The Professor
JF-Expert Member
- Apr 30, 2013
- 2,223
- 4,580
SITOSAHAU
(simulizi ya kweli) Ilikua jumatano mida ya saa 10 jioni
muda niliokua nimetoka kuoga na
kuvaa nguo nilizozipenda na kuzijali
sana kuliko nguo zangu zote
nakumbuka nilivaa T.shirt ya CCM na
kaptura ya bluu iliyokua imepambwa na viraka viwili kiraka kimoja kikubwa
kilikua sehemu ya makalio na kiraka
kingine kilikua maeneo ya mbele ya
kaptura yangu na kufanya zipu
ishindwe kufunga vizuri
miguuni nilijitupia ndala nyekundu zilizokua zimeisha kwenye visigino
*** *** *** *** ***
Baada za kuhakikisha kua
nimependeza nikaanza safari yangu ya
kwenda internet cafe kwa lengo la
kwenda kuperuzi facebook na ku confirm friends request 15 zilizokua
zikisubiri kujibiwa kwa hamu kubwa
sana
*** *** *** *** ***
Basi wakati naanza kwenda internet
cafe nikaamua nipite vichochoroni ili kukwepa mapaparazi na nyodo za
watoto wakike ili wasije wakanichuna
bure Basi mzee mwenyewe nikaanza safari
ya kwenda cafe kwa mbwembwe zote
huku mkononi nikiwa nimeshika ka
simu kangu ka mchina ka G-TIDE huku
nikiendelea kusikiliza ringtone
*** *** *** *** wakati napita pale uchochoroni
ghaflaaa nikasikia sauti za mahaba
zinatoka kwenye dirisha 1 lililokua
wazi
aseh zile sauti zilinivutia sana ikabidi
niairishe safari yangu na kwenda kuchungulia mle dirishani
daah sikuamini nilichokiona mzee 1
alikua akifanya mapenzi na mkewe
ilibidi nianze kupiga chabo
*** *** *** *** ***
wakati napiga chabo ghaaafla kuna jamaa 1 alikatiza pale uchochoroni kwa
speed kali na kunigonga na kufanya
kale ka G-TIDE kangu ka kichina
kadumbukie mle chumbani
niliacha kupiga chabo na kuanza
kukatoa ka simu kangu *** *** *** *** ***
wakati nahangaika kutoa ka simu
kangu ghaafla likatokea kundi kubwa
la watu waliokua na silaha kali
wakanizunguka na kuanza kunipiga
wakijua mimi ni mwizi aseh lile kundi ndo lilikua likimfukuza
yule jamaa alienigonga kumbe alikua ni
mwizi daah
*** *** *** *** ***
Nilichezea vitasa vya kufa mtu wale
jamaa walinipiga kweli yani walinivimbisha ghaafla wakati
naendelea kupewa vitasa nilianza
kupiga kelele
Mamaa weee nakufaaa
*** *** *** *** ***
Bahati nzuri zile kelele zilimshtua yule mzee aliekua akishughulika na mkewe
zile kelele zilifanya yule mzee ajue
tunapiga chabo daah ghaflaa yule
mzee akatoka na bunduki ya kukoki
kama zile za walinzi na kuja kule
tulipokua da alipofika tu hata hakumsemesha mtu alifyatua risasi juu
na kufanya kila mtu akimbie yaani
uwezi amini pamoja na kupigwa kote
kule mimi ndo nilikua wa kwanza
kukimbia
*** *** *** *** *** Nilikimbia speed 120 ile nafika tu
barabarani nikakutana na yule jamaa
alienigonga na kudumbukiza simu
yangu mle chumbani
Yule jamaa alikuja kunishukuru eti
nimemuokoa aseeh yaani nilitamani nimkate makofi lakini
sikua na nguvu
Ilibidi nirudi nyumbani
wakati nafika nyumbani nikakuta
wametenga maji ya ugali ibidi
wahairishe kupika ugali na wakaanza kunikanda
kwa sasa nashukuru MUNGU naendelea
vizuri ingawa nilipoteza ka simu kangu
