masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 18,621
- 14,577
Ugiriki wamefanya uchaguzi hivi karibuni, uchaguzi ambao matakwa ya wananchi walio wengi yameonyeshwa dhamira ya kujikomboa kutoka kwenye mfumo wa uchumi wa EU.
Ugiriki imefika hapo ilpofika baada ya kuingia katika mfumo wa uchumi wa European Union, itu ambacho kinalingana kidogo na kile sisi tunachokililia cha East African Monetary Union.
Kwa bahati mbaya EU Union ni mtoto wa wanasiasa , huko Ulaya, lakini kwa wajanja wa uchumi kama Uingereza waliona matatizo siku nyingi sana na walikataa kujiunga.
Kimsingi makubaliano hayo ilikuwa kutumia sarafu moja kwa nchi zote.
Mimi nimeuliza swali hili kwa wachumi jinsi ya ku-control uhamishaji wa capital kwa kutumia sarafu moja lakini sijapata jibu lenye mantiki.
Mtego uko hapa: Nchi zote zikitumia sarafu moja ni kwamba sasa soko la nchi zote linakuwa moja.
Dis advantage yake ni kwamba hata zile nchi ambazo uchumi wake ni hafifu na hauwezi kushindana na nchi tajiri katika soko hilo ,wanaishia kununua vitu/bidhaa/huduma zilizo bora zaidi kutoka nchi zenye uchumi mkubwa.
Kwa mfano, kama kuna kigari kinatengenezwa Ugiriki, na Ujerumani. Mgiriki atadunduliza kununua gari bora zaidi la kijerumani kuliko lile hafifu la kigiriki.
Matokeo yake ni kwamba fedha toka Ugiriki zinahamishwa , tena kwa wingi tu, kwenda Ujerumani, wapende wasipende.
Baada ya muda utakuta kile kiwanda cha magari cha Ugiriki kinakufa kwa kukosa wateja, na watu wanakosa kazi.
Hili ndio tatizo lililotokea kwa uchumi wa Ugiriki.
Leo ,Tanzania tukianzisha umoja wa sarafu, au sarafu moja ya East Africa , hicho ndicho kitatokea-uhamishaji wa liquid capital en masse kuelekea Kenya.
Huu si utani, tusome alama za nyakati, wenzetu wagiriki wakinyolewa sisi tutie maji.
Ugiriki imefika hapo ilpofika baada ya kuingia katika mfumo wa uchumi wa European Union, itu ambacho kinalingana kidogo na kile sisi tunachokililia cha East African Monetary Union.
Kwa bahati mbaya EU Union ni mtoto wa wanasiasa , huko Ulaya, lakini kwa wajanja wa uchumi kama Uingereza waliona matatizo siku nyingi sana na walikataa kujiunga.
Kimsingi makubaliano hayo ilikuwa kutumia sarafu moja kwa nchi zote.
Mimi nimeuliza swali hili kwa wachumi jinsi ya ku-control uhamishaji wa capital kwa kutumia sarafu moja lakini sijapata jibu lenye mantiki.
Mtego uko hapa: Nchi zote zikitumia sarafu moja ni kwamba sasa soko la nchi zote linakuwa moja.
Dis advantage yake ni kwamba hata zile nchi ambazo uchumi wake ni hafifu na hauwezi kushindana na nchi tajiri katika soko hilo ,wanaishia kununua vitu/bidhaa/huduma zilizo bora zaidi kutoka nchi zenye uchumi mkubwa.
Kwa mfano, kama kuna kigari kinatengenezwa Ugiriki, na Ujerumani. Mgiriki atadunduliza kununua gari bora zaidi la kijerumani kuliko lile hafifu la kigiriki.
Matokeo yake ni kwamba fedha toka Ugiriki zinahamishwa , tena kwa wingi tu, kwenda Ujerumani, wapende wasipende.
Baada ya muda utakuta kile kiwanda cha magari cha Ugiriki kinakufa kwa kukosa wateja, na watu wanakosa kazi.
Hili ndio tatizo lililotokea kwa uchumi wa Ugiriki.
Leo ,Tanzania tukianzisha umoja wa sarafu, au sarafu moja ya East Africa , hicho ndicho kitatokea-uhamishaji wa liquid capital en masse kuelekea Kenya.
Huu si utani, tusome alama za nyakati, wenzetu wagiriki wakinyolewa sisi tutie maji.