Simulizi za Patrick Ck
New Member
- Nov 25, 2022
- 2
- 2
SIRI YA MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
( SIMULIZI YA KIJASUSI
EP 01
ARUSHA
Kikao cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kilichofanyika katika makao makuu ya Jumuiya hiyo yaliyopo Arusha Tanzania kilimalizika kwa mafanikio makubwa. Kikao hicho cha kawaida kilichohudhuliwa na marais kutoka nchi zote sita zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki, kilipokea na kujadili taarifa mbalimbali zinazohusu jumuia
hiyo ikiwamo taarifa kuhusiana na mchakato wa uanzishwaji wa sarafu moja ya Afrika Mashariki ulikofikia.
Kikao hicho pia kilijadili ombi la nchi ya jamhuri ya kidemokrasi ya Congo kujiunga na Jumuiya hiyo na kuikubali kuwa mwanachama wa saba wa Jumuiya hiyo.
Jambo lingine lililofanyika katika kikao hicho ni nchi ya Tanzania kuchukua nafasi ya uenyekiti wa Jumuiya kwa muda wa mwaka mmoja. Baada ya kikao kumalizika na wakuu wa nchi kuzungumza na wana habari
kuhusu yale yaliyojiri katika kikao hicho, wakuu wote wa nchi walielekea katika hoteli ya Kobe Village kwa ajili ya kupata chakula cha mchana na baada ya chakula baadhi ya wakuu wa nchi waliondoka na walibaki wachache waliokuwa na mazungumzo binafsi na Rais wa Tanzania na baada ya kumaliza mazungumzo yao marais wa Kenya na Burundi wakaondoka akabaki Rais Patrice Eyenga wa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ambaye alikuwa na mazungumzo binafsi na mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki rais wa Tanzania Dr Fabian Kelelo. Dr Fabian alimkaribisha Rais Patrice katika chumba chake kwenye hoteli kubwa Jijini Arusha Kobe village kwa ajili ya mazungumzo maalum.
Walinzi wote wa marais hawa wawili wakabaki nje na kuwapa nafasi wakuu wao wazungumze faragha.
JE WANA MAZUNGUMZO GANI? USIKOSE MWENDELEZO.
( SIMULIZI YA KIJASUSI
EP 01
ARUSHA
Kikao cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kilichofanyika katika makao makuu ya Jumuiya hiyo yaliyopo Arusha Tanzania kilimalizika kwa mafanikio makubwa. Kikao hicho cha kawaida kilichohudhuliwa na marais kutoka nchi zote sita zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki, kilipokea na kujadili taarifa mbalimbali zinazohusu jumuia
hiyo ikiwamo taarifa kuhusiana na mchakato wa uanzishwaji wa sarafu moja ya Afrika Mashariki ulikofikia.
Kikao hicho pia kilijadili ombi la nchi ya jamhuri ya kidemokrasi ya Congo kujiunga na Jumuiya hiyo na kuikubali kuwa mwanachama wa saba wa Jumuiya hiyo.
Jambo lingine lililofanyika katika kikao hicho ni nchi ya Tanzania kuchukua nafasi ya uenyekiti wa Jumuiya kwa muda wa mwaka mmoja. Baada ya kikao kumalizika na wakuu wa nchi kuzungumza na wana habari
kuhusu yale yaliyojiri katika kikao hicho, wakuu wote wa nchi walielekea katika hoteli ya Kobe Village kwa ajili ya kupata chakula cha mchana na baada ya chakula baadhi ya wakuu wa nchi waliondoka na walibaki wachache waliokuwa na mazungumzo binafsi na Rais wa Tanzania na baada ya kumaliza mazungumzo yao marais wa Kenya na Burundi wakaondoka akabaki Rais Patrice Eyenga wa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ambaye alikuwa na mazungumzo binafsi na mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki rais wa Tanzania Dr Fabian Kelelo. Dr Fabian alimkaribisha Rais Patrice katika chumba chake kwenye hoteli kubwa Jijini Arusha Kobe village kwa ajili ya mazungumzo maalum.
Walinzi wote wa marais hawa wawili wakabaki nje na kuwapa nafasi wakuu wao wazungumze faragha.
JE WANA MAZUNGUMZO GANI? USIKOSE MWENDELEZO.