MWANASIASA HURU
Senior Member
- Oct 4, 2012
- 180
- 245
Ndo maana mnaambiwa muwe na kifuaa, wanawake wa siku hizi anaweza kutongozwa na shemej mtu au hata baba mkwe anasema kwa mume we akifikiri anajenga kumbe ndo anabomoa moja kwa moja, mitandaon a napata kipi cha maana like na comment? Mbona hii mitandao imekuja kivingine sasaMwanamke akiwa na matatizo ya ndoa atatafuta mtu wa kumwambia tu, either mama yake, dada, rafiki au huko kwenye social media. Sasa ni ule wakati mmeshayamaliza matatizo yenu, mama anakumbusha si alifanya hivi na vile, unajuta kwanini nilisema.
Lakini issue ni hiyo tu bro au na wewe hukumpenda kivileee heb eleza ukwel
Hahahahaha aisee umeongea kitu cha msingi sana
Wanawake wa siku izi sijui ni nini kimewakuta yani asilimia 70 ni matatizo matupu,mimi wa kwangu nlitumbua na mimba ya kujifungua leo au kesho maana ni upuuzi sasa,unakaa na lijitu uko ndani lipo kama shetani.Sikiliza jamaa yangu kuwa kama mwanaume unayejielewa mbona issue hiyo mdogo Sana mnyang'anye hiyo smart phone halaf mnunulie simu ya kawaida na onyesha uko serious aache ujinga ukiona kama bado haeleweki mrudishe kwako akawaambie wazazi wake kuwa Facebook ndo iliyomuoa atabadilika, huo ujinga unashindwaje kumcontrol ubavu wako bwana bila usimpige ndoa nzuri ni ile ambayo kila mmoja anajitahidi kutafuta furaha ya mwenzake sasa yeye kuweka mambo ya ndani mtandaoni unaona like na comment zitamsaidia kutunza ndoa yake ujinga huo
Yaani sijui nini kimewapata mitandao wameipokea vibayaWanawake wa siku izi sijui ni nini kimewakuta yani asilimia 70 ni matatizo matupu,mimi wa kwangu nlitumbua na mimba ya kujifungua leo au kesho maana ni upuuzi sasa,unakaa na lijitu uko ndani lipo kama shetani.
Ni changamoto kubwa sana!Yaani sijui nini kimewapata mitandao wameipokea vibaya
MKE WAKE ASHAAMBIWA MARA NYINGI BADO HASIKIIIUnataka Acha mke kisa Facebook tu??angalia hayo madongo ni Yapi,ana maumivu ya kihisia probably, muweke karibu mke yapaswa umjali na ajue unampenda, then mweleweshe tu upya asiweke ishu zenu huko
Pia na wewe mara moja moja si mbaya kumuweka mkeo watsap na fb,tafta picha kapendeza muweke mtag, caption hata ndogo tu 'my wifey' inatosha kumpa raha ajijue unampenda, to her anaamini kuwekwa mitandao ya kijamii ni mapenzi
Ila grow up mke haachwi kirejareja hivo
Waungwana kila siku tunasema mwanamke ni tabia, ni nyie huwa wakwanza kupinga na kudai mwanamke tako, tabia tutavumikiana, sasa vumilieni tu hamna namna.
Nafikiri hakuna situation ambayo inafanya mtu mzima na akili yake aweke family matters kwenye public walls. Kuna mambo we disagree kabisa lakini mazungumzo ni priority number one. Maana mtu anapoamua kubehave immaturely hapo ndo shida inaanza. Kwanza haijengi zaidi ya kubomoa. Maana hata kama kulikua na masikilizano kidogo inaua kabisa hata hio kidogo. Pili, hata kama kulikua na mapenzi nayo yanakufa. Situation inakua mbaya kuliko mwanzo, ndio maana wahenga wanasema ziba ufa kabla hujajenga ukuta. Nafiri nidhamu kwanza mengine baadae. Hata kama unakereka ni vizuri ukatumia heshima kuwasilisha ujumbe wako. Hakuna mume anaejitambua atakusikiliza kama humuaproach kwa heshima.
Kabla ya kumuoa hukujua kuwa napenda attention hasa hizo za social networks?
Dawa naona kaka naye kwanza mzungumze mueleza vitu usivyovipenda cos ingawa kasi ya watoto kulelewa na single parent inaongezeka kwa kasi asikwambie mtu iyo situation ina impacts flani kwenye maisha ya hao watoto ,THINK TWICE BRO Mungu akupe busara ufanye maamzi sahihi pole
Huwa Sijui ni ulimbukeni wa mtandao au ni ukichaa wa mtandao.
Believe me mkuu tupo wengi sana tunaokerwa na hiyo tabia.
Ni upuuzi, ila sasa na wewe dawa yake ni ndogo.
Unfriend fb-Good umeshafanya
Viber na wassap hapo vyote vya nini!?
Jitoe Viber, ubakize wassap
Wassap fanya setting ambayo haitaonesha dp na status yako ambayo automatically na za wenzako hutaziona ikiwemo mkeo
Utaacha wangapi, hapo shukuru Mungu hujakutana na story inayokuhusu wewe humu jf.
Hata hii thread ni dongo kwa mkeo kupita jf.
Nafikiri anza na plan A kwanza mnyang'anye hiyo simu mnunulie hizi za kawaida swala lakuachana iwe ni option ya mwisho baada ya hili kushindikana.Wakati namuoa hata hakuwepo kwenye social networks kabisa, enzi hizo alikua na simu mchina ya tochi.