Azarel
JF-Expert Member
- Aug 25, 2016
- 29,020
- 40,835
Ukweli Mtupu.Moja kati ya mambo ambayo hatupo nayo makini kama waafrika ni msosi. Sijui ni nani aletuambiaga vyakula vinavoongeza nguvu ndo vya maana kuliko vingine.
Watu wanaokula ugali wanaonekana wa maana kuliko watu wa vyakula vingine. Hivi hatujiulizi kama ugali ungekuwa wa maana nchi zilizoendelea si zingechukua na kufanya moja ya chakula chao?
Katoto kadogo hata mwaka mmoja hakajafika vizuri unakatwanga uji, na ugali wa sembe kwa mbali. Ndomana akili zimedumaa, tuchina ni lege lege kweli lakini akili kibao.
Mi sijui hizo nguvu zinatusaidia nini wakati hata kwenye michezo hatufanyi vizuri.
Tunafundishwa masuleni, watoto wadogo wanatakiwa kula sana na kula protein kwa wingi, lakini sisi sasa uji ndo tunaona wa maana na kumfanya mtoto ale mara tatu tu kwa siku.
Wakati tumbo dogo manake linawahi kumeng'enya hivo linahitaji mlo mara nyingi zaidi kuliko tumbo kubwa.
Uji wa mahindi umejaa wanga, sukari ndo carbohydrate yenyewe sasa sijui tunakuza nguruwe. Tuna choroko, maharage, kunde na proteins nyingi kweli lakini kazi ni kuuzia wahindi, sisi wala.
Tuache ujinga vyakula vya kuongeza nguvu vitatufanya tuwe watumwa mpaka mwisho wa dunia.
Inawezekana maendeleo yetu yanashabihiana sana na aina ya vyakula tunavyokula.
Kama unasoma uzi huu, wewe umechelewa ila hakikisha kizazi chako kinaachana na ugali na vyakula visivyomaana.
Nasisi tupate kizazi cha teknolojia kama India na Asia mashariki jamani, achaneni na mavyakula yasio maana.
Tatizo ni ujinga wa kutokujua wala sio pesa.
Mtu anaingia mahali anavuka vibanda ambavyo vina matango, machungwa na maembe yaliyolimwa hapa nchini bila kemikali lakini anakimbilia juice za viwandani zenye kemikali au soda.
Mfano chungwa ni moja kwa sh. 100 lakini unakuta Mtanzania ananunua fanta ya sh. 500 ambapo angekula machungwa matano angekuwa ameongeza vitamin ya kumwongezea immunity.