Wanachojivunia wanasiasa wa Tanzania ni upumbav.u na ujing.a wa wapiga kura wa taifa hili......
Tanzania ina wapiga kura ambao huwezi kuwapata sehemu yoyote ile duniani.....ni wapiga kura ambao uwezo wao wa kufikiri na kuchanganua mambo ulishakufa kitambo....bali vichwa vyao vimebaki kuwa kama maboksi ya kuhifadhia propaganda za wanasiasa wachumia tumbo.......
Ni rahisi sana kuwa mwanasiasa hapa nchini kwani hauhitaji kuwa na hoja nzito na mikakati ya kimaendeleo dhidi ya wapinzani wako.....bali unachohitaji ni kuibua kashfa na matusi dhidi ya mpinzani wako basi una uhakika wa kuzoa kura kutosha........
Haikuhitaji kuwa na ajenda kuu za maendeleo pindi utakapochaguliwa bali ni kungoja matukio na kwenda nayo sambamba.......
Kwa mujibu wa moja ya nukuu za baba wa taifa....ili taifa liendelee moja kati ya nguzo imara ni siasa bora.....kwani kupitia siasa bora ndipo tunapata viongozi wenye dira na maoni ya kuweza kuliendesha vyema gurudumu la maendeleo ya taifa letu kutokana na mikakati yao ya kimaendeleo.........lakini kwa kutazama hata kwa jicho moja tu....utagundua kuwa tumeshafeli kwenye kipengele cha siasa bora na ndio ulipo mzizi wa matatizo yetu........
Unategemea taifa litapigaje hatua kama tunawachagua wezi na vibaka kulinda hazina kuu......
Taifa litapigaje hatua kama tunawapima wagombea kwa uwezo wao mkubwa wa kuwatukana wapinzani wao na kuibua kashfa zao na sio kwa mikakati yao kwenye kuliinua taifa hili.....!??
Nasisitiza tena ujing.a na upumbav.u wa wapiga kura wa taifa hili ndio msingi au mtaji wa wanasiasa wetu kwa manufaa yao....na ndio tiketi ya umaskini na ufukara kwenye taifa hili......
MUNGU IBARIKI TANZANIA

.

.