Skata la Escrow: PAC Ilichepuka kwa manufaa ya nani?

Skata la Escrow: PAC Ilichepuka kwa manufaa ya nani?

intruder

Member
Joined
Nov 25, 2014
Posts
47
Reaction score
16
BUNGE ni Taasisi yenye heshima kubwa ndani na nje ya Nchi. Heshima ya Bunge inatokana na umuhimu wa kazi yake kwa maslahi ya nchi na wananchi.

Kazi za Bunge kupitia kamati zake mbalimbali zina manufaa makubwa kwa Taifa. Mathalani, Kamati ya Hesabu za Serikali ya Bunge ina kazi muhimu ya kuhakikisha kuwa hesabu za serikali zinakuwa bayana na sahihi.

Kwa kufanya kazi zake kwa uadilifu na uzalendo, Kamati za Bunge zina nafasi muhimu ya kuisukuma na kuiwajibisha serikali kwa manufaa ya Umma. Kwa kiasi fulani, hatusiti kusema kuwa Kamati hizo zinajitahidi kutimiza wajibu wao.

Hata hivyo, tunalazimika kuikosoa hadharani Kamati ya Hesabu za Serikali ya Bunge kwa namna ilivyoandaa na kuwasilisha ripoti yake ya Fedha za Akaunti ya Escrow.

Taifa lilishitushwa na taarifa ya Kamati hiyo kuwa fedha nyingi za nchi zimechotwa kinyume na taratibu. Kamati imetaja majina ya watu na hata mazingira ya wizi ikiwa ni pamoja na maboksi, viroba na masandarusi yaliyotumika kubebea fedha hizo!

Mjadala ukawa mzito ambapo ndani ya Bunge na nje yake, moto wa hasira uliwaka kwelikweli. Ni ujasiri wa hali ya juu uliohitajika kutuliza hasira hizo kwa
maneno tofauti na yale ya Kamati.

Ilikuwa kana kwamba kila mtu alitakiwa kuamini bila kuhoji. Aliyehoji au kutoa maoni tofauti akaonekana kama ‘mchawi’ na labda ni sehemu ya watu waliopata mgao.

Ndani ya Bunge, ujasiri wa mawaziri kama Hawa Ghasia, Celina Kombani na Angellah Karuki pamoja na Wabunge kama Asumta Mshama na Job Lusinde na waziri mahiri Simbachawene wa kukataa uongo ulionekana kama ‘kero’ tu ambayo Taifa halikutakiwa kuisikia. Mawaziri hawa wanwake na Wabunge hawa wanabaki kama wapiganaji waliojitoa muhanga kuhakikisha kuwa ukweli unachukua nafasi masikioni na machoni mwa wananchi.

Pale mwanzo, ujasiri huo ulionekana kwa wachache ambao ilionekana kama vile wangeshindwa na wengi walioamini kila kilichoandikwa na kusemwa na Kamati hiyo ya Bunge!

Ni kweli, PAC ilivuna imani ya wananchi wengi. Lakini, kadiri muda ulivyokwenda hasa baada ya ripoti kukabidhiwa kwa Rais,na serikali kufanya uamuzi wa kuichunguza upya kadhia nzima ya Escrow,kiwango cha imani ya watu juu ya Ripoti ya Kamati kimeonekana kupungua.

Hatua ya Rais kuteua CAG mpya yaweza kuhesabika kama msingi wa kujenga mazingira ya kupata ukweli juu ya hesabu zilizoleta utatanishi. Kila mtu sasa akatulia kusubiri CAG mpya angesema nini.

Yumkini wengi waliamini kuwa majibu ya CAG yangewaweka pagumu wale waliotuhumiwa. Lakini Ripoti ya CAG,baada ya uhakiki, imewalowesha wale
ambao awali waliamini Ripoti ya PAC!

Kusawajika huko kunatokana na masahihisho ya hesabu zilizowasilishwa na Kamati. Mgongano wa kimahesabu kati ya dola milioni 306.6 zilizodaiwa na PAC kuwemo katika Akaunti ya Escrow na dola milioni 182.7 ambazo CAG anasema ndizo zilizokuwemo kwenye Akaunti hiyo umewashangaza wengi!

