Siyo Siri CHADEMA Imepata Jeraha

Siyo Siri CHADEMA Imepata Jeraha

G4N

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2014
Posts
4,449
Reaction score
10,300
Chadema kama taasisi imepata jeraha kubwa. Jeraha hili linahitaji tiba madhubuti ili lisikigharimu chama. Maana viongozi waliopo ACT wanajua siri zote za chadema. Walikuwa wanashiriki vikao vya ndani kabisa vya chama. Ni sawa na kuachana na mke/mume. Hakuna wa kujivuna. Bali akili lazima itulie ili kuendelea na maisha mapya. Na usipo kaa vema utaishia kunywa pombe au kufanya ukahaba kwa kuchanganyikiwa.

Na ndiyo maana kwa mnaofuatilia kinachoendelea ukumbi wa Diamond Jubilee. Kuna mwanadada muigizaji alipotupa dogo linaloilenga chadema ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe. Nitanikuu "kumpiga chura teke ni kumpunguzia safari".
 
Ni mchubuko siyo jeraha, hakuna siri katika chama zaidi ya yale yaliyomo kwenye katiba ambayo kila mtu husoma, huwezi ukawazuia bendera fuata upepo kutoka ndani ya chama kwenda chama kingine wakifuata maslahi yao, kila siku tunatangaziwa watu wanarudisha kadi za CHADEMA lakini chama kinazidi kukua. Ilikuwa ni wakati muafaka kwa ZZK kufukuzwa ndani ya Chama kuondoka kwake ni siyo jeraha bali ni kamchubuko tuuu
 
Ni mchubuko siyo jeraha, hakuna siri katika chama zaidi ya yale yaliyomo kwenye katiba ambayo kila mtu husoma, huwezi ukawazuia bendera fuata upepo kutoka ndani ya chama kwenda chama kingine wakifuata maslahi yao, kila siku tunatangaziwa watu wanarudisha kadi za CHADEMA lakini chama kinazidi kukua. Ilikuwa ni wakati muafaka kwa ZZK kufukuzwa ndani ya Chama kuondoka kwake ni siyo jeraha bali ni kamchubuko tuuu

Well said mkuu
 
Hakuna kitu kama hicho, wasiwasi wako tu. Hao wote wanaoonekana kwenye mikutano inayorushwa live wamekodiwa, nasikia kila mmoja kavuta 50,000. Je wanaubavu wa kuendelea kulipa watu wote watakaokuwa wanahudhuria mikutano yao. Hata kama itakuwa hivyo tutahoji wamepata wapi fedha hizo

Kwa akili ya kawaida tu, unafikiri pesa za madoido yote hayo wamepata wapi?
 
Afande Sele anasema kocha wa ....anafukuza wafunga magoli kila mara fainali inapokaribia. Ametoa mfano kwamba 2010 striker Kafulila alifukuzwa siku chache kabla ya uchaguzi mkuu na sasa amefukuzwa mfunga magoli mwingine. Sasa wenye akili akina Afande Sele wamefanya maamuzi makini.

Maneno haya yanaposikilizwa na wananchi wa Mwitongo, Nakapanya na Kaliua wengine yanawaingia akilini. Chadema ifanye kila linalowezekana kuzuia sumu hii kali kupenya kwenye vichwa vya watanzania.
 
Mtoto wa kiume akimbaka mama yake na mama kama ana akili timamu lazima amlaani....hawezi kumsamehe eti kisa ni mwanae....Ayatollah Zitto amelaaniwa na chadema kwa hiyo chama kimeona njia nzuri ni kumlaani tu bila kujali umaarufu wake.
 
Kwani Yeye Afande alipovua nguo hadharani ni Kwamba vijana wote wanavua nguo?. Chadema ni Chama hakiwezi kumvumilia mwenda wazimu.
 
Alipoondoka Kafurila ndio CDM kikapata wabunge na Madiwani wengi. Na Ameondoka Msaliti Tumepata vitongoji na Wenyeviti wa Mtaa wengi. Cdm ni Dume.
 
Mada ya aliyeshiba na kuvimbiwa maana haina fact wala rejea.
 
Chadema kama taasisi imepata jeraha kubwa. Jeraha hili linahitaji tiba madhubuti ili lisikigharimu chama. Maana viongozi waliopo ACT wanajua siri zote za chadema. Walikuwa wanashiriki vikao vya ndani kabisa vya chama. Ni sawa na kuachana na mke/mume. Hakuna wa kujivuna. Bali akili lazima itulie ili kuendelea na maisha mapya. Na usipo kaa vema utaishia kunywa pombe au kufanya ukahaba kwa kuchanganyikiwa.

