Sophia Simba Alihudhuria semina Elekezi pale Ngudoto?

Serendipity

JF-Expert Member
Jan 24, 2009
486
43
Wana JF salaam!
Ama baada ya salaam, ningependa kufahamu(kukumbushwa) kama Mh. Sophia Simba alihudhuria Zile series za semmina Elekezi zilizofanyika kwa mawaziri na watumishi wengine wa juu sirikalini.(Inaonyesha kama vile hakuhudhuria)
Pili, kwa kua tunaelekea mwanzo wa mwisho wa kipindi cha kwanza kwa uongozi wa JK, je hizi semina ziliwasaidia wahusika? Na je watanzania tumefaidika na semina hizo?(kwa maana ya ufanaisi katika utendaji wa mawaziri na wakuu wengine serikalini)
Nawakilisha.
 
Sijaelewa umemtaja Sofia Simba katika title yako, umeenda mbali zaidi kuuliza ufanisi wa hii semina elekezi kwa mawaziri wote.Kwa nini swali lisingekuwa general kwa mawaziri wote ? what so special or hidden about SS?

Kamauliuliza specifically kwa SS jibu ni;

Ngurdoto sio mwarobaini wa matatizo ya uongozi,uongozi Tanzania inabidi ufundishqe kutoka ngazi ya primary, watu wajue kujua maana ya kuwajibika kuanzia katika familia zao, kuwa viranja, wakuu wa idara n.k. Tangu utotoni hata uchaguzi wa viranja tu hauko serious, ndio tabii hiyo hiyo inamfanya mtu mzima kumchagua Kikwete!

Kama umeuliza kwa mawaziri wote;

Well refer jibu la juu, lakini kumbuka SS ni mfanyakazi wa CCM na anayoyaongea anaongea kwa makusudi kabisa kutuchanganya, kamwe usije ukafikiri anaongea hajui impact yake kwa wananchi au mjinga--Usijae nyavuni kiasi hicho.SS, mAKAMBA KINGUNGE they know what they are doing.

Wiki hii ataongea Kingunge, atakuja Sofia Simba, kisha makamba, tutapoteza miezi na mwaka kuwalaani na kuwasonya hawa watu, lakini mara zote hufanikiwa kututoa kwenye reli.
 
Back
Top Bottom