Siri ya Kikwete TRA yaanikwa

Siri ya Kikwete TRA yaanikwa

Kama Kikwete alikuwa hafai kwa nini wana CCM walikuwa wanampamba kwa nyimbo kama vile ni malaika aliyekuwa ametumwa kukomboa Tanzania.
Ndio maana huwa nawaita CCM misukule......wanafanya wasiyoyataka,ili mradi bwana mkubwa afurahi.
 
Kwa kuwa jana amenukuliwa akisema hana cha kuchomoa kwa kuwa hana alichochomeka na kama amechomeka yeye hajui amechomekaje, basi atambue kuwa hiki ndicho kilichomaanishwa na si maneno yake ya Pwani yanayoashiria tabia fulani ambazo amekuwa akisemwa kuwa nazo za lambalamba apitaye...
 
Mnanikumbusha wakati mkapa anaingia madarakani Mwinyi alichafuliwa hadi kunuka ... Mkapa alipotoka madarakani ikawa kimya huku akiwa ameuza nchi !!! Leo ametoka Kikwete Madarakani lazima anuke .... Chezea Roman Empire wewe ...
Mawazo kama haya ni balaa......hata wasio Roman wenye imani kama yako wanaona kabisa Tanzania ilikuwa inadidimia chini ya huyo unayejaribu kumtetea, pole kama umeguswa na speed ya Magufuli ila ndio hakuna jinsi.......hapa hatujali uroma wala nini, cha msingi Nchi inyooke.
 
Kama ndo aliyoyafanya huko bandarini ndo hayo basi jk's reputation is hanging on a thread,
 
...nafarijika kuona kwene baraza la JPM hayumo prince wa msoga....maana wamesaza...watuache...
 
Tanzania Hatujajua Haki Zetu,wala Hatujui Kwa Nini Tunawachagua Viongozi Wanaotuibia Na Wanaoshirikiana Na Wezi Kila Wakati.Uongozi Sio Kipawa Bali Ni Tabia.Katika Marais Wote Waliopita Hatujawahi Kumpata Rais Mwenye Tabia Za Uongozi Wote Ni Wasanii Wanaotuhadaa Kwa Ujanja Wao Na Wakati Wote Wako Kwa Masilahi Yao Binafsi Na Vyama Vyao.Kiongozi Haongozi Kwa Mihemko Kufanya Maamuzi.Bali Kiongozi Anapaswa Kuweka Maslahi Ya Watu Wake Mbele Kwanza.Magufuli Alipaswa Kutumia Taratibu Za Kisheria Na Kuwashughulikia Wasimamizi Wa Idara Sio Watenda Kazi Rais Kushika Mfagio Kufagia Uchafu Ni Usanii.Mamlaka Zinazosimamia Usafi Zinazoacha Huo Uchafu Zinakazi Gani.Ukiona Baba Mwenye Watoto Na Mke Nyumbani Anadeki Au Kusafisha Choo Nyumbani Kwake Huku Akijua Nyumba Hiyo Kuna Housegirls Anaowalipa Kwa Kazi Hiyo Ujue Ana Matatizo Makubwa.Na Hajielewi Wala Hajui Mamlaka Aliyonayo Na Hana Sifa Ya Uongozi Katika Nyumba Hiyo Bali Ni Mtumwa Katika Nyumba Hiyo.
 
Alafu hao vijana si tunawafahamu...!!! Inakuaje kila mmoja alie nao wao tuu..Vyombo vya usalama hapo ndipo pa kushtuka waangalieni vizuri pengine ndio waingizaji wakubwa wa PODA maana wao wanaenda kwa mwendo wa TIP tuu kuanzia mpiga deki mpaka kwa afisa mkuu..wanapita tuuu!!!
 
Taratibu naanza kuona kwa nini Kikwete aliizuia katiba ya wananchi isipite.
 
Kwa hali yoyote JK asingeacha hili jambo lipite hivi hivi kama asingekuwa na maslahi binafsi au maslahi mapana ya chama chake. Ikumbukwe kuwa chanzo cha ufisadi mkubwa hapa nchini ni rushwa katika siasa (political corruption) hasa wakati wa uchaguzi. Chama tawala kinategemea wafanyabiashara wakichangie; lakini hii ina gharama zake. Kuna ule usemi: "I scratch your back and you scratch mine" ikiwa na maana ukimwomba mfanyabiashara akuchangie kwenye mambo ya kisiasa hakika naye atakuomba umsaidie kwenye biashara zake ukishinda na kuwa madarakani. This is how the damaging mutual relationship between CCM the business elite works and there is nothimg Magufuli can do about it.
 
Nikukumbushe tu "Magufuli alichaguliwa kuwa mgombea wa CCM kwa bahati mbaya"

Haikuwa kwenye Calculations zao kabisa kumleta Magufuli na alikua "mtu mdogo mno", CCM walikua wanamuandaa Soft Boi Membe

Kwa taarifa yako...
CCM haijawahi kwenda Dodoma bila kumjua mgombea Urais wao.
 
Nasubiri kuona au kusikia hili gazeti la Raia Mwena likitakiwa kutoa maelezo juu ya ukweli wa habari hii, endapo hiyo haitatokea siku saba kutoka sasa basi kutakuwa kuna haja ya kuzaliwa nabii mwingine maana ule unabii alioacha Mwalimu Nyerere wa Ikulu kuwa 'pango la wanyang'anyi' utakuwa umetimia pasi kuwa na shaka yoyote.
 
Pamoja na mazuri yake mengi tu, lakini kwa ukwepaji wa kodi bandarini, Mzee wa Pwani should be ashamed of himself!
 
Back
Top Bottom