Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,557
- 21,512
Mvua hiyo iliyonyesha majira ya saa tisa za mchana na kudumu kwa muda wa zaidi ya nusu saa ikiambatana na upepo mkali imeezua pia madarasa ya shule ya msingi Mipeta, kuharibu vitabu na kusababisha wanafunzi wa shule hiyo kukosa madarasa ya kusomea huku pia nyumba mbili za walimu nazo zikiezuliwa.
Wananchi waliokumbwa na maafa hayo wanasema mvua hiyo ambayo haijawahi kutokea kijijini hapo mbali ya kuezua mapaa na kubomoa nyumba zao pia imeharibu akiba yao ya mazao mbalimbali ya chakula yakiwemo Mahindi na Maharage.
Hata hivyo mkuu wa wilaya ya Songea, Bw. Pololeti Kamando Mgema amesema serikali bado inaendelea kufanya tathimini ili kujua hasara iliyojitokeza kutokana na maafa hayo huku akiwawatahadharisha wananchi kuezeka nyumba zao katika ubora unaotakiwa ili kuepukana na maafa kama hayo.
ITV