Jokajeusi
JF-Expert Member
- Jun 1, 2018
- 6,336
- 10,895
Habari Wakuu!
Katika uzi huu nitajaribu kueleza chanzo kikuu cha watu kuchapiwa au kuibiwa wake zao. Lengo la uzi huu si kuleta mitafaruku ndani ya ndoa bali kuishi kwa kufuata misingi mikuu ya maisha ili kufurahia maisha yetu.
Hakuna jambo linalouma kama kuchapiwa, kupigiwa, kulambiwa mke wako umpendae kwa dhati. Mke ambaye unahangaika kutwa kucha kuhakikisha nafurahia maisha. Kiukweli inauma sana na kama hutokuwa na busara basi madhara makubwa huweza kutokea.
Mwanamke hupenda kupendwa, hupenda kuhisi, kusikia, na kuona yakuwa mume wake anampenda. Na wanaume kiasili wanapenda kuona wake zao wakifurahi na wakipendeza. Pia wanaume wanapenda kusikilizwa, kunyenyekewa na kuabudiwa.
Siku hizi watu huhangaika na madawa kuwaridhisha wanawake. Biashara hii imekuwa biashara kubwa ulimwenguni. Na makampuni mamia yameundwa na yananufaika na dawa za nguvu za kiume.
Zipo Siri Kuu mbili ambazo ni chanzo cha wanaume wengi kuchapiwa Mke wako:
1. Kutokushika Amri za Mungu
Hii ni siri ya kwanza, Ikiwa hushiki amri za Mungu na unazivunja kwa makusudi kabisa. Tegemea Usaliti wa kipekee kwa mke wako. Mwanamke lazima achepuke na mwanaume mwingine. Kuchapiwa ni moja ya adhabu kubwa apewayo mtu na Mungu wake. Huwezi ukachapiwa ikiwa unashika amri za Mungu. Haijalishi una kibamia, haijlishi huna pesa, haijalishi wewe una mapungufu kiasi gani. Ilimradi unatimiza mapenzi ya Mungu na unahaja ya kuyafanya basi huwezi kuchapiwa. Amini usiamini ukichapiwa jua hiyo ni adhabu kubwa upewayo na Mungu. Mungu anajua maumivu ya mapenzi yalivyo hivyo adhabu hii ni mahususi na kubwa kama vile maradhi.
Mke wa TAJIRI anaweza akachapwa, Mke wa Waziri, Rais, na Viongozi wakubwa huweza kupigwa tuu na hata kuleta watoto wa nje. Mke wa Wana muziki mashuhuri na maarufu huliwa tuu bila tabu yoyote ikiwa watu hao hawafuati sheria za Mungu. Ila Mke wa Mtu ashikaye sheria na maagizo ya Mungu hawezi kuchapiwa kamwe. Mungu ameichagua adhabu hii mahususi kuutesa moyo wa watu wakaidi. Zipo adhabu za mwili kama Magonjwa, njaa na kadhalika. Ila Adhabu za moyo ambazo ni za kihisia ni usaliti wa mapenzi. Ibrahimu mke wake alikoswa koswa na Mfalme almanusura alambwe lakini Mungu aliingilia kati. Wanaoifahamu hii stori wataungana nami. Huwezi ukala na mke wa Mtu wa Mungu ukasimamisha au ukabaki salama.
Kumbukumbu la torati 28:
30 Utaposa mke na mume mwingine atalala naye; utajenga nyumba usiikae; utapanda mizabibu usitumie matunda yake.
41 Utazaa wana na binti, lakini hawatakuwa wako wewe; kwa sababu watakwenda utumwani.
2. Kutokuoa Mwanamke Bikira
Jamani kuna watu humu wanadhani nimekuja kuwatukana au kukejeli. Hapana kwani kwanza hatufahamiana. Lengo ni kurudisha jamii ikae kwenye mstari. Bikra ni muhimu, nasisitiza Bikra ni muhimu sana. Mama unayesoma hapa. Mlinde mwanao kwa jina la mwenyezi Mungu naye atabaki salama.
Watu wana hangaika kutumia mitishamba ili wawaridhishe wanawake, ndugu zangu mwanamke hata ridhika kama hakuwa wako. Take from me. Haijalishi utamsugua kiasi gani lakini hiyo si muarobaini wa yeye kutokuonja vya nje.
Kijana ambaye haujaoa, shika sana maneno haya ni muhimu kwa maisha yako yote. Shika amri za Mungu na maagizo yake na Oa Bikra. Huwezi kujuta.
Hivyo jukumu la mwanamke ni kutunza bikra yake kwa vyovyote hata atakapoolewa na jukumu la mwanaume ni kushika amri za Mungu na kuoa Bikra.
