Sitasoma tena gazeti la Mawio

MzeePunch

JF-Expert Member
Jun 8, 2009
1,412
203
Leo nilinunua gazeti la Mawio ili kupata uchambuzi kuhusiana na CHADEMA kumpokea mkuu wa mafisadi na kumfanya mgombea wa urais kwa tiketi ya UKAWA.

Lakini badala yake nimekutana na habari nyingi zinazoonesha kusifia na kutetea uamuzi wa fisadi huyo kuingia CHADEMA.

Nilikuwa naliamini gazeti hili kama nilivyokuwa naiamini CHADEMA katika mapambano dhidi ya ufisadi. Sasa kuanzia leo sitanunua wala kusoma tena gazeti hili.

Siku fisadi alipopokelewa CHADEMA nilichana kadi yangu ya uanachama na kuitumbukiza chooni! Sitaki kuwa sehemu ya uchafu unaoendelea hivi sasa ndani ya upinzani.
 
Mimi nilikua nalisoma sana siku nilipoligundua nilichoma yote na sinunui tena'Yaani ni bora hata Tanzania Daima.TARATIIBU watu watamuelewa ZITTO.MBOWE is a very gr8t political entrepreneur........
 
Ndio usisome, wengine tutasoma. Hata CHADEMA hatutaki uiamini. Sisi tutaendelea kuiamini, na tunamuunga mkono mgombea wetu Lowassa. Siyo watu mnakuja na propaganda za upuuzi kutoka CCM, halafu mnajidai ni wapenzi wa CHADEMA. Tumeshawagundua
 
Leo nilinunua gazeti la Mawio ili kupata uchambuzi kuhusiana na Chadema kumpokea mkuu wa mafisadi na kumfanya mgombea wa urais kwa tiketi ya Ukawa. Lakini badala yake nimekutana na habari nyingi zinazoonesha kusifia na kutetea uamuzi wa fisadi huyo kuingia Chadema. Nilikuwa naliamini gazeti hili kama nilivyokuwa naiamini Chadema katika mapambano dhidi ya ufisadi. Sasa kuanzia leo sitanunua wala kusoma tena gazeti hili. Siku fisadi alipopokelewa Chadema nilichana kadi yangu ya uanachama na kuitumbukiza chooni! Sitaki kuwa sehemu ya uchafu unaoendelea hivi sasa ndani ya upinzani.

Mafuriko hayazuiwi kwa mikono! poleee
 
Back
Top Bottom