kwa upande wangu mm inategemea na aina ya siri, mfano unakuta kwenu kuna matatizo fulani, si vizuri kumwambia mwenza wako ,maana anaweza kukushusha thamani kutokana na ndugu zako( mf labda kaka yako ni mdokozi) bahati mbaya mkazaa mtoto mdokozi, mwanaume ataanza kukutukana na kusema mtoto karithi kwa wajomba zake. lakini ukiweka siri mnakuwa mnashirikiana kutatua tatizo .AU uns historia mbaya ya kuwa na wanaume /wanawake wengi kabla hujakutana naye, hapo kwa kweli si vizuri kumhadithia mwenza wako maana utamfanya asiwe na imani na wewe tena , na inaweza kumpelekea hata mkaachana, akija kujua unamwambia yalikuwa mambo ya ujana na sasa nimebadilika na nakuheshimi mke/mume wangu.
SIRI YA PESA kwa kweli hili linatokana na jinsi mnavyoishi hapo home, kwa upande wangu mimi huwa sisemi kipato chote nipatacho kwa sababu unaweza kuta ndugu yangu ana shida, huwa sipendi kwenda kumuomba mume wangu huwa matatizo ya upande wangu hasa ndugu zangu natatua mwenyewe, nahisi kama kashfa akijua kuwa dada yangu ananiomba pesa, au home kunatakiwa pesa za matumizi, hiyo huwa nacover mwenye kimya kimya, kiasi heshima ya home inabaki pale pale.