Somo zuri kwa maisha yetu

Somo zuri kwa maisha yetu

Lavan Island

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2015
Posts
2,378
Reaction score
2,057
Wanandoa waliokuwa ndio kwanza wanaanza maisha walihamia katika mtaa mmoja na kupanga nyumba katika eneo hilo,Siku ya pili wakiwa wanapata chai asubuhi mke alimwona jirani kwa mbaali kupitia dirishani akianika nguo alizotoka kuzifua.

Mke akamwambia mumewe nguo zile hazikufuliwa vizuri na hazikutakata yule mama hajui kufua nguo au anahitaji sabuni nzuri zaidi,Mme alitazama pia ila hakutamka neno zaidi ya kukaa kimya.

Ikawa kila siku yule jirani anapo anika nguo yule mama lazima angeongea neno kwani nguo bado zilikuwa zinaonekana hazikutakata.Baada ya mwezi mmoja hivi siku moja yule mama aliamka na kushuhudia yule jirani akianika nguo zilizo fuliwa na kutakata vizuri sana,bila hata ya kusubiri alimwambia mumewe.

Woow angalia mume wangu yule mama kapata somo sehem angalia alivyofua nguo na kutakata vizuri sijui nani kamfundisha.

Mme akasema nimeamka leo mapema na kuyasafisha madirisha yetu,na ndio maisha yetu yalivyo kile tukionacho kwa wenzetu kinatokana na usafi wa madirisha yetu jinsi yalivyo.

Ni rahisi kwa sisi kuongea mengi juu ya wenzetu na maisha yao ambayo sisi hayatuhusu,Na tunasahau kuwa sisi ni wachafu zaidi.
 
Wanandoa waliokuwa ndio kwanza wanaanza maisha walihamia katika mtaa mmoja na kupanga nyumba katika eneo hilo,Siku ya pili wakiwa wanapata chai asubuhi mke alimwona jirani kwa mbaali kupitia dirishani akianika nguo alizotoka kuzifua.Mke akamwambia mumewe nguo zile hazikufuliwa vizuri na hazikutakata yule mama hajui kufua nguo au anahitaji sabuni nzuri zaidi,Mme alitazama pia ila hakutamka neno zaidi ya kukaa kimya.Ikawa kila siku yule jirani anapo anika nguo yule mama lazima angeongea neno kwani nguo bado zilikuwa zinaonekana hazikutakata.Baada ya mwezi mmoja hivi siku moja yule mama aliamka na kushuhudia yule jirani akianika nguo zilizo fuliwa na kutakata vizuri sana,bila hata ya kusubiri alimwambia mumewe..Woow angalia mume wangu yule mama kapata somo sehem angalia alivyofua nguo na kutakata vizuri sijui nnani kamfundisha.
Mme akasema nimeamka leo mapema na kuyasafisha madirisha yetu,na ndio maisha yetu yalivyo kile tukionacho kwa wenzetu kinatokana na usafi wa madirisha yetu jinsi yalivyo.Ni rahisi kwa sisi kuongea mengi juu ya wenzetu na maisha yao ambayo sisi hayatuhusu,Na tunasahau kuwa sisi ni wachafu zaidi.
Aisee!
 
Nimekubali. Maana RAIA wepesi sana kujadili makosa ya wengine.

Somo nzuri sana hili
 
Ila naye hyo Dada alkuwa mmbea kwann anakunywa chai huku anachungulia dirishaniii??? hahaha


yote ya yote story nzuuri imetoa funzo
 
Ni rahisi kukosoa wenzako wakiwa uwanjani wanacheza football ila ingie wewe ucheze sasa.. kama hautakuwa KITUKO😀
NB: Ukimnyoshea mwenzio kidole, kumbuka kuna vinine vimekugeukia wewe.
 
Wepesi sana kutoa kasoro watu wengine ndivyo tulivyo binadamu. Good msg
 
Mtoa uzi umeeleweka njoo nikupe soda ila usifikiri nina chips mayai.
 
Ni rahisi kukosoa wenzako wakiwa uwanjani wanacheza football ila ingie wewe ucheze sasa.. kama hautakuwa KITUKO😀
NB: Ukimnyoshea mwenzio kidole, kumbuka kuna vinine vimekugeukia wewe.
Mkuu vp ulifanikiwa kumuoa yule dada
 
Back
Top Bottom