nasri, wewe huijui tanzania vizuri! Hivi ni sehemu gani hamna raslimali kama unavyosema? Kanda ya kati kuna dhahabu, uranium, chuma e.t.c. Kusini kuna mafuta, gesi, dhahabu, n.k. Kaskazini hivyohivyo nchi yetu hamna kanda maskini kama unavyofikilia maskini ni mawazo yetu tuu
"Now or Never".
Kutokana na mapitio ya maoni yafauti taliyotangulia, ninachokiona hapa ni kuwa bado CCM wameganda katika sera za Chama kushika Hatamu bila ya kujali kuwa kuanzia 1992 CCM haina mamlaka ya Tanzania yote.
Kama watu kadhaa humu wanavyokuwa wanadhihaki lakini ndio ukweli, CCM ni janga la Taifa.
Ndugu zangu, hii ni fursa ya mwisho kwetu kama Watanzania na wala sio kama wanasisiemu, kuhakikisha tunaandika yetu inayotokana na maoni ya wengi. Vyenginevyo, hiyo kejeli inayosemwa kuwa CCM ni janga kwa taifa itakuja kuwa kweli pale tutakapowaachia kufanya watakavyo. TusipotahadhCCari patakuja kuchimika hapa. Miaka 50 ya kuburuzwa inatosha.
MTU HAWEZI KUKUPANDIA MGONGONI IKIWA HUKUINAMA - Tusiwaruhusu zaidi CCM kutupandia migongoni.
Heshima Mkuu!Hatamu hakuna tena, mjadala unarudi kwa wananchi, ieleweke hii ni katiba mpya. Hakuna mwenye haki ya kuhodhi mjadala, hata wabunge wa CCM wamekiona cha moto. Na bado, inawezekana ukarudi bungeni kwa marekebisho. Mwisho tunataka maoni ya wenye nchi (Umma) yaheshimiwe. Kwa upande mwingine tujitahidi kusoma historia iliyojificha, itatusaidia.
Heshima Mkuu!
Ninakubaliana na wewe na wengine wengi juu ya kile "Tunachokita", lakini kwa bahati mbaya, kilichopo ni kile "Tulichopewa". Naomba upitie thread ya Mwanakijiji ambapo inaonesha kuwa Watanzania tumepitishwa katika uchochoro usio na pa kutokea. Bado naamini kuwa tunaweza kubadilisha hili, sio kwa kushiriki japo kwa wingi katika kutoa maoni kwani maoni yetu yanaweza kuwekwa upande na kutumikia matakwa ya CCM, bali kuupinga mchakato huu hivi sasa katika Mahakama ya Katiba kabla haijafikia hiyo hatua ya katiba kupitishwa.
Hansen, fanya utafiti kwanza kuhusu miundo na uendashaji wa serikali za majimbo.nimekuelewa kuwa una kero kubwa kuhusu ukanda fulani kuwa tajiri zaidi kirasilimali na kwamba kipato kitokanacho na rasilimali hizo kitaishia kuendeleza ukanda huo.Lakini,kama moja ya provisions za katiba itatamka kwamba (kwa mfano) asilimia 50 ya pato la jimbo itakwenda federal govt,na iliyobaki state/provincial govt,shida iko wapi?pato litakalo kwenda federal govt litakuwa linaelekezwa kwenye majimbo yanayohitaji support kujiendeleza,kama jimbo lako kwa mfano!kwa karne zote za serikali ya jamhuri mbona kanda flani bado ziko nyuma?mbona serikali za majimbo katika Marekani zimeendelea sana kwa mfumo wa state govt kama tunaohitaji?Penda usipende,hakuna mtawala yeyote mtakaeletewa ambae sio mzaliwa wa ukanda wenu ambae atakuwa na uchungu wa rasilimali zenu,matumizi yake na maendeleo mnayoyataka kama mtawala mzawa wa jimbo lenu na aliyepewa dhamana na wanajimbo lenu na hivyo kuwajibika kwenu.Lakini la msingi sana ni kwamba mtakuwa na fursa ya pekee ya kumchagua governor wa jimbo lenu kwa sifa mnazozitaka wenyewe.kwa mfano uzawa wake,vision yake kwa jimbo LAKE, mikakati yake kwa jimbo LAKE, na mengineyo mengi kwa jimbo LAKE.Lakini pia,huyu kiongozi atakuwa accountable kwa wanajimbo waliomchagua!na siyo kwa mtu fulani mmoja.Faida za kuwa na serikali za majimbo ni nyingi sana!Kama taifa,tume-centralize sana power & authority.na ndiyo maana mfumo huu unachelewesha maamuzi muhimu na ya haraka katika kanda.rasilimali za taifa letu zinapotea kwa sababu ya wanaotakiwa kuzilinda kutokuwa na uchungu nazo kwa sababu ama siyo wazawa na au wanawajibika kwa mtu fulani na sio wanajimbo au kanda!msipotoshwe na kuchoshwa na propaganda za chama kilichotufikisha kwenye umaskini tulionao.abject poverty.FIKIRIA,CHUKUA HATUA!
