Inawezekana kabisa hii ni story ya kutunga au umesikia mtu anasimulia ukaidaka bila kujua undani wake. Kama una kitu chochote kinacho-trigger alarm, kwa uzoefu wangu huambiwi rudi kapange tena foleni bali unawekwa pembeni na ''tatizo'' lako linajaribu kutatuliwa hapo kwa hapo chini ya uangalizi wa wakaguzi. Anaweza akatokea mkaguzi akaanza kukuuliza una nini mfukoni, toa mkanda, toa viatu etc. Kiusalama watakuwa wamefanya kosa la kijinga sana ''kukupa'' muda kwa kukuambia rudi, ukapange foleni upya.