Siyo Siri CHADEMA Imepata Jeraha

Ni kweli usemacho. Tusitangulize ushabiki mbele katika hili. Think tanks wa chadema wakae chini na kutafuta namna ya kuvuka mtihani huu. Vinginevyo mpasuko na mmeguko utaendelea

Tangu zzk afurushwe cdm sasa mwaka wa pili na cdm ndio inazidi kupasua anga
 
Huyu nae!! angalia akiba ya vichwa vilivyopo cdm zzk ataleta madhara gani kwa kuondoka kwake? siri gani zaidi ya ilani?
 
Nimeipenda hii ndani yake kama ukisoma kwa umakini unaona kitu ndani yake chadema wajipange siyo utani ni jeraha kubwa sana.
 
Huyu nae!! angalia akiba ya vichwa vilivyopo cdm zzk ataleta madhara gani kwa kuondoka kwake? siri gani zaidi ya ilani?

Mimi pamoja na familia yangu pamoja na marafiki wangu watano tumechoma kadi za uachama wa chadema pamoja na nguo zao, chama gani cha ukabila na ukoo namna ile.
kutoka watu 12 ndani ya chadema ni pengo, huoni kwamba ni hasara?
 
Kwa vyovyote vile chadema wamepoteza kura nyingi sana maana watu wengi wanaojiunga ACT wanatoka chadema.
 

Sasa kama hakuna siri, mbona tulikuwa tunaambiwa kuwa Zitto alikuwa akivujisha SIRI za chama upande wa pili na Usalama wa Taifa?
 

Kelele za chura hazimzuii ng'ombe kunywaa maji kisimani, CDM mbele kwa mbele, nyie endeleeni na mipasho!
 
Mbona wanasiasa wote walitoka CCM na hakuna siri zozote zile tulisikia wakisema kuhusu CCM
 
Hakuna jeraha wala mama yake jeraha. Msaliti aliyekuwa anatumika ndani ya chama kwa nia ya kukisambaratisha chama kamwe pale anapofukuzwa hawezi kuacha chama kikiwa na jeraha kubwa. Hii ilikuwa ni kansa ambayo ilikuwa inatambaa taratibu ndani ya chama na kupunguza kwa kiasi kikubwa mshikamano wa hali ya juu uliokuwepo chamani kwa kuiondoa kansa hii sasa chama kitarudia katika afya yake badala ya kuendelea kupoteza muda chungu nzima kuijadili kansa iliyokuwa inatishia uhai wa CHADEMA.

πŸ˜›eace:πŸ˜›eace:πŸ˜›eace:

Alutta continua! continua!





 

mkuu,nilikuwa shamba wilaya moja ya mkoa wa Pwani ambako huko ni CUF na CCM,lakini kitu nilichokiona kwa siku 2 nilizokuwepo huko,wana CCM na CUF wengi sana wanasema wangependa kujiunga na chama hiki kipya (ACT) kama kitakuwa tofauti na vyama walivyokuwepo,yaani CCM na CUF.
Mimi kwa mtazamo wangu naona hiki chama kama kitajipanga kweli na kujitanabaisha bayana kuhusu sera,itikadi,katiba na mambo yanayohusu mustakabari mzima wa mwananchi wa kawaida,basi kitavuna maelfu ya wafuasi,hasa hasa wafuasi wa CCM.
 

MKUU.

Ni kweli usemayo kwamba chadema tumepata jeraha; lakini kuna ubaya gani kuuguza jeraha lililotokana na kutumbua jipu? Wala usipate hofu kwa kuwa eti, Palipoingia kovu haparudi kuwa sawa;kumbuka, Heri pengo kuliko jino bovu na Pengo la jino mmoja halizuwii kinywa kutafuna
 
Hakuna jeraha hapo,hapo kuna mchubuko tu ndugu.
tambua kwamba kila kukicha mbinu zinaibuliwa,alafu kitu kingine ni kwamba zzk aliacha kushiriki mambo ya chama karibia miaka miwili,so from there mambo mengi mema ya kukijenga chama yamefanyika.
let him go,we can do better without him.
 
Reactions: BAK

Mkuu naungana na wewe,watu wanachukulia ki utaniutani lakini practicaly chadema itaathirika sana,tuchukulie mfano kigoma ambapo wananchi wana hasira sana na chadema baada ya watu wao(Zito na kafulila)kufukuzwa ni kura ngapi zitapotea hasa ukizingatia kwa sasa upinzani unataka kuchukua dola kwa namna yoyote ile ku ignore kura za kigoma kwa mfano ni kosa kubwa sana kwa Ukawa,somthing urgent need to be done.Nafikiri viongozi wa juu wanafaham hilo kazi kwao.
 

Well said mkuu
 
Ahsante sana Mkuu

 
ACT fanyeni juhudi za kuichukua Kigoma YOTE. CDM maeneo yao yatatwaliwa na mgawanyiko huo. CDM ni chama cha Wachaga pekee. Ni chama cha Kikanda hasa Kaskazini. Maeneo kama Iringa Mjini na Mbeya ni kwa makosa waliyofanya CCM wakati huo. Nao wamejua walijikwaa wapi.

UKAWA sasa kwisha habari yao. Cake yao sasa imemegwa na kwenda ACT. Hiyo pekee itatengeneza njia kwa CCM kujihakikishia ushidi Oktoba na ACT kuambulia maeneo kadhaa. Nakitahilia ACT viti 15 vya Ubungo ifikapo Uchaguzi Mkuu.

Kama wanaakili nzuri,CDM wajipe miaka 5 mbeleni ya kujiandaa na kujipanga. Kwa sasa bado ni wachanga na nchi haitachukuliwa kirahisi kwa uroho wa Madaraka.

Wanawatumia Wafanyabiashara eti wakidhani ni mkakati kumbe ni kunyesa tu Mwenyekiti wao,MCHAGA,MWANA CDM,MINJA!

CDM watakula jeuri yao mwaka huu!
 
Si kweli kwamba CHADEMA wamepata jeraha bali wameonesha kupevuka kisiasa, na kama ACT imeanzishwa kwa ajili ya kupambana na CHADEMA na si kushiriki katika harakati za kuiondoa CCM madarakani basi hili ni pigo namba moja kwa ACT na demokrasia hapa nchini Tanzania.

Ukweli ni kwamba CHADEMA kiko imara sana na wote walioko ACT wanajua hivyo na si muda tutarajie mtifuano mkubwa kutokana na walioko huko wanao uchu mkubwa wa madaraka hivyo si vema kuanza tambo za mapema hali hatujafika hata nusu ya mlima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…