Taifa linamwamini CAG kwa asilimia 100 kwamba ndiye chombo cha kuweza kutoa taarifa sahihi. Na hata PAC inategemea taarifa za CAG. Swali linaweza kuulizwa, ni nani aliyesababisha mgongano wa mahesabu kwa kughushi na kukikuza kiasi cha fedha kinyume na taarifa ya CAG?

Na aliyefanya hivyo alikusudia nini? Na alifanya kwa maslahi ya nani? Je, huu sio mchezo mchafu wa kuchezea hesabu za serikali kwa malengo yaliyojificha yakiwemo ya kimasilahi, kisiasa na kibiashara?

Kwa kuwasilisha hesabu ambazo CAG anasema si sahihi, maana yake PAC imelidanganya Bunge na Taifa kwa ujumla! Kwa kuwa uongo huu umeleta usumbufu na umegharimu heshima za watu, pamoja na kulishulishushia heshima Tiafa mbele ya jumuiya ya kimataifa kuwa la wala rushwa na wafuja pesa, sisi tunapendekeza kuwa Bunge likutane kwa dharura ili PAC iliombe radhi Taifa kwa uongo huo.

Zaidi ya hivyo, kwa kuwa imepoteza imani ya watu juu ya umakini na uadilifu wake, PAC haina sababu ya kubaki na uongozi uliopo hivi sasa. Bunge linahitaji kujisafisha kwa kuivunja PAC na kuiunda upya.

Ni muhimu kuivunja PAC na kuipatia uongozi mpya kwani, kwa sura ya sasa haitaaminika tena masikioni na machoni mwa wananchi. Sio tu viongozi wake wa sasa hawapaswi kuwepo madarakani bali wana kila sababu ya kukabiliwa na jinai ya kuwapotosha Wananchi na kuhatarisha usalama wa Taifa.

BUNGE ni Taasisi yenye heshima kubwa ndani na nje ya Nchi. Heshima ya Bunge inatokana na umuhimu wa kazi yake kwa maslahi ya nchi na wananchi.

Kazi za Bunge kupitia kamati zake mbalimbali zina manufaa makubwa kwa Taifa. Mathalani, Kamati ya Hesabu za Serikali ya Bunge ina kazi muhimu ya kuhakikisha kuwa hesabu za serikali zinakuwa bayana na sahihi.

Kwa kufanya kazi zake kwa uadilifu na uzalendo, Kamati za Bunge zina nafasi muhimu ya kuisukuma na kuiwajibisha serikali kwa manufaa ya Umma. Kwa kiasi fulani, hatusiti kusema kuwa Kamati hizo zinajitahidi kutimiza wajibu wao.

Hata hivyo, tunalazimika kuikosoa hadharani Kamati ya Hesabu za Serikali ya Bunge kwa namna ilivyoandaa na kuwasilisha ripoti yake ya Fedha za Akaunti ya Escrow.

Taifa lilishitushwa na taarifa ya Kamati hiyo kuwa fedha nyingi za nchi zimechotwa kinyume na taratibu. Kamati imetaja majina ya watu na hata mazingira ya wizi ikiwa ni pamoja na maboksi, viroba na masandarusi yaliyotumika kubebea fedha hizo!

Mjadala ukawa mzito ambapo ndani ya Bunge na nje yake, moto wa hasira uliwaka kwelikweli. Ni ujasiri wa hali ya juu uliohitajika kutuliza hasira hizo kwa maneno tofauti na yale ya Kamati.

Ilikuwa kana kwamba kila mtu alitakiwa kuamini bila kuhoji. Aliyehoji au kutoa maoni tofauti akaonekana kama ‘mchawi’ na labda ni sehemu ya watu waliopata mgao.

Ndani ya Bunge, ujasiri wa mawaziri kama Hawa Ghasia, Celina Kombani na Angellah Karuki pamoja na Wabunge kama Asumta Mshama na Job Lusinde wa kukataa uongo ulionekana kama ‘kero’ tu ambayo Taifa halikutakiwa kuisikia.

Mawaziri hawa wanwake na Wabunge hawa wanabaki kama wapiganaji waliojitoa muhanga kuhakikisha kuwa ukweli unachukua nafasi masikioni na machoni mwa wananchi.

