Sophia Simba: Siasa na tendo la ndoa

Pengine hata uwaziri wetu na uongozi wetu unalenga hapo kwenye tunda tuuuuuuuuu hatuna kitu kingine cha kuwaza
 
sio yeye tu.wapo wengi wenye akiri finyu kama yeye.hana jipya, ni aibu kubwa kuwa na kiongozi km huyo.lakini zaidi anatoa picha ya JK sababu yeye ndo aliyemteua .
 
nukuu ya kunukulika:

"Naogopa kumtaja Mama huyu kama ni mkware au vipi, yaani pamoja na nafasi zake zote alizoshikilia... uwezo wake wa kifikiri hauvuki hisia na matamanio ya ngono!"
 
Hii story ilinitisha kidogo kwani jamaa aliandika bila kumung'unya maneno. Nadhani uhuru wa habari upo wa kutosha hapa nchini vinginevyo hali ingekuwa nyingine. Sasa kama hii nukuu hapa chini, nani huyo anatembeza ngono hadi anagawa uwaziri?

Lakini kwa kuwa nafasi za uwaziri zilikwisha kurahisishwa siku nyingi, bado ataendelea kutesa na kutesa, kwani ana shida gani wakati akili yake imeganda kwenye ngono na hicho ndicho kilichompa uwaziri?

Na hii siyo picha ya mteuzi wake (behind the scene)?
 
Kwenye gazeti la Tanzania Daima la tarehe 21/06/2010 mwenyekiti wa UWT na pia waziri wa Utawala bora, Sophia Simba, amewashauri wanawake ambao ni wanachama wa CCM kutowapa unyumba waume zao ambao si wanachama wa CCM.

Sasa siasa na ndoa vinaendana kweli? Huku sio kuongeza soko la machangudoa Ohio na kuchochea maambukizi ya Ukimwi? Hao ma-housegirl watapona kweli? Au ndio kasi zaidi, nguvu zaidi, ari zaidi imekwisha anza? Hivi huku sio kuvunja katiba ya nchi ambayo inatoa uhuru kwa kila mwananchi kujiunga au kutojiunga na chama chochote cha siasa?

Hivyo mume hapati unyumba mpaka aoneshe kadi halisi ya uanachama wa CCM? Basi wanaume wengi watakaojiunga na CCM muda huu itakuwa ni utekelezaji wa ushauri wa mama Simba?


sasa hapa tutaelewa kipi na kipi?
 
Ama kweli kuji-attach na CCM ni kujiweka kwenye hatari ya kupungua uwezo wa kufikiri. Huyu mama mzima kweli huyu??

Kama ndiyo wanayofundishana huko UWT basi kwisha kazi nchi yetu
 
Back
Top Bottom