Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,804
- 1,871
Kama kura za uraisi zingekuwa zinapigwa kupitia mtandaoni na kujumuisha wapenda mtandao tu, na hasa kama JF ndio ingekuwa ni kituo pekee cha upigaji kura, basi Slaa angeshinda kwa kishindo. Hilo lingewezekana kama tu tungefikiria kuwa idadi ya wapiga kura wote Tanzania hawazidi elfu 10.
Lakini hiyo ni ndoto tu kwani hali halisi ni nyingine kabisa katika viwanja vya mpira kule Ulyankuru, Sekenke na maeneo mengine yafananayo na hayo Tanzania. Kiujumla tamko sahihi ni kwamba, Kikwete ni mzito sana kwa Slaa. Slaa angegombea wakati wa Mkapa ungekuwa wakati Muafaka, lakini safari hii kajiua kisiasa au pengine kakiua chama kizima kisiasa. Lau kama angesubiri mpaka 2015 angeweza kuambulia chochote, lakini kushindwa kwake mwaka huu kutamshushia hadhi yake hata 2015 kama ilivyokuwa kwa Mrema 1995 na kulamba dume 2000.
Kuna sababu tatu kuu zitazomuangusha Slaa; Kikwete kamaliza matatizo ya kimsingi ya Mtanzania ikiwa pamoja na usalama wa Raia na mali zake. Pili matatizo ya ujambazi yaliyokuwa yanawakera watanzania tokea Boko mpaka wasafiri wa mabasi mikoani ameyaondoa kabisa. Tatu kaondoa tofauti za wananchi kivyama au kaviunganisha vyama kwa kuelewa kuwa mpinzani wako si adui yako bali ni rafiki yako unayoweza kukaanaye na mkala sahani moja. Kuchaguliwa kwa akina Kabwe kushiriki katika kamati ya madini ni moja ya miujiza aliyoifanya Kikwete. Hata akisafiri haishi kuwachukua wapinzani katika misafara yake huko Ughaibuni. Sijakueleza maswala ya Muafaka alivyoyapeleka mpaka kafika kituoni BILA HATA VIONGOZI WA WAPINZANI KUTIWA NDANI. Kifupi hakuna mpinzani aliyetiwa ndani mwaka huu. Uhuru wa kusema ndio sikwambii, hata akina zawadi Ngoda eti leo wanaandika bila woga wowote ule.
Hayo na mengine mengi, yamefanya hata uchaguzi wa mwaka huu kutokuwa na mfuto sana, kwa kila mtanzania anajua kuwa katika nafasi ya uraisi Slaa ni msindikizaji tu. WanaCHADEMA wote wanafahamu kuwa hapo wamepoteza kiti cha Ubunge, na hii itawagharimu sana CHADEMA SIKU ZIJAZO.
Panga pangua, Slaa hawezi kushinda kwa vile zaidi ya kujiita Dr hana sifa kama zile za Kikwete. Kikwete kashika nafasi nyingi serikalini na jeshini, je Slaa ana nini la kutuambia. Kutosoma alama za nyakati ndiko kulikompotosha Slaa au CHADEMA kwa ujumla. Washauri wake hawakumchagulia wakati muafaka kwake kugombea uraisi. Pengine wamemtosa kistile. Mkaidi hafaidi mpaka siku ya IDD, lakini je siku ya Idd kwa Slaa imefika? Hilo ni swali ambalo kila mwana CHADEMA ajiuliza.
Lakini hiyo ni ndoto tu kwani hali halisi ni nyingine kabisa katika viwanja vya mpira kule Ulyankuru, Sekenke na maeneo mengine yafananayo na hayo Tanzania. Kiujumla tamko sahihi ni kwamba, Kikwete ni mzito sana kwa Slaa. Slaa angegombea wakati wa Mkapa ungekuwa wakati Muafaka, lakini safari hii kajiua kisiasa au pengine kakiua chama kizima kisiasa. Lau kama angesubiri mpaka 2015 angeweza kuambulia chochote, lakini kushindwa kwake mwaka huu kutamshushia hadhi yake hata 2015 kama ilivyokuwa kwa Mrema 1995 na kulamba dume 2000.
Kuna sababu tatu kuu zitazomuangusha Slaa; Kikwete kamaliza matatizo ya kimsingi ya Mtanzania ikiwa pamoja na usalama wa Raia na mali zake. Pili matatizo ya ujambazi yaliyokuwa yanawakera watanzania tokea Boko mpaka wasafiri wa mabasi mikoani ameyaondoa kabisa. Tatu kaondoa tofauti za wananchi kivyama au kaviunganisha vyama kwa kuelewa kuwa mpinzani wako si adui yako bali ni rafiki yako unayoweza kukaanaye na mkala sahani moja. Kuchaguliwa kwa akina Kabwe kushiriki katika kamati ya madini ni moja ya miujiza aliyoifanya Kikwete. Hata akisafiri haishi kuwachukua wapinzani katika misafara yake huko Ughaibuni. Sijakueleza maswala ya Muafaka alivyoyapeleka mpaka kafika kituoni BILA HATA VIONGOZI WA WAPINZANI KUTIWA NDANI. Kifupi hakuna mpinzani aliyetiwa ndani mwaka huu. Uhuru wa kusema ndio sikwambii, hata akina zawadi Ngoda eti leo wanaandika bila woga wowote ule.
Hayo na mengine mengi, yamefanya hata uchaguzi wa mwaka huu kutokuwa na mfuto sana, kwa kila mtanzania anajua kuwa katika nafasi ya uraisi Slaa ni msindikizaji tu. WanaCHADEMA wote wanafahamu kuwa hapo wamepoteza kiti cha Ubunge, na hii itawagharimu sana CHADEMA SIKU ZIJAZO.
Panga pangua, Slaa hawezi kushinda kwa vile zaidi ya kujiita Dr hana sifa kama zile za Kikwete. Kikwete kashika nafasi nyingi serikalini na jeshini, je Slaa ana nini la kutuambia. Kutosoma alama za nyakati ndiko kulikompotosha Slaa au CHADEMA kwa ujumla. Washauri wake hawakumchagulia wakati muafaka kwake kugombea uraisi. Pengine wamemtosa kistile. Mkaidi hafaidi mpaka siku ya IDD, lakini je siku ya Idd kwa Slaa imefika? Hilo ni swali ambalo kila mwana CHADEMA ajiuliza.