Pale mwanzo, ujasiri huo ulionekana kwa wachache ambao ilionekana kama vile wangeshindwa na wengi walioamini kila kilichoandikwa na kusemwa na Kamati hiyo ya Bunge!

Ni kweli, PAC ilivuna imani ya wananchi wengi. Lakini, kadiri muda ulivyokwenda hasa baada ya ripoti kukabidhiwa kwa Rais, na serikali kufanya uamuzi wa kuichunguza upya kadhia nzima ya Escrow, kiwango cha imani ya watu juu ya Ripoti ya Kamati kimeonekana kupungua.

Hatua ya Rais kuteua CAG mpya yaweza kuhesabika kama msingi wa kujenga mazingira ya kupata ukweli juu ya hesabu zilizoleta utatanishi. Kila mtu sasa akatulia kusubiri CAG mpya angesema nini.

Yumkini wengi waliamini kuwa majibu ya CAG yangewaweka pagumu wale waliotuhumiwa. Lakini Ripoti ya CAG, baada ya uhakiki, imewalowesha wale ambao awali waliamini Ripoti ya PAC! Kusawajika huko kunatokana na masahihisho ya hesabu zilizowasilishwa na Kamati.

Mgongano wa kimahesabu kati ya dola bilioni 306.6 zilizodaiwa na PAC kuwemo katika Akaunti ya Escrow na dola bilioni 182.7 ambazo CAG anasema ndizo zilizokuwemo kwenye Akaunti hiyo umewashangaza wengi!

Taifa linamwamini CAG kwa asilimia 100 kwamba ndiye chombo cha kuweza kutoa taarifa sahihi. Na hata PAC inategemea taarifa za CAG. Swali linaweza kuulizwa, ni nani aliyesababisha mgongano wa mahesabu kwa kughushi na kukikuza kiasi cha fedha kinyume na taarifa ya CAG?


Na aliyefanya hivyo alikusudia nini? Na alifanya kwa maslahi ya nani? Je, huu sio mchezo mchafu wa kuchezea hesabu za serikali kwa malengo yaliyojificha yakiwemo ya kimasilahi, kisiasa na kibiashara?

Kwa kuwasilisha hesabu ambazo CAG anasema si sahihi, maana yake PAC imelidanganya Bunge na Taifa kwa ujumla!

Kwa kuwa uongo huu umeleta usumbufu na umegharimu heshima za watu, pamoja na kulishulishushia heshima Tiafa mbele ya jumuiya ya kimataifa kuwa la wala rushwa na wafuja pesa, sisi tunapendekeza kuwa Bunge likutane kwa dharura ili PAC iliombe radhi Taifa kwa uongo huo.

Zaidi ya hivyo, kwa kuwa imepoteza imani ya watu juu ya umakini na uadilifu wake, PAC haina sababu ya kubaki na uongozi uliopo hivi sasa. Bunge linahitaji kujisafisha kwa kuivunja PAC na kuiunda upya.

Ni muhimu kuivunja PAC na kuipatia uongozi mpya kwani, kwa sura ya sasa haitaaminika tena masikioni na machoni mwa wananchi. Sio tu viongozi wake wa sasa hawapaswi kuwepo madarakani bali wana kila sababu ya kukabiliwa na jinai ya kuwapotosha Wananchi na kuhatarisha usalama wa Taifa.
 
Pesa ya mfanyabiashara dalali na mwenye uchu,ndg Reginard Mengi.Huyu anatamani awe Aliko Dangote ndani ya mda mfupi,anataka rasilimali yote iwe chini yake na pia aiendeshe serikali kwa jinsi anavyotaka.
 
Kazi ya PAC nafikiri imeisha kama lilivyoisha ya BMT! Tunasonga mbele, tugange yajayo.
 
Wahusika wote wachukuliwe hatua wafukuzwe kazi mara moja, ikiwa na pamoja na kufikishwa mahakamani. Cheo ni dhamana ifike wakati watu wajisute nafsi zao wabwage manyanga ili nchii itulie. Kama Jaji Werema alijua kweli ushauri wake haukueleweka na uliaribu hali ya hewa basi; Prof.Tiba jinsi alivyopata 1.6bil alichafua hali ya hewa hata kuliko Jaji Werema. Ebu wabwage manyanga ili kali ya nchi itulie watu wafanyekazi na misaada toka nje ifunguliwe: Jamani hivi Prof, Tiba;Prof muhongo na Maswi wao ni zaidi ya Tanzania??; kwa nini wasitoke tupate misaada. Na je ina maana hapa TZ hakuna mbadala wa hao watu???? Hapana waondoke "They must go by any means" tumechokana nao.
 
Tulisema humu kuwa escrow ilikuwa na billion 182 na ndizo zimo kwenye ripoti ya CAG, hizo 300 na PAC walizitoa wapi?

PAC wamedanganya Watanzania, inafaa kamati yote ya PAC iende jela kwa kulidanganya taifa au wapigwe risasi hadharani iwe fundisho kwa wengine.
 
Tulisema humu kuwa escrow ilikuwa na billion 182 na ndizo zimo kwenye ripoti ya CAG, hizo 300 na PAC walizitoa wapi? PAC wamedanganya Watanzania, inafaa kamati yote ya PAC iende jela kwa kulidanganya taifa au wapigwe risasi hadharani iwe fundisho kwa wengine.
JK aliposema tu ripoti ya CAG iwekwe hadharani wakaishiwa nguvu.
 
Tulikuwa marafiki kwa siku 2 sasa naona umerudi kwako! Anyway liwalo na liwe ! Kwani nyani akija kumchongea nguruwe kuwa amekula mahindi huatachukua hatua ! Kama PAC ilikuwa na lake jamabo sisi tunasonga mbele ,tunakata panga mwizi yoyote
Tulisema humu kuwa escrow ilikuwa na billion 182 na ndizo zimo kwenye ripoti ya CAG, hizo 300 na PAC walizitoa wapi?

PAC wamedanganya Watanzania, inafaa kamati yote ya PAC iende jela kwa kulidanganya taifa au wapigwe risasi hadharani iwe fundisho kwa wengine.
 
Tulisema humu kuwa escrow ilikuwa na billion 182 na ndizo zimo kwenye ripoti ya CAG, hizo 300 na PAC walizitoa wapi?

PAC wamedanganya Watanzania, inafaa kamati yote ya PAC iende jela kwa kulidanganya taifa au wapigwe risasi hadharani iwe fundisho kwa wengine.
Mheshimiwa Asumpta nakuunga mkono.
 
Sasa hata ikiwa ni bilioni 182 je ndiyo watu waziibe? Acha ujinga wizi ni wizi tu hata shilingi 100 unapaswa kuwajibishwa.
tulisema humu kuwa escrow ilikuwa na billion 182 na ndizo zimo kwenye ripoti ya cag, hizo 300 na pac walizitoa wapi?

Pac wamedanganya watanzania, inafaa kamati yote ya pac iende jela kwa kulidanganya taifa au wapigwe risasi hadharani iwe fundisho kwa wengine.
 
Tulisema humu kuwa escrow ilikuwa na billion 182 na ndizo zimo kwenye ripoti ya CAG, hizo 300 na PAC walizitoa wapi?

PAC wamedanganya Watanzania, inafaa kamati yote ya PAC iende jela kwa kulidanganya taifa au wapigwe risasi hadharani iwe fundisho kwa wengine.
Argue don't shout woman! Very naive and novice sort of lament.
 
we ni ----- kwelikweli,hivi unajua ni kwanini hiyo akaunti ya dhamana ilifunguliwa,katika mauzo ya hisa za IPTL,kodi haikulipwa,mkataba kati ya IPTL na TANESCO ulikuwa wa kitapeli,mwanasheria wa TANESCO alipotoa ushauri akafukuzwa kazi,mtumishi wa uma anapokea zawadi ya mamilioni ya pesa,kwa ajiri ya shughuri yake binafsi,anakaa kimya,kwanini hakuita vyombo vya habari na kuweka mambo hadharani,ili umma wote wa wa TZ,tumshukuru huyo mfanyabiashara, bado tu hapo huoni kwamba kuna harufu ya rushwa,

