Skendo za upangaji matokeo kwenye ndondi nani awajibishwe? TPBC, Mapromota au wadamini

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
3,744
6,332
Ngumi kwa sasa zimekuwa dili na ajira nzuri kwa mabondia.

Katika michezo ya kimataifa skendo za Match fixing ni mbaya sana kwa nchi yetu.

Mpaka ABU wameamua kutokukubaliana na maamuzi ya majaji walioko huku Tanzania, basi tufahamu ya kuwa tayari bomba linavuja na dunia imeanza kufahamu kuwa Tanzania ni CHUPLI CHUPLI.

YES, KWA MKAPA HATOKI MTU

Lakini hii slogan inajikita zaidi katika jitahada na juhudi binafsi za timu mwenyeji na si mamlaka za usimamizi kulazimisha matokeo.

Ya Mwakinyo na ya Tony Rashid yanakwenda kutufanya tusiaminike duniani na ni mbaya sana kwa wadamini waliojitolea kukuza tasnia hii nchini.

Nadhani ni wakati muafaka sasa wa KUSAFISHA PALE TPBC, Chaurembo & co wapishe kizazi kipya cha uongozi wenye weledi.

Anyway nilimshangaa sana Rais Chaurembo kuingia na kufuta ushindi wa Mandonga ilhali mapambano mengine yakifixiwa na yeye akitazama tu, KISA UZAWA!!..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom