Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,315
- 33,109
Kura kumkataa Pinda kumbe ilimlenga Rais Kikwete
Filikunjombe: Angezungumza Zitto isingekuwa na nguvu
Makinda awashukia mawaziri wanaojisafisha nje ya Bunge
Rais Jakaya Kikwete
Imebainika kuwa mkakati wa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ulimlenga Rais Jakaya Kikwete.
Mkakati huo uliandaliwa ukiwa ni sehemu ya kushinikiza kutimuliwa kutoka kwenye nyadhifa zao, mawaziri waliotajwa kuhusika kwa namna tofauti katika wizi na ubadhirifu wa mali za umma.
Hata hivyo mkakati huo unadaiwa kuvujishwa kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, hivyo kuibua hoja ya kupiga kura hiyo, ikimuelekea Waziri Mkuu, Pinda.
Hayo yamebainika huku Kamati Kuu (CC) ya CCM ikiridhia mpango wa Rais Kikwete kuwashughulikia mawaziri wanaotajwa katika kashfa hizo na kulisuka upya Baraza la Mawaziri.
Mawaziri wanaotakiwa kujiuzulu kutokana na kashfa tofauti ni Mustafa Mkulo (Fedha na Uchumi) Cyril Chami (Viwanda na Biashara) William Ngeleja (Nishati na Madini) na Omar Nundu (Uchukuzi).
Wengine ni Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii), George Mkuchika (Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), Profesa Jumanne Maghembe (Kilimo Chakula na Ushirika) na Dk. Haji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii).
Hata hivyo, kwenye orodha hiyo anatajwa pia Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara ambaye pia ni Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu.
Habari za uhakika kutoka ndani ya wabunge wa CCM walioasisi mkakati huo, kisha ukakubalika kwa idadi kubwa miongoni mwao, zilieleza kuwa kura ya kutokuwa na imani ilipangwa kupigwa dhidi ya Rais Kikwete.
Hali hiyo ilifikiwa kama sehemu ya kumshinikiza awawajibishe mawaziri wanaotuhumiwa kwa wizi na ubadhirifu wa mali za umma.
Lengo la awali lilikuwa kutumia kanuni za Bunge zinazohalalisha kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais Kikwete, lakini tukaliona hilo ni jambo kubwa sana hivyo tukaamua kumheshimu Rais wetu, kilieleza chanzo chetu kutoka miongoni mwa wabunge wa CCM.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, wabunge wa CCM walielezea kumheshimu Rais Kikwete hivyo kuondokana na azma ya kumpigia kura hiyo, ndipo ikatafutwa mbinu mbadala ya kushinikiza kuondolewa kwa mawaziri hao.
Hivyo mkakati wa kutokuwa na imani na Waziri Mkuu haina maana kwamba Pinda ana makosa, bali ni mchakato utakaofanikisha kujiuzulu kwa mawaziri husika, kilieleza chanzo chetu.
SPIKA MAKINDA AWASHUKIA MAWAZIRI
Spika wa Bunge, Anne Makinda, amesema kitendo cha baadhi ya mawaziri waliotakiwa kuwajibika kutokana na ubadhirifu wa fedha za umma, kujitetea nje ya chombo hicho cha uwakilishi wa wananchi, hakina mantiki bali kukidhi utashi binafsi.
Akizungumza kwa njia ya simu na NIPASHE Jumapili juzi, Makinda alisema kauli za kukanusha taarifa zilizowasilishwa bungeni ama kutoa vielelezo kwa lengo la kujiweka kando ya tuhuma zilizotolewa hakuathiri mambo yaliyoamuliwa ndani ya Bunge.
Ingawa Makinda hakutaja majina ya mawaziri wahusika, lakini mmoja wao ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, ambaye alikaririwa akipinga
tuhuma zilizotolewa bungeni dhidi yake.
Maige ameonekana na kusikika kwenye vyombo kadhaa vya habari, akikanusha tuhuma dhidi yake na kusema huenda kuna mkakati wenye lengo la kisiasa, vinginevyo yeye ni mtu safi.
Hayo yanayoendelea nje ya Bunge hayawezi kushawishi mambo yaliyoamuliwa bungeni, yale yanayosemwa huko hayawezi kubadilisha msimamo tuliofikia, alisema.
Makinda alisema ripoti zote zilizowasilishwa bungeni, kujadiliwa na kutolewa maagizo haziwezi kubadilika ama kuathiriwa na matukio yanayotokea nje ya Bunge.
Alisema kitendo cha Waziri kutoa ufafanuzi ama kuzungumzia mambo yanayomhusu, ni moja ya haki zake kwa vile hakuna mamlaka yenye kumziba mdomo.
Bunge haliwezi kumziba mtu mdomo kwa sababu kila mtu ana uhuru wake wa kuzungumza, kwa hiyo waendelee tu kuzungumza lakini msimamo wa Bunge upo pale pale, alisema.
FILIKUNJOMBE ANENA
Mbunge wa Ludewa (CCM) aliyekuwa mmoja wa walioshinikiza kuondoka madarakani kwa mawaziri wanaotuhumiwa, alisema hatua hiyo itaiweka CCM kukubalika katika jamii na kuwa na uhakika zaidi wa kudumu madarakani.
Akizungumza katika mahojiano maalum ya NIPASHE Jumapili jijini Dar es Salaam juzi, Filikunjombe alisema tuhuma zinazowakabili mawaziri husika ni moja ya maeneo yanayoiathiri jamii pana ya Tanzania hivyo hakuna sababu ya kuweka mbele maslahi ya kisiasa.
Alisema kama hoja ya kuwataka mawaziri kujiuzulu ingesimamiwa kidete na wabunge wa upinzani, isingekuwa na nguvu kama ilivyotokea kwa upande wa CCM.
Hoja hii ingesimamiwa na akina Zitto Kabwe isingekuwa na nguvu kwa maana watu wangesema ni kawaida ya upinzani, lakini wabunge wa CCM tuliposimama na kuzungumza, imeleta matokeo makubwa, alisema.
Filikunjombe alisema hali ya ustawi wa jamii imedumaa huku baadhi ya viongozi wa serikali wakiwemo mawaziri wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wakijilimbizia mali kinyume cha sheria.
Tunapokuwa majimboni kama kule kwangu Ludewa, wananchi wanahoji kuhusu ukosefu wa huduma bora za afya, elimu, miundombinu na maji safi na salama, alisema.
Aliongeza, kwa hali ilivyo sasa na hulka hii ya mawaziri wasiokuwa waaminifu kuhujumu rasilimali za nchi, si rahisi kuyafikia maisha bora kwa kila Mtanzania.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Rais Jakaya Kikwete
Imebainika kuwa mkakati wa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ulimlenga Rais Jakaya Kikwete.
Mkakati huo uliandaliwa ukiwa ni sehemu ya kushinikiza kutimuliwa kutoka kwenye nyadhifa zao, mawaziri waliotajwa kuhusika kwa namna tofauti katika wizi na ubadhirifu wa mali za umma.
Hata hivyo mkakati huo unadaiwa kuvujishwa kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, hivyo kuibua hoja ya kupiga kura hiyo, ikimuelekea Waziri Mkuu, Pinda.
Hayo yamebainika huku Kamati Kuu (CC) ya CCM ikiridhia mpango wa Rais Kikwete kuwashughulikia mawaziri wanaotajwa katika kashfa hizo na kulisuka upya Baraza la Mawaziri.
Mawaziri wanaotakiwa kujiuzulu kutokana na kashfa tofauti ni Mustafa Mkulo (Fedha na Uchumi) Cyril Chami (Viwanda na Biashara) William Ngeleja (Nishati na Madini) na Omar Nundu (Uchukuzi).
Wengine ni Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii), George Mkuchika (Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), Profesa Jumanne Maghembe (Kilimo Chakula na Ushirika) na Dk. Haji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii).
Hata hivyo, kwenye orodha hiyo anatajwa pia Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara ambaye pia ni Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu.
Habari za uhakika kutoka ndani ya wabunge wa CCM walioasisi mkakati huo, kisha ukakubalika kwa idadi kubwa miongoni mwao, zilieleza kuwa kura ya kutokuwa na imani ilipangwa kupigwa dhidi ya Rais Kikwete.
Hali hiyo ilifikiwa kama sehemu ya kumshinikiza awawajibishe mawaziri wanaotuhumiwa kwa wizi na ubadhirifu wa mali za umma.
