Social Networking/Mitandao ya ki-Jamii...


Mbu mi nawapa mbinu ya kukwepa "mbona X kaLIKE picha uliyopiga beach mwenyewe ila hajaLIKE ile tulopiga wote?Mbona anaomba ujibu msg yake au muende 'inbox' kama wanavyoitaga wenyewe" na nyingine kama hizo.

Ni sawa tu na yale masharti usiguse simu yangu, usipokelee mbali, usifute msg.

Mambo ya ndani yamekua sio ya ndani tena aisee. Unakuta mtu kaandika kabisa "tonight i'm getting some". . . sasa jiulize wewe kama ndio X wake, mfanyakazi mwenzake au rafiki tu inakuhusu? Watu wanaruhusu hii mitandao iwafanye vichaa.
 
Reactions: Mbu

...hahahaha, huyo anayeandika atananihii usiku huenda anamrusha roho 'mgombea mwenza!'...
ila ndio kama unavyosema, kwa faida ya nani?
 

...hahahaha, huyo anayeandika atananihii usiku huenda anamrusha roho 'mgombea mwenza!'...
ila ndio kama unavyosema, kwa faida ya nani?

Yani, ni kaaazi kweli kweli.
Kuna mmoja nimeona kaandika leo hata kurudia kusoma sitaki, sasa sijui watu wanaomheshimu/anaowaheshimu watamchukuliaje baada ya kuandika alochoandika. It's kinda sad. . . watu wanakua malimbukeni bila hata kujua.
 
Reactions: Mbu
twitter hata matumizi yake magumu.
facebook unakuwa na friends 5000 na zingine pendings yaani unafans sawa na msanii mwenye jina tz

....almuradi ni usanii mtupu, mtu ana update, "najiskia mpweke, mume wangu leo kasafiri....!"
enzi zile za miaka ya 47 kauli kama hizi ni kukaribisha wezi tu kwako...leo hii inakuwa ni coded msg kwa
midowezi, yupo available.
 
Yani, ni kaaazi kweli kweli.
Kuna mmoja nimeona kaandika leo hata kurudia kusoma sitaki, sasa sijui watu wanaomheshimu/anaowaheshimu watamchukuliaje baada ya kuandika alochoandika. It's kinda sad. . . watu wanakua malimbukeni bila hata kujua.

Angalau jf ni
where we dare to talk openly, huko kwingine labda wanafuata msemo huu;

"Be who you are and say what you feel because those who mind don't matter and those who matter don't mind."
 

..hah? kiongozi hivi kuna umuhimu kumjua sijui kumfahamu ex wa mke/mume?
sasa wale one night stand utawa block vipi nao? nao wamo hao...

...Huwezi kublock 100% lakini pale ambapo unaweza kublock basi sioni sababu ya kutofanya hivyo. Kumbuka kuna mahusiano mengi tu yameshavunjika kupitia Twitter, FB, Skype, emails na upuuzi mwingine. Sasa ili nawe usije kuongeza statistics za walioathiriwa na technology katika mahusiano basi unapoona jambo halikukaa sawa sidhani kama ni vyema kunyamaza kimya bila kutia neno.

 
Reactions: Mbu

Angalau jf ni
where we dare to talk openly, huko kwingine labda wanafuata msemo huu;

“Be who you are and say what you feel because those who mind don't matter and those who matter don't mind.”

Hhahahahaha. . . . haya bana.

BAK Xs wengine wanaweza wakawepo kwenye friends list na wasilete matatizo, wengine wanaweza wasiwepo na wakaleta matatizo. Alafu kumchunga sana mtu ni kazi ya ziada, sidhani kama hiyo nayo inatakiwa iwe kwenye "mahusiano package". . . watu wanatesana tu bure.
 

...aiseee,

wazee wetu wa walijikinga na boma tu ndoa zao zikasalimika,
sie leo tumeyakaribisha haya ya utandawazi,....mtu ana flirt kwenye mtandao
mpaka pembeni yako kitandani!
 
