Special Thread: Walioachwa tuliwazane hapa

Special Thread: Walioachwa tuliwazane hapa

Kuna kamanzi nilikuwa natoka nacho huwa mara nyingi alikuwa ananitishia kuniacha kidume nikajiongeza
Ikabidi wiki nzima niwe naye beneti Na ku act kwake as real gentleman
Loh!nilichomfanya baada ya kuona amekolea sana kwangu nikamtema
Nilimuumiza Sanaa yaan mpaka Leo anachukia wanaume lakini wadau nilifanya hivyo coz
Kipindi cha mwanzo alikuwa ananitishia kuniacha me kidume nikawa napima upepo tu
Dah ni hatari
 
Hahaha, akiba haiozi mkuu yani angeachwa hapo wala asingekuwa NA MAWAZO kwa sababu anajua anapakukimbilia.
Kuna kuachwa kwingine unapigwa hadi bumbuwazi!akilo inaganda hadi unasahau kama ulikua na "Akiba"
Pole yake aliyeachwa atulize kichwa,atapata mwingine!mapenzi kama siti ya daladala akishuka mtu anapanda mtu
 
pole chukulia kawaida ni kama unavyopoteza hela zinauma lkn unatafuta tena kikubwa ni uhai utampata wa kukonga moyo wako utasahau ya zamani.
 
Kuna kuachwa kwingine unapigwa hadi bumbuwazi!akilo inaganda hadi unasahau kama ulikua na "Akiba"
Pole yake aliyeachwa atulize kichwa,atapata mwingine!mapenzi kama siti ya daladala akishuka mtu anapanda mtu

Hakika, atapata maumivu ya muda mfupi tu na atapata mbadala wake na Maisha yataendelea kama kawaida
 
Kuna kuachwa kwingine unapigwa hadi bumbuwazi!akilo inaganda hadi unasahau kama ulikua na "Akiba"
Pole yake aliyeachwa atulize kichwa,atapata mwingine!mapenzi kama siti ya daladala akishuka mtu anapanda mtu
Kabisa kama kuachwa kwangu nimepigwa na butwaa
 
Nilipoachwa niliumia sana, nilihitaji walau nipate furaha kwa siku moja. Aliye niacha alifahau kabisa udhaifu wangu na alininyanyasa sana. Nilikua mpweke, dhaifu na mwenye mawazo. Hakuna aliyejua, kwaiyo niliteseka sana. Hakuna aliyenifariji, nilibaki naugulia tu.
Maumivu yalidumu kwa muda mrefu, hatimaye yaliisha.

Maisha yalibadilika, na hatimaye nikamsahau.

...Time heals...
 
Sijawahi kuachwa
natamani siku moja niachwe ili nijue ladha yake
 
Kama upo kwenye majonzi ya kuachwa tukutane hapa, na utwambie ulipoachwa bila sababu kitu cha kwanza ulifanya nini, na ulizoea hali hiyo baada ya muda gani?

Kwa kifupi mi nimeachwa jana, bila sababu ya msingi, kimoyo moyo nikajua kuna njemba litakuwa limembeba,

Ila tuwe wakweli kuachwa ni hatari sana,

Nipo nimebembeleza sana kakataa,

Nikaamua nikaushe nipo naandika uzi huu nikiwa bar nakunywa castle,



Je we umeachwa pia?
haah ukiachwa achika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom