Specifications za Tigo Kitochi 4G

Msisahau kitochi cha Voda ni 3G na sio 4G, nimeenda leo Makumbusho kununua kitochi chenye uwezo wa 4G kama wanavyotangaza radioni nimeambiwa vitaanza kuuzwa kesho.
 
Nimenunua ya voda, kwanza ni 3G na sio 4G
Imetengenezwa na kampuni inaitwa AZUMi na model ni L3K
Unatumia mfumo endeshi wa KaiOS kama simu za nokia feature phones mfano banana phone na zingine

Inatumia chip ya mediatek, sikumbuki vizuri ila ni 65xx

Basically ni simu ya tochi usitegemee chochote cha ajabu

Ina whatsapp na social network apps ambazo unaweza kuinstall na ku uninstall kutoka app store yao.

Kitu nilichopenda ni uwezo wa ku sync contacts kutoka google na Live

Spidi ni ya simu ya tochi

Hitimisho, inaenda sawa na gharama unayolipia, by the way, voda walinipa bando 4Gb, dakika nyingiii na sms kibao

Nadhani ya tigo nayo ni kutoka azumi ila ni version ya 3G
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…