Wapi? Mbona unaishia njiani?
Kwani NIGERIA HAWANA SERIKALI ZA MAJIMBO? Mbona hayo majimbo yanataka kujitenga? Mbona Jos ambako kuna mafuta wanataka uhuru?
Au unamaanisha CONGO? Au Kenya? Au Angola? Ambako Cabinda hainufaiki na mfuta yake?
Mkuu ukizungumzia majimbo, usifananishe United States na hizi nchi zetu za Africa, wenzetu wameanzisha hayo majimbo from scratch, na majimbo yalipotaka kujitenga ilibidi wauane sana!
Ni rahisi sana kusema HAYA MAMBO HAYAWEZI KUTOKDEA TANZANIA
"Muungano ni kama koti joto likizidi unalivua" Ni kawaida kwa binadamu wenye akili timamu kila linapotokea tatizo la kutokuelewana katika jamii au baina ya watu wawili njia pekee ya kuleta maelewano baina yao ni kukaa chini na kulizungumza tatizo lao kwa maana ya kutaka kulipatia ufumbuzi na shuluhisho la kudumu ili katika siku za baadae lisitokee tena. Kwetu sisi tuna tatizo Wazanzibari wanasema kwa uwazi kabisa kuwa kuna kasoro katika muungano wetu japo Watanganyika tuliowengi hatusemi kwa nguvu kama wenzetu wa Zanzibar lakini kasoro zipo na tunaziona.Kwa kulitambua hilo ndio maana hata serikali ya JMT imeunda idara maalum chini ya ofisi ya makamu wa rais ili kushughulikia kero za muungano. Sasa kama tunatambua kuwa zipo kero kwani zisijadiliwe na wananchi ambao ndio wenye muungano?
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ameeleza kushtushwa na kauli ya Rais Jakaya Kikwete inayolenga kuzuia wananchi kujadili kuhusu Muungano wakati wa mchakato wa marekebisho ya Katiba.
Dk. Slaa aliye katika ziara ya kichama kukagua uhai wa chama hicho ikiwa ni pamoja na kukijenga, alitoa dukuduku lake hilo jana wakati akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shycom, mjini Shinyanga.
Katibu mkuu huyo wa CHADEMA alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja tu tangu Rais Kikwete alipowaapisha wajumbe 30 wa Tume ya kukusanya maoni ya Katiba mpya inayoongozwa na mwanasheria na mwanasiasa anayeheshimika, Jaji Joseph Warioba.
Wakati akizindua tume hiyo juzi, pamoja na mambo mengine, Rais Kikwete alisema tume hiyo katika kazi yake haitahusika katika kuhoji kuhusu kuwapo ama kutokuwapo kwa muungano.
Kwa upande wake Dk. Slaa aliwataka Watanzania kuachana na maneno ya watawala na kutobweteka baada ya kuundwa kwa tume hiyo ya Jaji Warioba.
Jamani Watanzania wenzangu wa Shinyanga, naomba tuzungumze kidogo hili la Katiba mpya, kwanza nawaomba msibweteke eti kwa sababu tume imeundwa, kuundwa tume hakuleti katiba mpya na bora. Pia tunataka Kikwete ajue kuwa Watanzania hawatengenezi katiba ya Kikwete wala ya CCM. Wanataka Katiba mpya na bora ya kwao.
Nami namuomba ni bora akajitahidi kujiepusha na matamko ya ajabu, maana anaendelea kutupatia ajenda. Anasema suala la muungano lisijadiliwe wakati wa mchakato wa utoaji maoni. Hapa anataka kutuma ujumbe gani alisema Dk. Slaa na kushangiliwa.