Nakaribisha Hoja
Katika uzi huu nitajaribu kueleza chanzo kikuu cha watu kuchapiwa au kuibiwa wake zao. Lengo la uzi huu si kuleta mitafaruku ndani ya ndoa bali kuishi kwa kufuata misingi mikuu ya maisha ili kufurahia maisha yetu.
Hakuna jambo linalouma kama kuchapiwa, kupigiwa, kulambiwa mke wako umpendae kwa dhati. Mke ambaye unahangaika kutwa kucha kuhakikisha nafurahia maisha. Kiukweli inauma sana na kama hutokuwa na busara basi madhara makubwa huweza kutokea.
Mwanamke hupenda kupendwa, hupenda kuhisi, kusikia, na kuona yakuwa mume wake anampenda. Na wanaume kiasili wanapenda kuona wake zao wakifurahi na wakipendeza. Pia wanaume wanapenda kusikilizwa, kunyenyekewa na kuabudiwa.
Siku hizi watu huhangaika na madawa kuwaridhisha wanawake. Biashara hii imekuwa biashara kubwa ulimwenguni. Na makampuni mamia yameundwa na yananufaika na dawa za nguvu za kiume.
Zipo Siri Kuu mbili ambazo ni chanzo cha wanaume wengi kuchapiwa Mke wako:
1. Kutokushika Amri za Mungu
Hii ni siri ya kwanza, Ikiwa hushiki amri za Mungu na unazivunja kwa makusudi kabisa. Tegemea Usaliti wa kipekee kwa mke wako. Mwanamke lazima achepuke na mwanaume mwingine. Kuchapiwa ni moja ya adhabu kubwa apewayo mtu na Mungu wake. Huwezi ukachapiwa ikiwa unashika amri za Mungu. Haijalishi una kibamia, haijlishi huna pesa, haijalishi wewe una mapungufu kiasi gani. Ilimradi unatimiza mapenzi ya Mungu na unahaja ya kuyafanya basi huwezi kuchapiwa. Amini usiamini ukichapiwa jua hiyo ni adhabu kubwa upewayo na Mungu. Mungu anajua maumivu ya mapenzi yalivyo hivyo adhabu hii ni mahususi na kubwa kama vile maradhi.
Mke wa TAJIRI anaweza akachapwa, Mke wa Waziri, Rais, na Viongozi wakubwa huweza kupigwa tuu na hata kuleta watoto wa nje. Mke wa Wana muziki mashuhuri na maarufu huliwa tuu bila tabu yoyote ikiwa watu hao hawafuati sheria za Mungu. Ila Mke wa Mtu ashikaye sheria na maagizo ya Mungu hawezi kuchapiwa kamwe. Mungu ameichagua adhabu hii mahususi kuutesa moyo wa watu wakaidi. Zipo adhabu za mwili kama Magonjwa, njaa na kadhalika. Ila Adhabu za moyo ambazo ni za kihisia ni usaliti wa mapenzi. Ibrahimu mke wake alikoswa koswa na Mfalme almanusura alambwe lakini Mungu aliingilia kati. Wanaoifahamu hii stori wataungana nami. Huwezi ukala na mke wa Mtu wa Mungu ukasimamisha au ukabaki salama.
Kumbukumbu la torati 28:
30 Utaposa mke na mume mwingine atalala naye; utajenga nyumba usiikae; utapanda mizabibu usitumie matunda yake.
41 Utazaa wana na binti, lakini hawatakuwa wako wewe; kwa sababu watakwenda utumwani.
2. Kutokuoa Mwanamke Bikira
Jamani kuna watu humu wanadhani nimekuja kuwatukana au kukejeli. Hapana kwani kwanza hatufahamiana. Lengo ni kurudisha jamii ikae kwenye mstari. Bikra ni muhimu, nasisitiza Bikra ni muhimu sana. Mama unayesoma hapa. Mlinde mwanao kwa jina la mwenyezi Mungu naye atabaki salama.
Watu wana hangaika kutumia mitishamba ili wawaridhishe wanawake, ndugu zangu mwanamke hata ridhika kama hakuwa wako. Take from me. Haijalishi utamsugua kiasi gani lakini hiyo si muarobaini wa yeye kutokuonja vya nje.
Kijana ambaye haujaoa, shika sana maneno haya ni muhimu kwa maisha yako yote. Shika amri za Mungu na maagizo yake na Oa Bikra. Huwezi kujuta.
Hivyo jukumu la mwanamke ni kutunza bikra yake kwa vyovyote hata atakapoolewa na jukumu la mwanaume ni kushika amri za Mungu na kuoa Bikra.
Nakaribisha Hoja