Waziri ambaye ardhi ipo chini yake anapewa zawadi na wawekezaji ambao wanaitaji ardhi,mwanasheria anayepitia mikataba yote yenye maslahi kwa taifa,anapewa zawadi na mwekezaji,bado tu huamini kwamba suala la TEGETA ESCROW,ni la kifisadi,yaani mijitu kama wewe mnastaili kuwa executed kwa risasi moja tu nyuma ya kisogo,

umepewa TSH ngapi mpaka uwatetee wezi,mnakula,mnavimbiwa,hamuoni kitu,harafu unakuja hapa na uharo huu,
 
Tulikuwa marafiki kwa siku 2 sasa naona umerudi kwako! Anyway liwalo na liwe ! Kwani nyani akija kumchongea nguruwe kuwa amekula mahindi huatachukua hatua ! Kama PAC ilikuwa na lake jamabo sisi tunasonga mbele ,tunakata panga mwizi yoyote

Ulikuwa unaota?

Sijawahi kuunga mkono PAC hata siku moja kwenye hili.
 
Waje hapa waseme hizo mia tatu na ushee badala ya 180.. walipata wapi? tuwahoji pia ilikuwa kwa masrahi ya nani alafu mwisho tuwaulize kama hii ingekuwa wanafanyiwa wao wangeikubali,na je wanastahili kuendelea kuwemo kwenye hiyo kamati?
 
Sasa hata ikiwa ni bilioni 182 je ndiyo watu waziibe? Acha ujinga wizi ni wizi tu hata shilingi 100 unapaswa kuwajibishwa.

Wamemuibia nani?

Mmekazana wameiba, wameiba, mkulizwa nani kaibiwa? hamna majibu. Ulifikiri Hebinder Singh anagawa umeme wa bure?

Jiulize, ulitaka umeme wa bure?
 
Waje hapa waseme hizo mia tatu na ushee badala ya 180.. walipata wapi? tuwahoji pia ilikuwa kwa masrahi ya nani alafu mwisho tuwaulize kama hii ingekuwa wanafanyiwa wao wangeikubali,na je wanastahili kuendelea kuwemo kwenye hiyo kamati?
mchukue tu kimwishomwisho huo mgao wenu mana siku zenu znahesabika mafisadi na watetea matumbo kama ninyi...
 
Kwa kuwasilisha hesabu ambazo CAG
anasema si sahihi, maana yake PAC
imelidanganya Bunge na Taifa kwa ujumla!
Kwa kuwa uongo huu umeleta usumbufu
na umegharimu heshima za watu, pamoja
na kulishulishushia heshima Tiafa mbele ya
jumuiya ya kimataifa kuwa la wala rushwa
na wafuja pesa, sisi tunapendekeza kuwa
Bunge likutane kwa dharura ili PAC iliombe
radhi Taifa kwa uongo huo.
Zaidi ya hivyo, kwa kuwa imepoteza imani
ya watu juu ya umakini na uadilifu wake,
PAC haina sababu ya kubaki na uongozi
uliopo hivi sasa. Bunge linahitaji
kujisafisha kwa kuivunja PAC na kuiunda
upya.
Ni muhimu kuivunja PAC na kuipatia
uongozi mpya kwani, kwa sura ya sasa
haitaaminika tena masikioni na machoni
mwa wananchi
. Sio tu viongozi wake wa
sasa hawapaswi kuwepo madarakani bali
wana kila sababu ya kukabiliwa na jinai ya
kuwapotosha Wananchi na kuhatarisha
usalama wa Taifa. BUNGE ni Taasisi yenye heshima kubwa
ndani na nje ya Nchi. Heshima ya Bunge
inatokana na umuhimu wa kazi yake kwa
maslahi ya nchi na wananchi.
Kazi za Bunge kupitia kamati zake
mbalimbali zina manufaa makubwa kwa
Taifa.

Ni muhimu kuivunja PAC na kuipatia
uongozi mpya kwani, kwa sura ya sasa
haitaaminika tena masikioni na machoni
mwa wananchi
. Sio tu viongozi wake wa
sasa hawapaswi kuwepo madarakani bali
wana kila sababu ya kukabiliwa na jinai ya
kuwapotosha Wananchi na kuhatarisha
usalama wa Taifa.

kwa taarifa yako wananchi wanataka wote waliohusika na sakata hili waishie jela pia wenye kuwajibika kwa nafasi zao wawajibike period. hizo longo longo za kuwasingizia wananchi hazitosaidia
 
Back
Top Bottom