Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Waalimu wa Saikolojia,Sosholojia,Historia na Siasa mara zote hutuambia kwamba "historia ni mwalimu mzuri".
Huko nyuma wakati Samuel Sitta akiwa ni spika wa Bunge aliwahi kuzuia Naibu wa Spika wakati huo Bi. Anne Makinda kuendesha mjadala wa Ritchmond kwa madai kwamba hiyo ni hoja nzito ambayo Makinda asingeweza kuimudu. Watu wengi mimi nikiwa ni mmoja wao tulimsakama sana Sitta kwamba anataka kuleta ukiritimba wa nafasi ya Uspika.
Lakini kwa jinsi Anne Makinda anavyoliendesha Bunge na jinsi alivyopendekezwa kugombea nafasi hiyo, nadhani tuko kwenye nafasi nzuri sana ya kuamua kama Samuel Sitta alikuwa sahihi wakati ule aliposema kwamba Makinda hana sifa ya kundesha baadhi ya mijadala bungeni kwa maslahi ya taifa.
Tafakari!!`
Huko nyuma wakati Samuel Sitta akiwa ni spika wa Bunge aliwahi kuzuia Naibu wa Spika wakati huo Bi. Anne Makinda kuendesha mjadala wa Ritchmond kwa madai kwamba hiyo ni hoja nzito ambayo Makinda asingeweza kuimudu. Watu wengi mimi nikiwa ni mmoja wao tulimsakama sana Sitta kwamba anataka kuleta ukiritimba wa nafasi ya Uspika.
Lakini kwa jinsi Anne Makinda anavyoliendesha Bunge na jinsi alivyopendekezwa kugombea nafasi hiyo, nadhani tuko kwenye nafasi nzuri sana ya kuamua kama Samuel Sitta alikuwa sahihi wakati ule aliposema kwamba Makinda hana sifa ya kundesha baadhi ya mijadala bungeni kwa maslahi ya taifa.
Tafakari!!`