Sipandi tena gari ya magazeti

Sipandi tena gari ya magazeti

Nishawahi panda na nitapanda once again nitakapopata nafasi. I like gearing up untill you feel crazy!
High speed ina raha yake kama unauwakika na chombo chenyewe na uendeshaji wako haha.
 
Hivi vigari viangaliwe kwa hicho la pili mi kuna Siku nilitoka dar to Dom Massa manne tu tumefika gari nilikuwa inatembea mpaka nikawa naona tunatumia tyre za nyuma( dede) kutembelea na Barbara nilikuwa sioni nilipofika Dom ndo nikajua bado Niko duniani.
 
Nishawahi panda na nitapanda once again nitakapopata nafasi. I like gearing up untill you feel crazy!
High speed ina raha yake kama unauwakika na chombo chenyewe na uendeshaji wako haha.

Huwa unatumia vilevi?
 
Huwa wanawapa Magazeti bure so huwasimamishwagi... Kuna wakati nilipata emergency ya ghafla usiku na nilitakiwa niwe Arusha saa 2 asubuhi.. Nilikuwa na uchovu nikaona kudrive sitafika salama... Nikaenda kupanda haya Magari, asalaleee, kwanza karibia na Wami tulitaka kutekwa, alafu huo mwendo ni hatari, nilione isiwe kesi sana nilishuka pale Mombo nikatafuta sehemu ya kulala asubuhi niendelee na safarii..

Huo mwendo wanaoenda na ukijiuliza hii gari imeenda service lini na hiyo mirungi wanayotafuna hapo mbele ni mtu mwenye kichaa na asiyependa maisha yake ndiyo atakubali kumaliza safari..

HAhaha sasa si ulichelewa kufika A town?
 
Mimi sikupanda bure kama ambavyo wewe umezoea. Halafu hujui ni haraka gani nilikuwa nayo mpk nikapanda hyo fastjet ya ardhini

ndio ujifunzage sasa siku nyingine hiyo haraka yako itaishia uvunguni mwa fuso
 
wakati ulipata discounts tofauti kama ungepanda basi, ukakimbilia la magazeti kisa bei dezo, utadead weweeee

ule mwendo raha sana yaani feeling high,
ngoja niwawekee wanangu mazingira safi niendeleze safari zangu.
 
Watanzania wengine wanashangaza sana, hiyo imeshaitwa gari ya magazeti wewe unapanda umekuwa gazeti?halafu unakuja kulia hapa
 
Mkuu hongera yako kwa kushtuka. Kifo nje nje

Gari za magazeti, wewe uliingiaje? Wewe gazeti? Ungekufa kifo si chako. Siku nyingine upande lile la CCM lenye maji ya pilipili likiwa na taarifa kwamba CHADEMA wapo mahali wanafanya usafi!
 
Southern highland route zinamwagika mara kwa mara na vibaka kuambulia magazeti. Kwao vifo...
 
Nilikuwa na rafiki mmoja nae aliwahi kupanda huo usafiri basi zile Hadithi zake zilikuwa mwaka mzima
woga mwengine sio...
 
Pole Ndugu!

Hizi gari ni Janga, hivi karibuni nimepoteza ndugu mmoja na rafiki katika route ya Dar-Mbeya. so sad!

Madereva wanasema huwa wanafuta 180 speed oddo.

Kwa anayejipenda, haya magari siyo...

Wakuu habari zenu,

Najuta na nathubutu kusema kwamba sitokaa nipande tena magari ya magazeti kwani spidi zao ni za kuogopa na kidogo tu tungepata ajali pale Wami kama si kudra za mwenyezi mungu.

Tulitoka Arusha saa 8 mchana na tumefika Dar saa 2 usiku. Kama una moyo mwepesi usije ukapanda hata siku moja.
 
Of course barabara yao ndiyo hiyo.. Hivi vigari kwa mwendo wake ile barabara ya Morogoro kipande cha kuanzia Mlandizi mpaka Chalinze wangekuwa wanaua kila siku..
Kule barabara mbovu, foleni, 50 nyingi, maroli Mengi Na wajuaji wengi.
 
Kule barabara mbovu, foleni, 50 nyingi, maroli Mengi Na wajuaji wengi.

Mkuu huwa wanaondokaga saa 7 za usiku hilo la foleni sidhani kama ni sahihi labda wakati wa kurudi Dar.. Ubovu wa barabara ni sawa..
 
Back
Top Bottom