kookolikoo
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 2,750
- 594
ni kwenye chuo kimoja huko kano. source mwananchi breaking news.
****************************************************
Taarifa Zaidi
****************************************************
Taarifa Zaidi
Mlipuaji wa kujitoa mhanga ameua watu wasiopungua sita katika chuo kikuu kimoja katika mji wa Kano kaskazini mwa Nigeria. Watu wengine kadhaa wamejeruhiwa.
Mlipuko huo umetokea wakati makundi makubwa ya wanafunzi wamekusanyika kutazama matokeo yao kwenye ubao wa matangazo. Watu walioshuhudia wamesema wameona miili ya watu imetapakaa.
Hili ni shambulio la tano mjini Kano tangu siku ya Jumapili. Takriban mashambulio matatu yamefanywa na walipuaji wa kujitoa mhanga wa kike.
Waandishi wa habari wanasema huenda kundi la Boko Haram linahusika na mashambulio hayo.