Yote tisa, swali moja tu kwa Sitta -Mbona mmeitambua Symbion walirithi wengine wa mitambo ile ile yenye historia ya Richmond??
Acha tabia ya usahaulifu, Kamati ya Mwakyembe ilikuwa ni kamati ya rais sii ya bunge hivyo Sitta alilazimika kuweka mjadala baada ya rais kuruhusu swala hilo liende bungeni na hadi kujiuzulu kwa Lowassa kama waziri mkuu. Sitta alikataa katakata swala la Richmond lisijadiliwe hata baada ya Lowassa kujiuzulu hakuruhusu swala hilo liendelee kuzungumziwa wakati ushahidi wote walikuwa nao bungeni.
Mimi nilishindwa kuelewa kwa nini wananchi na Bunge walitaka rais ndiye awawajibishe Lowassa na Rostam hali kesha wapeni greenlight ya kufanya uchunguzi na hata kukubali kujiziulu kwa Lawassa ktk mhimili wake (serikali). Hivi kweli ilikuwa kazi ya rais kufungua mashtaka hali bungeni hajapatikana na makosa? Swala la Richmond lilifia bungeni chini ya uongozi wa Sitta, Jk alishaifanya kazi yake toka upande wake.
Sitta angesema ushahidi ulokusanywa unatosha kuwawajibisha watuhumiwa na kumwambia Lowassa kama mbunge anapaswa kujieleza bungeni dhidi ya tuhuma hizo. Lowassa alijiuzulu kama Waziri mkuu, mhimili wa serikali na sii kama mbunge mhimili ambao Sitta alikuwa mwenye mamlaka yote ya kuwaita wahusika na tungepata ufumbuzi na pengine hata tusingewaona hawa Lowassa na Rostam wakisimama tena kugombea Ubunge mwaka 2010.. Sitta was the man behind kila liloshindikana bungeni na hata tukaletewa Dowans na leo tumefungashiwa Symbion...