Lengo la awali lilikuwa kutumia kanuni za Bunge zinazohalalisha kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais Kikwete, lakini tukaliona hilo ni jambo kubwa sana hivyo tukaamua kumheshimu Rais wetu, kilieleza chanzo chetu kutoka miongoni mwa wabunge wa CCM.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, wabunge wa CCM walielezea kumheshimu Rais Kikwete hivyo kuondokana na azma ya kumpigia kura hiyo, ndipo ikatafutwa mbinu mbadala ya kushinikiza kuondolewa kwa mawaziri hao.
Hivyo mkakati wa kutokuwa na imani na Waziri Mkuu haina maana kwamba Pinda ana makosa, bali ni mchakato utakaofanikisha kujiuzulu kwa mawaziri husika, kilieleza chanzo chetu.
SPIKA MAKINDA AWASHUKIA MAWAZIRI
Spika wa Bunge, Anne Makinda, amesema kitendo cha baadhi ya mawaziri waliotakiwa kuwajibika kutokana na ubadhirifu wa fedha za umma, kujitetea nje ya chombo hicho cha uwakilishi wa wananchi, hakina mantiki bali kukidhi utashi binafsi.
Akizungumza kwa njia ya simu na NIPASHE Jumapili juzi, Makinda alisema kauli za kukanusha taarifa zilizowasilishwa bungeni ama kutoa vielelezo kwa lengo la kujiweka kando ya tuhuma zilizotolewa hakuathiri mambo yaliyoamuliwa ndani ya Bunge.
Ingawa Makinda hakutaja majina ya mawaziri wahusika, lakini mmoja wao ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, ambaye alikaririwa akipinga
tuhuma zilizotolewa bungeni dhidi yake.
Maige ameonekana na kusikika kwenye vyombo kadhaa vya habari, akikanusha tuhuma dhidi yake na kusema huenda kuna mkakati wenye lengo la kisiasa, vinginevyo yeye ni mtu safi.
Hayo yanayoendelea nje ya Bunge hayawezi kushawishi mambo yaliyoamuliwa bungeni, yale yanayosemwa huko hayawezi kubadilisha msimamo tuliofikia, alisema.
Makinda alisema ripoti zote zilizowasilishwa bungeni, kujadiliwa na kutolewa maagizo haziwezi kubadilika ama kuathiriwa na matukio yanayotokea nje ya Bunge.
Alisema kitendo cha Waziri kutoa ufafanuzi ama kuzungumzia mambo yanayomhusu, ni moja ya haki zake kwa vile hakuna mamlaka yenye kumziba mdomo.
Bunge haliwezi kumziba mtu mdomo kwa sababu kila mtu ana uhuru wake wa kuzungumza, kwa hiyo waendelee tu kuzungumza lakini msimamo wa Bunge upo pale pale, alisema.
FILIKUNJOMBE ANENA
Mbunge wa Ludewa (CCM) aliyekuwa mmoja wa walioshinikiza kuondoka madarakani kwa mawaziri wanaotuhumiwa, alisema hatua hiyo itaiweka CCM kukubalika katika jamii na kuwa na uhakika zaidi wa kudumu madarakani.
Akizungumza katika mahojiano maalum ya NIPASHE Jumapili jijini Dar es Salaam juzi, Filikunjombe alisema tuhuma zinazowakabili mawaziri husika ni moja ya maeneo yanayoiathiri jamii pana ya Tanzania hivyo hakuna sababu ya kuweka mbele maslahi ya kisiasa.
Alisema kama hoja ya kuwataka mawaziri kujiuzulu ingesimamiwa kidete na wabunge wa upinzani, isingekuwa na nguvu kama ilivyotokea kwa upande wa CCM.
Hoja hii ingesimamiwa na akina Zitto Kabwe isingekuwa na nguvu kwa maana watu wangesema ni kawaida ya upinzani, lakini wabunge wa CCM tuliposimama na kuzungumza, imeleta matokeo makubwa, alisema.
Filikunjombe alisema hali ya ustawi wa jamii imedumaa huku baadhi ya viongozi wa serikali wakiwemo mawaziri wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wakijilimbizia mali kinyume cha sheria.
Tunapokuwa majimboni kama kule kwangu Ludewa, wananchi wanahoji kuhusu ukosefu wa huduma bora za afya, elimu, miundombinu na maji safi na salama, alisema.
Aliongeza, kwa hali ilivyo sasa na hulka hii ya mawaziri wasiokuwa waaminifu kuhujumu rasilimali za nchi, si rahisi kuyafikia maisha bora kwa kila Mtanzania.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI