Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,489
- 40,018
Sijui kama kweli tunataka mabadiliko au tunaombea mabadiliko yatokee. Sijui kama tunafanya ili kusababisha mabadiliko au tunasubiri wengine wafanye ili tufurahie mabadiliko; Sijui hata kama tunajua vizuri ni mabadiliko gani hasa tunayataka na kama tunataka ni juhudi gani tumezifanya kushiriki kwenye mchakato wa kuleta mabadiliko hayo.
Tunaweza kubishana vijiweni na kwenye mitandao na kujaribu kubadilishana mawazo mchana kutwa na usiku kucha lakini mabadiliko hayaji kwa kusema. Mabadiliko hayaji kwa kupigiwa magoti au kwa kukemea giza usiku. Mabadiliko husababishwa na kutekelezwa.
Tukijifunza kwenye kampeni ya Obama utaona kuwa Wamarekani hawakuombea tu kuwa kiongozi mzuri au wamtakaye aje na alipojitokeza hawakukaa pembeni kuombea kuwa afanye vizuri ili hatimaye "alete mabadiliko" wanayoyataka. Wamarekani walishirikishwa katika kampeni kuanzia kuchangia fedha, muda wao, vipaji vyao n.k
Je kwanini tunafikiri sisi Tanzania tutapata mabadiliko kwa kubishana vijiweni na kwenye mitandao na kuoneshana nani anajua nini na anahusika na nini? Mabadiliko ndugu zangu hayaji kwa kunuia au kuwa "kusudio zuri" au kwa kujua ufisadi ulivyo mbaya na fisadi ni nani!!
Mabadiliko huletwa na watu waliokusudia kuleta mabadiliko hayo. Nisikilize.
[mp3]http://mwanakijiji.podomatic.com/enclosure/2009-08-23T18_12_10-07_00.mp3[/mp3]
Simple answer is that most people can talk the talk but can't walk the walk. Ni sawa sawa na baadhi ya viongozi ambao wana pinga ufisadi kwa maneno lakini hawafanyi chochote cha maana kuudhibiti. Watanzania tumezidi sana kupay lip service kutoka kwa viongozi mpaka wananchi wa kawaida. Kudebate is a starting point but what we do after our debates here on JF or else where is what really matters and counts. Ni sawa sawa na upige kelele kiongozi fulani hafai lakini ikija siku ya kupiga kura hauendi kumpinga kwa vitendo unaishia kulala mika tu kwa nini kashinda tena.
Watu washapiga hizo kura na matokeo ya kabadilishwa. CCM na Serikali yake, na hao viongozi hawawezi kuondoka kwa njia ya KURA. Viongozi (Mafisadi) wetu wako tayari kufanya jambo lolote ili imradi wakae madarakani. WTZ hatuna mtu kama Martin Luther King au Gandhi. Kitu kilichobakia ni kupandikiza watu ndani ya CCM in order kuleta mabadiliko.
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu nitakueleza zaidi uzembe wa mwafrika... na hasa Mtanzania. Ni jana tu nilikuwa nimekaa barazani na mshikaji wangu tukipiga domo tukisubiri muda wa futar, unajua tena wengine ndio tupo ktk funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhan..naomba unisiome vizuri mkasa huu maanake una shadidi zake..
Mbele yetu tulipokaa kuna njia panda ya njia nne, yaani makutano ya barabara mbili..na hakuna traffic lights ila stop sign pande zote nne za barabara..
Basi tulikaa kwa muda mrefu sana tukizungumza mambo mengi ya dunia wakati huo huo tukitupia chapuo jinsi jamaa wenzetu (wazungu)walivyokuwa wakiachiana nafasi ya kupita bila kuwepo kwa askari wala mtu kuwaongoza...isipokuwa sheria ya udereva inayosema -First at the junction, has the right of!..
Mara kadhaa magari yalijikusanya wakashindwa kupishana kwa dakika chache kutokana na kwamba pembeni ya makutano hayo kuna sehemu kubwa ya kuegesha magari (Parking Garage), hivyo kuna magari yaliyokuwa yakiingia ku park, menginew kutoka na bado kuna njia panda sehemu hiyo hiyo.. lakini hata hivyo mara zote waliweza kuachiana nafasi tena bila kutumia horn wala mtu kubwatuka kwa hasira na traffic ikaendelea bila tatizo kubwa...
Mara mshikaji wangu akanidokeza na kuuliza what if hali hiyo ingekuwa Bongo... pale pale nika shift akili yangu na kufikiria sehemu kama hizi tanzania huwa vipi?..Nafikiri jibu unalo wala sina haja ya kusimulia maanake magari yetu ktk sehemu kama hiyo yangefunga kila kona na asiondoke mtu kwa sababu ya kuchomekea.. Kila mtu hutaka yeye kuwa wa kwanza kuondoka na mara nyingi sana utagundua kwamba traffic kubwa Tanzania sii swala la kuwa na barabara ndogo au magari mengi wakati wa rush hours isipokuwa uendeshaji wa magari Tanzania ni kinyume cha taratibu, ustaarabu na mara zote tunakwama kwa sababu kila mtu ni mjuaji zaidi ya mwingine. Hivyo mara zote tunapokwama ktk traffic na hasa njia panda sii kwamba watu hawa hawajua wanapotaka kwenda isipokuwa huwekeana kizuizi sisi wenyewe na hatuwezi kuondoka hadi traffic aje kuongoza magari moja baada ya jingine hadi njia itakapo funguka..
Sasa nini mahusiano ya kile tulichokiona jana na mada hii tunayozungumzia maswala ya kubishaa na kadhalika..
Mkuu wangu mara nyingi ni rahisi sana kumwona mtu mwingine mbishi na mbovu wa kufikiri ikiwa tu wewe mwenyewe utaweza kutazama vituko hivyo ukiwa pembeni kaa tulivyokuwa tumekaa sisi pale barazani tukitazama magari..Lakini mara zote wale wanaohusika ktk vituko hivyo, yaani wale wanaoendesha magari na kujikuta wamekwama ktk junction wakichomekeana magari kila mmoja wao humwona mwingine ndiye mkosefu na kibaya zaidi kwa kila inchi ya ardhi inayoachwa wazi mtu mwingine husogeza gari lake..Matokeo yake traffic hukwama pande zote wakashindwa wote kwenda wanakotaka kwenda ktk wakati waliokusudia..
Hii ndio hulka ya Mtanzania hata katika maisha yetu iwe Uchumi, maisha ya kawaida ktk kuparamia daladala kulima kula na kadhalika yaani kila kitu tunachofanya ni vituko vitupu hakuna maarifa, busara wala hekima. Tunapuyanga tu na tunapokwama mara zote hatuwezi kutatua matatizo yetu hadi atokee mtaalam toka nje kutusawazisha Huyo (Traffic Polisi)..
Muda tunaochukua kuparamia daladala kama tukipanda kwa utaratibu watu watakao ondoka ni hesabu ile ile, kuparamia hakuongezi hesabu ya watu, ukubwa wa bus wala kuharakisha safari, isipokuwa kuchelewesha, kukaribisha wizi, (ufisadi) na kuchosha wasafiri maanake ukisha ingia ndani ya dalaldala energy yote imekwisha....
Ukitazama hata Kula chakula, Mdanganyika huwezi kupima tonge lake ..yaani anafukanya utadhani kachangia na mtu sahani yake, tonge tatu tu kafuta sahani nzima within minutes mkuu anatafuta maji.. Lakini ukifikiria kwa makini, mtu akila matonge kumi au matatu hakuna tofauti yoyote ktk kuzidisha au kupunguzxa kipimo, nutrition au muda wa digestion..ya chalula alichokula. Pengine utafikiria ni muda labda anaharakisha apate kurudi kazini haraka, utaambiwa hapana.. Mtanzania lazima apate a nap kila anapomaliza kula chakula cha mchana - at least half hour!..
Kwa hiyo baabu kujaribu kufikiria maswala ya mstkabali wa tanzania ni kazi ambayo inategemea wewe unaendesha gari lako wapi (Mazingira) na kuna WATU gani nyuma ya Usukani wa magari mengineyo..
Ni imani yangu kwamba hadi siku tutakapojifunza discipline, tukaheshimu sheria na taratibu zote.. tukatumia akili zetu kuelewa umuhimu wa ubunifu na matumizi ya elimu ktk utendaji kazi wetu..ndipo tunaweza kutegemea mabadiliko ya aina yoyote ile lakini kama tutaendelea kufikiria kwamba tunaweza kubadilisha maisha yetu kwa kuendelea kuchomekeana ktk njia panda... hakuna mtu atakayetoka..
Mwanakijiji,
Unajisumbua bure kwamba wana JF watafanya mabadiliko kwa kumuunga mtu mpya ambaye hawamfahamu.
Tumezidishiwa ubinafsi na wivu katika mambo yetu yote na hicho ndio kilema kikuu cha sisi Watanzania.
Huku vijijini mtu akifanya jambo lolote la maana watu wataweka majungu tu. Badala ya kuiga na wenyewe wakafanya makubwa zaidi ya hayo wao ni majungu na wivu tu.
Hata hapa JF tumeona siku za karibuni jinsi wana JF hawa hawa walivyoamua kuwabomoa baadhi ya wana JF wenzao kwa kutumia majungu.
Sisi kazi zetu ni kuimba nyimbo zile ambazo tayari zipo. Kama Dr. Salaa kajitengenezea jina lake basi sisi tutaanza kuimba wimbo huo huo. Akitokea kijana mdogo kama Zitto anataka kumpinga basi hapo kutakuwa na maneno kibao na kila sababu ya visingizio.
Amkeni na nendeni kufanya mabadiliko kwenye sehemu zenu badala ya kukaa hapa tu na kuandika mbovu mbovu.
Kumbukeni Obama hakuwa na jina kubwa kabla ya kuanza kugombea. Watu waliona ana uwezo lakini hakuwa tested kabla ya hapo na bado walimwunga mkono na kuwaacha wenye majina. Mabadili hayaji kwa kufuata mambo yale yale.
Historia inaionyesha mapinduzi huja baada ya watu kuamua wanataka kuona mabadiliko. Hata hivyo lazima tujue there is a space between stimulus and response.MABADILIKO MAZURI na ya KUDUMU ni yale yanayokuja YENYEWE bila ya SHINIKIZO, CHAGIZO au KULAZIMISHWA. Kwa Tanzania mabadiliko haya hayako MBALI ili mradi tumeanza kuona wapi tulikuwa, tulipo na tunakojaribu kwenda. Tuvute subira tu na kutakiana HERI na AMANI. Bahati nzuri mabadiliko ya kuja yenyewe yanawaumiza wachache ambao wanajaribu kukinzana nayo.
tatizo hao 'wapiganaji' wakereketwa wengi wako ughaibuni. sasa ni kama kitendo cha mtu kutupa mawe gizani. mje bongo muonekane kama wanasiasa na wataalam wengine. kutumia remote control si jambo la msingi
Sijui kama kweli tunataka mabadiliko au tunaombea mabadiliko yatokee. Sijui kama tunafanya ili kusababisha mabadiliko au tunasubiri wengine wafanye ili tufurahie mabadiliko; Sijui hata kama tunajua vizuri ni mabadiliko gani hasa tunayataka na kama tunataka ni juhudi gani tumezifanya kushiriki kwenye mchakato wa kuleta mabadiliko hayo.
Tunaweza kubishana vijiweni na kwenye mitandao na kujaribu kubadilishana mawazo mchana kutwa na usiku kucha lakini mabadiliko hayaji kwa kusema. Mabadiliko hayaji kwa kupigiwa magoti au kwa kukemea giza usiku. Mabadiliko husababishwa na kutekelezwa.
Tukijifunza kwenye kampeni ya Obama utaona kuwa Wamarekani hawakuombea tu kuwa kiongozi mzuri au wamtakaye aje na alipojitokeza hawakukaa pembeni kuombea kuwa afanye vizuri ili hatimaye "alete mabadiliko" wanayoyataka. Wamarekani walishirikishwa katika kampeni kuanzia kuchangia fedha, muda wao, vipaji vyao n.k
Je kwanini tunafikiri sisi Tanzania tutapata mabadiliko kwa kubishana vijiweni na kwenye mitandao na kuoneshana nani anajua nini na anahusika na nini? Mabadiliko ndugu zangu hayaji kwa kunuia au kuwa "kusudio zuri" au kwa kujua ufisadi ulivyo mbaya na fisadi ni nani!!
Mabadiliko huletwa na watu waliokusudia kuleta mabadiliko hayo.
Nisikilize:
[mp3]http://mwanakijiji.podomatic.com/enclosure/2009-08-23T18_12_10-07_00.mp3[/mp3]
Tunaweza kubishana vijiweni na kwenye mitandao na kujaribu kubadilishana mawazo mchana kutwa na usiku kucha lakini mabadiliko hayaji kwa kusema. Mabadiliko hayaji kwa kupigiwa magoti au kwa kukemea giza usiku. Mabadiliko husababishwa na kutekelezwa.
Je kwanini tunafikiri sisi Tanzania tutapata mabadiliko kwa kubishana vijiweni na kwenye mitandao na kuoneshana nani anajua nini na anahusika na nini? Mabadiliko ndugu zangu hayaji kwa kunuia au kuwa "kusudio zuri" au kwa kujua ufisadi ulivyo mbaya na fisadi ni nani!!
Mabadiliko huletwa na watu waliokusudia kuleta mabadiliko hayo.
[mp3]http://mwanakijiji.podomatic.com/enclosure/2009-08-23T18_12_10-07_00.mp3[/mp3]