maharage ya ukweni
JF-Expert Member
- Aug 25, 2016
- 1,231
- 2,400
Rupia pamoja hela fulani za zamani ambazo zinatafutwa sana na watu hata kwakununuliwa kwa mabilioni ya fedha kuna uhusiano fulani na baraka za kutoka kwa mungu.Hili swala nalizungumzia kwa ushahidi ambao umenitokea baada ya kuota nimeokota rupia kwenye mchanga,niliota mara mbili mara ya kwanza niliota nimeokota rupia baada ya kuingiza mkono wangu na kufukua kwenye mchanga mwingi.Siku iliyofuata ninilipewa kiasi kikubwa cha pesa ambacho nilimuomba tajiri mmoja mkubwa mionogoni mwa matajiri hapa Tanzania.
Mara ya pili niliota niko msikitini nasubiri kuswali jamaa na nilikua nina msongo mubwa sana wa mawazo kutokana na maisha yangu kua magumu na wala hakuna mtu wenye uwezo katika familia yangu ambaye ana nia ya kunisaidia ili nipate nafuu ya maisha.Basi nilivyotoka msikitini nje nilikutana na mtu sio mzungu,mwarabu,muhindi wala mchina basi nikamsalimia baada ya hapo yule mtu akanipa rupia tatu moja iliyokua juu ilikua na picha ya Eagle basi nikawa nazishangaa sana zile hela huku nasema hizi hela zinatafutwa sana na mtu ukizipata unakua tajiri nikiwa nimeinama naziaangalia zile hela kwenye kiganja changu cha mkono.
Nikasikia yule mtu ananiambia usishangae wewe nenda,yule mtu na yeye alikua anatoka msikitini na kuelekea kule ambako mimi naelekea.Basi nilivyonyenyua kichwa niende nikaangalia mbele lakini kilichonishangaza yule mtu sikumuona na mbele yangu hakukua na nyumba wala kichochoro na hata yule mtu angekua anakimbia kama Usain Bolt bado ningemuona.Basi kuanzia nilivyoamka mpaka leo hali yangu ya kimaisha inaonesha ntakua na maisha mazuri sana baadae inshaalah kwani nimepata nafasi ya kazi ambayo kuipata ni vigumu sana
Kwa ndoto hizi mbili nimegundua kua kuna uhusiano mkubwa sana kati ya baraka za mungu na rupia kwani mimi sio mshirikina,swala tano na sunnah juu.pia nimegundua nina nguvu sana ambazo mungu amenijaalia na kuna watu wamegundua kua nina future nzuri ndio maana nilikua najiuliza mimi masikini lakini mbona nafanyiwa sana fitina,nachukiwa bila ya sababu za msingi mpaka na watu ambao maisha yao ni mazuri sana.Jamani nawashauri dunia isitudanganye tumrudie mungu kwani maisha baada ya kifo yapo na mungu ndio kila kitu,riziki anatoa mungu na akisema kua basi inakua na hakuna ambaye anaweza uzuia
Mara ya pili niliota niko msikitini nasubiri kuswali jamaa na nilikua nina msongo mubwa sana wa mawazo kutokana na maisha yangu kua magumu na wala hakuna mtu wenye uwezo katika familia yangu ambaye ana nia ya kunisaidia ili nipate nafuu ya maisha.Basi nilivyotoka msikitini nje nilikutana na mtu sio mzungu,mwarabu,muhindi wala mchina basi nikamsalimia baada ya hapo yule mtu akanipa rupia tatu moja iliyokua juu ilikua na picha ya Eagle basi nikawa nazishangaa sana zile hela huku nasema hizi hela zinatafutwa sana na mtu ukizipata unakua tajiri nikiwa nimeinama naziaangalia zile hela kwenye kiganja changu cha mkono.
Nikasikia yule mtu ananiambia usishangae wewe nenda,yule mtu na yeye alikua anatoka msikitini na kuelekea kule ambako mimi naelekea.Basi nilivyonyenyua kichwa niende nikaangalia mbele lakini kilichonishangaza yule mtu sikumuona na mbele yangu hakukua na nyumba wala kichochoro na hata yule mtu angekua anakimbia kama Usain Bolt bado ningemuona.Basi kuanzia nilivyoamka mpaka leo hali yangu ya kimaisha inaonesha ntakua na maisha mazuri sana baadae inshaalah kwani nimepata nafasi ya kazi ambayo kuipata ni vigumu sana
Kwa ndoto hizi mbili nimegundua kua kuna uhusiano mkubwa sana kati ya baraka za mungu na rupia kwani mimi sio mshirikina,swala tano na sunnah juu.pia nimegundua nina nguvu sana ambazo mungu amenijaalia na kuna watu wamegundua kua nina future nzuri ndio maana nilikua najiuliza mimi masikini lakini mbona nafanyiwa sana fitina,nachukiwa bila ya sababu za msingi mpaka na watu ambao maisha yao ni mazuri sana.Jamani nawashauri dunia isitudanganye tumrudie mungu kwani maisha baada ya kifo yapo na mungu ndio kila kitu,riziki anatoa mungu na akisema kua basi inakua na hakuna ambaye anaweza uzuia