Reactions: BAK
Nakubaliana nawe Lizzy lakini ni vigezo gani vitatumika Xs hawa hawafai kuwepo na wale wanafaa kuwepo? si ajabu hao waliobaki ndio hao wanajipitishapitisha kujaribu kumdowea mwenye mali 🙂🙂... Hii kitu ni ngumu sana kusema kweli 🙂🙂 ukiwa na wivu wa kufa mtu unaweza kupata uchizi 🙂🙂


 
.....Mhhhhh! We unakoroma kumbe kuna njemba linazengea lol! na wewe uko hapo hapo 🙂🙂





...aiseee,

wazee wetu wa walijikinga na boma tu ndoa zao zikasalimika,
sie leo tumeyakaribisha haya ya utandawazi,....mtu ana flirt kwenye mtandao
mpaka pembeni yako kitandani!
 
Last edited by a moderator:

Mwenye X ndie anaetakiwa kujua BAK. Yani kama mtu anajua X wake ni msumbufu,amewahi kumsumbua, hajatulia n.k asimuadd au amdelete bila mwenzake kumtaka fanye hivyo. Yani tusiwe kama watoto kila kitu mpaka mmoja aagize/alazimishe, tutumie common sense. Kama ambavyo hua tunawapotezea marafiki ambao tunaona hawatufai.
 

..hhaaa?!

...hivi hujui kuna vichwa panzi wengine wanajua kwa idadi kubwa ya admirers na ex-'wapenzi' wanaokumbushana enzi zao online ndio naye anajijengea heshima na adabu (boost self esteem) kwa mume/mke'we hapo nyumbani?

...acheni nyie, hii mitandao hasa facebook inawakomoa wengi majumbani....refer post za Nyani Ngabu pale unapokuta mwenza anakataa kuku-accept friendship request, au akishaku add kuna post anakunyima access, au anaku delete!
 
Reactions: BAK

Nakubaliana nawe Lizzy lakini tukumbuke kwamba common sense in not so common :rant:
 
Reactions: Mbu

Najua Mbu, ila kama mtu kuboost hiyo self-esteem mpaka X ahusishwe basi ana hasara. Hiyo inatakiwa iwe kazi ya mwenzi, kila mmoja amuongezee mwenzie kujiamini.

Naona dalili za kumuendea mtu BWAGAMOYO nikamtengeneze ntakavyo. . . . lolzz. . . maana mambo ya kuchungana mpaka usiku wa manane (asichat, txt na ongea na simu) sitoweza kwakweli.
 
Reactions: Mbu

Hii kazi ya kukimbizana na vivuli siyo mchezo,

Honestly kazi ngumu kuifanya hata kwa malipo...

Jambo la muhimu ni kukubaliana mambo ya msingi kama alivyosema RR na kumwachia kila mtu ajichunge...Ila pia ni vizuri kuweka mstari ambao mtu akishauvuka ajue matokeo yake hata bila kuulizwa!!
 
Reactions: Mbu

....amaaa? sasa ilikuwaje mke nae aende utangazia ulimwengu, ndoa yake i mashakani?
mimi tatizo langu linaanzia hapo bana....

Unajua hata Mungu alisema nawapenda wale wanipendao, wasionipenda out! sasa wewe ndoa yako mnalala vyumba tofauti unaanzaje kujiita married wakati mko separate kidizaini?

Ki ukweli mimi kama mimi siwezi kuishi na mtu asiye na maendeleo au msaada kwangu. Kwa mfano mke na mume wanaunganishwa na Tendo la ndoa, achana na mambo mengine ya ki ulimwengu. Sasa kama hilo tendo la ndoa hutoii au hupati unaishi na mtu wa hini? unamwandikaje kwenye facebook married?

Haya wenye ndoa zao watwambie, manungayembe kimyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!
 
Reactions: Mbu

...hahahaha, ndilo lililobakia, ...kulishana limbwata na kutegeana tego tu!



....kwa tafsiri ya maisha ya kileo status hiyo inaitwa OPEN RELATIONSHIP, au cheat responsibly :A S-coffee:
 

...hahahaha, ndilo lililobakia, ...kulishana limbwata na kutegeana tego tu!




....kwa tafsiri ya maisha ya kileo status hiyo inaitwa OPEN RELATIONSHIP, au cheat responsibly :A S-coffee:

Kaka,

Mtu mzima na akili zake timamu hafugiki hata kwa kutumia majeshi yote ya ulinzi na usalama!!

Labda kama unataka kuwa kichaa bure!!

Babu DC!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…