jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 35,053
- 28,245
Kwa muda mrefu spika sitta amesikika mara kadhaa akiipinga serikali hadharani.mojawapo ya masuala anayoyapinga ni malipo kwa kampuni ya dowans. Kinachonishangaza mzee huyu amebakia kulalamika bila kuchukua hatua, hana tofauti na mwananchi wa kawaida ambaye hana uwezo wa kukaa meza moja na JK.
Sitta kwa nafasi yake alitakiwa kumshauri au kumshawishi mh raisi kwamba kuilipa dowans ni ufisadi. Sina hakika kama alishawahi kumuandikia barua JK au kupeleka hoja binafsi kwenye cabinet kuhusu suala la dowans.
Kama ikishindikana kwenye cabinet basi Sitta afanye maamuzi magumu mfano kuongoza maandamano ya wanaharakati dhidi ya dowans,kuanzisha chama cha upinzani au kuhamia chama cha upinzani chenye nguvu kama chadema.kuendelea kupiga kelele kwenye T.V na magazeti ni kujitafutia umaarufu tu.
Nashauri mzee sitta aamue kunyoa au kusuka kwa vitendo na sio kuuma na kupuliza kama hawezi akae kimya ashughulikie mambo ya EAC.
Najua mzee huyu huwa anapitia humu jamvini kama mimi,hata kama hapiti naomba mumfikishie salamu kwa niaba yangu.
Jingalao
Sitta kwa nafasi yake alitakiwa kumshauri au kumshawishi mh raisi kwamba kuilipa dowans ni ufisadi. Sina hakika kama alishawahi kumuandikia barua JK au kupeleka hoja binafsi kwenye cabinet kuhusu suala la dowans.
Kama ikishindikana kwenye cabinet basi Sitta afanye maamuzi magumu mfano kuongoza maandamano ya wanaharakati dhidi ya dowans,kuanzisha chama cha upinzani au kuhamia chama cha upinzani chenye nguvu kama chadema.kuendelea kupiga kelele kwenye T.V na magazeti ni kujitafutia umaarufu tu.
Nashauri mzee sitta aamue kunyoa au kusuka kwa vitendo na sio kuuma na kupuliza kama hawezi akae kimya ashughulikie mambo ya EAC.
Najua mzee huyu huwa anapitia humu jamvini kama mimi,hata kama hapiti naomba mumfikishie salamu kwa niaba yangu.
Jingalao