Hmaster
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 346
- 86
Huku hali ikiwa si shwari ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) aliyekuwa spika wa bunge la tisa na waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki mh. Samuel Sitta inasemekana amejiunga na chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA). Kwa mujibu wa taarifa ambazo hata hivyo bado hazijathibitishwa na muhusika kutoka kwa chanzo cha habari cha kimataifa mheshimiwa huyo amesema kwamba lengo lake kuu ni kutetea maslahi ya wananchi bila kuwa na wasiwasi wa kuambiwa eti anakikosoa chama nje ya vikao. Walipopigiwa simu Dr. Slaa na Mh.Mbowe walishindwa kutoa maelezo ya moja kwa moja ila walisema tu wapo katika kikao kizito na watalizungumza hilo baada ya kikao hicho. Kuna mwenye uhakika na taarifa hii kwa undani, atujuze zaidi.:mmph: