Socialist party of Tanzania

Tupo pamoja katika hilo, nitakuwa mwanachama namba mbili baada ya wewe, lakini iwapo Azimio La Arusha litafanyiwa marekebisho kidogo/machache sana. Tunahitaji chama cha namna hiyo.

Mkuu ujamaa ni sawasawa na ubepari i.e. ujamaa=ubepari

Wakati ujamaa wanaomiliki mali ni serikali (theoritcally) lakini in fact wanaomiliki ni viongozi wa chama au walio na madaraka

Ubepari wanaomiliki mali ni kampuni binafsi (watu wachache) in fact lazima wawe na uhusiano mzuri na wenye madaraka

Ujamaa ni siasa za kale ambazo hazina tija kwa nchi na watu wake; muhimu tuangalie something between those "extreme opposite sides"
 
 
Style ya utawala wa China sio .. full kunyongana matajiri wa kichina wamekimbia inchi wengi waishi Canada .... Sidhani kama watu flani flani watakubali
 

labda hujui tu, kilichofanya uhisi umesoma bure ni equal distribution of resources. umewahi kujiuliza hizo pesa mlizokuwa mnapewa kama nauli, chakula na mavazi, malazi na matibabu zilikuwa zinatoka wapi? acha umbumbumbu open ur mind elewa ujamaa na sio kulewa ujamaa
 

Source za hizo pesa zilikuwa
1.Kodi za mapato.Tanzania ilikuwa iko kati ya nchi zenye viwango vya juu sana vya kodi ili kuhakikisha mwenye nacho anachangia sana tu kikodi kumsaidia asiyer nacho kwa njia ya kodi ili wote wainuke.Hicho cha juu kilipelekwa kumsaidia maskini asome bure
2.Mgao wa faida toka mashirika ya umma yaliyokua yamezagaa nchi nzima na kila sekta
3.Mikopo ambayo serikali ilikuwa inahangaika kukopa na kukopa sana tu siyo ili wafisadi bali wawajengee uwezo wananchi wake wasikokuwa na uwezo kwa kuwasomesha bure
4.Misaada toka kwa wahisani ilipoletwa ilikuwa ikitumiwa vizuri mno hasa kwenye sekta ya elimu.Nyerere alikuwa akienda huko na huko kuomba asomeshe wanawe watanzania na wengi ziliwafikia wakafaidi hadi wale waliozaliwa maporini kwenye mangedere na umaskini wa kutupwa wakasomeshwa hadi kuwa maprofesa na watu wa kuaminiwa duniani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…