Huwa napinga sana hizi propaganda za kijinga na hii inadhihirisha kuwa sisi Watanzania wengi wetu elimu bado sana.
Moja, hakuna hopsital inayokataza usishuhudie mwili wa mpendwa wako ukioshwa ama kuuvesha nguo. Ila kuna vizuizi kutokana na watu kushikwa na hisia kali pindi wakimuona marehemu wao.
Pili, sehemu za kuoshea maiti huwa kuna bomba la kutolea uchafu moja kwa moja.
Tatu, hakuna ndugu anakatazwa kusimamia zoezi lolote kuhusu mwili wa mpendwa wao. Nina mdogo wangu mmoja alifariki miaka ya nyuma. Tuliitwa kwa ajili ya zoezi la usafishaji mwili, tukatoa mwili kwenye jokofu hadi pale unapopaswa kulazwa kwa ajili ya usafi. Hata ule uchafu tulioukuta kwenye lile beseni la kwenye jokofu tuliimwaga wenyewe palepale hospital. Zoezi la kusafisha mwili tulilikataa sababu alikuwa wa kike na kingine wenzangu walishikwa na hisia kali palepale so wote tukaiachia Hospitali.
Ninachoweza kusema ni hiki, ile harufu ya pale Mortuary ilikaa ndani mwangu kwa miezi isiyopungua 6. Ikifika wakati nikipita sehemu yenye harufu mbaya ikawa ni kama na mimi inanirudia harufu ya pale Mortuary. Zoezi la mule ndani tuwaachie wahusika.
Mwisho, kama madai yako yangekuwa sahihi kuwa uchafu huo ni pesa nzuri, basi hao watu wa Mortuary tungewaona na maisha mazuri sana, zamani watu walikuwa wanafanya tu hii kazi ila kwa sasa kazi ya Mortuary inafundishwa kabisa mavyuoni na hao ndio wanaoajiriwa. So tusifanye hitimisho ZITO katika mambo ambayo tunaweza tukatumia akili pia kuyaelewa.