Somo la Ugiriki, Tanzania tujifunze

Somo la Ugiriki, Tanzania tujifunze

Mkuu ni kweli ushirikiano mara zote ni muhimu, lakini ni lazima tuwe makini.
Kulinda ajira, viwanda vyetu, uchumi wetu ni jukumu letu na hatuwezi kuliachia soko huria kufanya hivo ingawaje ushindani ni muhimu.
Hivyo basi tuhnahitaji wachumi wetu wawe wazuri sana kuona mashimo tunayoweza kutumbukia na kuvunja miguu ili tuweze kuyaepuka.

Suala la Ugiriki si utani, watu wamefikia adi kujinyonga kwa kuuziwa numba na maisha ya kistaarabu waliyoyazoea, na bado deni la taifa ni kubwa mno kiasi cha Ugiriki kuanza kuonekana kama 3rd world country.

Waingereza wale ni ligi tofauti sana, pamoja na matatizo yao yote hawajawahi hata kidogo kukubali nchi yao iingie katika Eurozone.
London bado ni a robust financial capital.
Tujikumbushe historia kidogo, hawa Wagiriki kabla ya kujiunga na sarafu ya Ulaya ya kwao ilikuwa hoi. Nakumbuka katika safari zangu n iliwahi kupitia huko na nilipofika airport na kubadilisha fedha kidogo ni kawa milionia mara moja. Lakini fedha hiyo iliniwezesha kununua Tshirt tu nikarudi kwenye "ufukara" wangu! Ninacho jaribu kusema hapa ni kuwa Wagiriki hawajawahi kwa kipindi kirefu kuwa na nidhamu ya matumizi na uchumi wao umekuwa katika matatizo muda mrefu. Ilitarajiwa kuwa wakiwa katika umoja wa ulaya watabadirika lakini haijawa hivyo. Ninakubaliana nawe kuwa lazima tuwe makini na hasa kwa kuzingatia kuwa hata sisi serikali yetu ni watumiaji kweli kweli bila nidhamu.
 
Back
Top Bottom