Akiuchambua muungano, Dk. Slaa alisema ni haki ya Watanzania kwa maana ya wale wa Zanzibar na wa Bara kujadili muungano wanaoutaka kwani kufanya hivyo hakuna nia ya kuuvunja.
Sisi CHADEMA tunasimamia nini? Tunataka Watanzania wajadili wanataka muungano wa aina gani, tunataka Zanzibar ipate haki zake kama ilivyokuwa mwaka 1964.
Hapa hoja si muungano uwepo ama usiwepo, hoja ni aina gani ya muungano wa kisiasa Watanzania wanautaka. Tunaamini kuwa hakuna mwanasiasa mwenye akili timamu anaweza kuhubiri kuvunja muungano.
Mwanasiasa anayezungumzia kuvunja muungano huyo ni mwendawazimu, maana muungano wa kweli wa Watanzania uko kwenye damu zao. Lakini katika suala la kiutawala wananchi waachwe waamue wanataka aina gani, hii ndiyo hoja hapa, alisema Dk. Slaa.
Akifafanua, Dk. Slaa alisema wanazo taarifa kwamba tayari CCM kupitia katika Halmashauri Kuu yao ya Taifa wameshafikia hatua ya kuwatumia makada wao, wakiwamo viongozi wa kiserikali kama wakuu wa mikoa na wilaya katika kuhakikisha yale ambayo chama hicho tawala kinayataka, yanaingizwa katika Katiba mpya.
Napenda kumwambia haya huku akijua kuwa, mkononi kwangu au ofisini kwetu tayari tunao uamuzi wa Halmashauri Kuu ya chama chao, ambayo imewaagiza viongozi ambao ni makada wao, kuhakikisha masuala ambayo chama hicho kinataka yanaingia katika Katiba mpya, hii ni hatari, alisema Dk. Slaa.
Akifafanua, alisema chama hicho kitaendelea kuwa mstari wa mbele kuwaongoza Watanzania waandike Katiba mpya inayozingatia haki za msingi kama vile masuala ya ardhi, huku pia akisisitiza kuwa suala la mamlaka ya rais linapaswa kuangaliwa upya na kurekebisha.
Aliongeza kuwa, moja ya mwarobaini wa kuachana na wateule wengi wa rais ni kuwa na serikali za majimbo ambako viongozi wake sharti wachaguliwe na watu badala ya sasa wananchi kutawaliwa na mkuu wa mkoa au wilaya wasiyemjua.
[TD="bgcolor: #FFFFFF"]
[/TD]
Slaa amgomea JK
Amtaka aache Watanzania waunde Katiba yao
na Mwandishi wetu, Shinyanga
[TD="width: 140, bgcolor: #FFFFFF"]
[/TD]
"Muungano ni kama koti joto likizidi unalivua" Ni kawaida kwa binadamu wenye akili timamu kila linapotokea tatizo la kutokuelewana katika jamii au baina ya watu wawili njia pekee ya kuleta maelewano baina yao ni kukaa chini na kulizungumza tatizo lao kwa maana ya kutaka kulipatia ufumbuzi na shuluhisho la kudumu ili katika siku za baadae lisitokee tena. Kwetu sisi tuna tatizo Wazanzibari wanasema kwa uwazi kabisa kuwa kuna kasoro katika muungano wetu japo Watanganyika tuliowengi hatusemi kwa nguvu kama wenzetu wa Zanzibar lakini kasoro zipo na tunaziona.Kwa kulitambua hilo ndio maana hata serikali ya JMT imeunda idara maalum chini ya ofisi ya makamu wa rais ili kushughulikia kero za muungano. Sasa kama tunatambua kuwa zipo kero kwani zisijadiliwe na wananchi ambao ndio wenye muungano?
Mwisho wa malalamiko ni kuwa na Serikali tatu,
Wananchi waamasishwe kuwepo kwa serikali ya tatu
a. Serikali ndogo ya Muungano yenye makao makuu Dar es Salaam
b. Serikali ya Tanganyika yenye makao makuu yake Dodoma
c. Serikali ya watu wa zanzibar yenye makao makuu unguja (kama sasa)