - Mwenyekiti