Mkuu Lunyungu, kuhusu uwezo wa duni, uwezo mdogo na lack of confidence aliyonayo Spika, Mhe. Anna Makinda, tumeisha lizungumza sana hili!. Akidi haijatimia!, ila kwa vile wabunge wote ambao hawapo, wameomba rasmi ruksa kwa spika, hivyo ni spika ndiye anajua wako wapi, hiv yo hata kama wanaonekana hawapo physically, uwepo wao by imagination upo, hivyo wanahesabika wapo, na akidi imetimia!.Nilisema juzi juzi, hawa wabunge wa Chadema, wanatuharibia sana bunge letu!. Wanamkosesha amani spika wetu na naibu wake kwa kuwaendesha puta, hadi kukiuka/kuvunja, kupindisha na kuunda kanuni mpya kinyume cha sheria!.Nilishauri, kama Chadema wamekuwa mwiba hadi kugeuka kero, bora hiki chama kifutwe tujue moja!. Pasco.