Na ndiyo maana kwa mnaofuatilia kinachoendelea ukumbi wa Diamond Jubilee. Kuna mwanadada muigizaji alipotupa dogo linaloilenga chadema ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe. Nitanikuu "kumpiga chura teke ni kumpunguzia safari".

Jitahidi kutafakari kabla ya kuandika, hao unaowaona leo huko ACT waliishatupwa kando na CHADEMA kabla chama hakijafanya uchaguzi mkuu na ni vema ukajiuliza kama wangekuwa na madhara kwenye chama matokeo ya uchaguzi serikali za mitaa kwa CHADEMA yangekuwa kama yalivyo? Zitto kafukuzwa kukiwa bado maeneo mengine yanafanya chaguzi za marudio serikali za mitaa vipi kuhusu matokeo yake.
Ni vema ukatambua kuwa kwa sasa ACT inashabikiwa kiasi kikubwa na wanaCCM kama ilivyokuwa kwa ADC kwani kwa upande wa CHADEMA wafuasi, wapenzi na wanachama wote wanakipenda chama na sio mtu au watu na ndio maana hawateteleki na chama kitabaki kuwa imara daima.
 
Ni muhimu kutazama CHADEMA na ACT kama taasisi na sio mtu mmojamoja ili kuweza kuja na neon linaloweza kuwakilisha yanayotokea ndani ya taasisi hizo sasa hivi. Kama ni pigo labda kwa mtu mmojammoja kama ZZK alivyo au Slaa au Mbowe. Taasisi zilizoundwa kwa misingi thabiti huwa haziyumbi pale individuals wanapobadili misimamo yao kama ZZK alivyofanya kwa CHADEMA.
 
Chadema kama taasisi imepata jeraha kubwa. Jeraha hili linahitaji tiba madhubuti ili lisikigharimu chama. Maana viongozi waliopo ACT wanajua siri zote za chadema. Walikuwa wanashiriki vikao vya ndani kabisa vya chama. Ni sawa na kuachana na mke/mume. Hakuna wa kujivuna. Bali akili lazima itulie ili kuendelea na maisha mapya. Na usipo kaa vema utaishia kunywa pombe au kufanya ukahaba kwa kuchanganyikiwa.

Na ndiyo maana kwa mnaofuatilia kinachoendelea ukumbi wa Diamond Jubilee. Kuna mwanadada muigizaji alipotupa dogo linaloilenga chadema ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe. Nitanikuu "kumpiga chura teke ni kumpunguzia safari".

Ni kweli usemacho. Tusitangulize ushabiki mbele katika hili. Think tanks wa chadema wakae chini na kutafuta namna ya kuvuka mtihani huu. Vinginevyo mpasuko na mmeguko utaendelea

Well said mkuu

Kwahiyo act tanzania/act wazalendo kipo kwa ajili ya kupambana na CHADEMA au kukomboa wananchi wenye matatizo mengi! Huku ni kujichanganya kubaya kabisa UNAPOHUBIRI USICHOAMINI! NA KUAMINI USICHOHUBIRI🔥🔥🔥
 
Chadema sasa itafute bomba jipya la kupumulia. Kama walipanga mapema kumfukuza Zitto na wameweza, basi wapange mbinu mpya za kuretain status waliyokuwa nayo ili waendelee kusimama dede kama walivyokuwa. Tusiposema kuwa hili ni pigo tutakuwa tunajidanganya kwa kujiangalia kwenye kioo huku tumefumba macho ilhali sura inaonekana kwenye kioo, CDM jipangeni upya kuzuia wimbi la uhamiaji kwenda kwa zitto, hakika term hii ccm imejijenga bila gharama. SUBIRINI MUONE General election itakavyokuwa tamu!!

Haters gonna be like :A S 20:
 
Last edited by a moderator:
wewe unasema imepata jeraha wakti imepona kidonda ndugu, waliolelewa na chama ndo wanasaliti, kidondo hicho
 
Chadema kama taasisi imepata jeraha kubwa. Jeraha hili linahitaji tiba madhubuti ili lisikigharimu chama. Maana viongozi waliopo ACT wanajua siri zote za chadema. Walikuwa wanashiriki vikao vya ndani kabisa vya chama. Ni sawa na kuachana na mke/mume. Hakuna wa kujivuna. Bali akili lazima itulie ili kuendelea na maisha mapya. Na usipo kaa vema utaishia kunywa pombe au kufanya ukahaba kwa kuchanganyikiwa.

Na ndiyo maana kwa mnaofuatilia kinachoendelea ukumbi wa Diamond Jubilee. Kuna mwanadada muigizaji alipotupa dogo linaloilenga chadema ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe. Nitanikuu "kumpiga chura teke ni kumpunguzia safari".

Kama viongozi wa cdm wanavyojua siri zoote za ccm
 
Back
Top Bottom