(Kumbuka: kuna aina nyingi za tabia ya matumbo ya kawaida. Baadhi ya watu kwa kawaida huenda chooni kutoa kinyesi mara 2-3 kwa siku. Kwa wengine, mara 2-3 kwa wiki ni kawaida.
Zingatia milo 2-3 kwa siku na iwe milo ya uhakika au ni vyema kula vyakula sahihi au vya kuviandaa wewe mwenyewe
Kabla ya kula hakikisha unatanguliza matunda yenye hali ya nyuzi nyuzi(fible) na majimaji kama vile papai,embe,ndizi,chungwa,tikiti apple na mengine mengi.
Zingatia kunywa maji walau lita2-3 kwa siku kwa ajili ya kuongeza nguvu ya mwili na umeng’enyaji wa chakula.
Punguza kula vyakula vilivyokobolewa na hali ya nyama nyekundu kwa sababu ni ngumu kumeng’enyeka kwa wakati sahihi.
Fanya mazoezi ya aina yoyote walau dakika 5 kwa siku ili kutengeneza na kuimarisha mwili kwa ujumla.
MADHARA YA KUTOKUPATA CHOO KWA MUDA MREFU NI
Bawasili &
Vidonda vya tumbo
N:B
Magonjwa hayo ni hatari sana kwa mwanadamu ingawa yanatibika ila sio rahisi na ni gharama pia.