ka G-TIDE ka kichina
(simulizi ya kweli) Ilikua jumatano mida ya saa 10 jioni
muda niliokua nimetoka kuoga na
kuvaa nguo nilizozipenda na kuzijali
sana kuliko nguo zangu zote
nakumbuka nilivaa T.shirt ya CCM na
kaptura ya bluu iliyokua imepambwa na viraka viwili kiraka kimoja kikubwa
kilikua sehemu ya makalio na kiraka
kingine kilikua maeneo ya mbele ya
kaptura yangu na kufanya zipu
ishindwe kufunga vizuri
miguuni nilijitupia ndala nyekundu zilizokua zimeisha kwenye visigino
*** *** *** *** ***
Baada za kuhakikisha kua
nimependeza nikaanza safari yangu ya
kwenda internet cafe kwa lengo la
kwenda kuperuzi facebook na ku confirm friends request 15 zilizokua
zikisubiri kujibiwa kwa hamu kubwa
sana
*** *** *** *** ***
Basi wakati naanza kwenda internet
cafe nikaamua nipite vichochoroni ili kukwepa mapaparazi na nyodo za
watoto wakike ili wasije wakanichuna
bure Basi mzee mwenyewe nikaanza safari
ya kwenda cafe kwa mbwembwe zote
huku mkononi nikiwa nimeshika ka
simu kangu ka mchina ka G-TIDE huku
nikiendelea kusikiliza ringtone
*** *** *** *** wakati napita pale uchochoroni
ghaflaaa nikasikia sauti za mahaba
zinatoka kwenye dirisha 1 lililokua
wazi
aseh zile sauti zilinivutia sana ikabidi
niairishe safari yangu na kwenda kuchungulia mle dirishani
daah sikuamini nilichokiona mzee 1
alikua akifanya mapenzi na mkewe
ilibidi nianze kupiga chabo
*** *** *** *** ***
wakati napiga chabo ghaaafla kuna jamaa 1 alikatiza pale uchochoroni kwa
speed kali na kunigonga na kufanya
kale ka G-TIDE kangu ka kichina
kadumbukie mle chumbani
niliacha kupiga chabo na kuanza
kukatoa ka simu kangu *** *** *** *** ***
wakati nahangaika kutoa ka simu
kangu ghaafla likatokea kundi kubwa
la watu waliokua na silaha kali
wakanizunguka na kuanza kunipiga
wakijua mimi ni mwizi aseh lile kundi ndo lilikua likimfukuza
yule jamaa alienigonga kumbe alikua ni
mwizi daah
*** *** *** *** ***
Nilichezea vitasa vya kufa mtu wale
jamaa walinipiga kweli yani walinivimbisha ghaafla wakati
naendelea kupewa vitasa nilianza
kupiga kelele
Mamaa weee nakufaaa
*** *** *** *** ***
Bahati nzuri zile kelele zilimshtua yule mzee aliekua akishughulika na mkewe
zile kelele zilifanya yule mzee ajue
tunapiga chabo daah ghaflaa yule
mzee akatoka na bunduki ya kukoki
kama zile za walinzi na kuja kule
tulipokua da alipofika tu hata hakumsemesha mtu alifyatua risasi juu
na kufanya kila mtu akimbie yaani
uwezi amini pamoja na kupigwa kote
kule mimi ndo nilikua wa kwanza
kukimbia
*** *** *** *** *** Nilikimbia speed 120 ile nafika tu
barabarani nikakutana na yule jamaa
alienigonga na kudumbukiza simu
yangu mle chumbani
Yule jamaa alikuja kunishukuru eti
nimemuokoa aseeh yaani nilitamani nimkate makofi lakini
sikua na nguvu
Ilibidi nirudi nyumbani
wakati nafika nyumbani nikakuta
wametenga maji ya ugali ibidi
wahairishe kupika ugali na wakaanza kunikanda
kwa sasa nashukuru MUNGU naendelea
vizuri ingawa nilipoteza ka simu kangu
ka G-TIDE ka kichina