Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Geri Halliwell akihojiwa.....................
Hivi karibuni nilibahatika kusoma mahojiano ya Mwanamuziki wa kundi la zamani la muziki, maarufu kama Spice Girls la nchini Uingereza Geri Halliwell. Nilisoma mahojiano yake mtandaoni aliyoyafanya na Gazeti la Woman's Day la nchini humo.
Labda niwakumbushe wale wasiolifahamu kundi hili la Spice Girls.Kundi Hili liliwahi kuvuma sana miaka ya 90 nchini uingereza likijumuisha wanamuziki wanne, Victoria, aliyeolewa na Mchezaji maarufu wa soka nchini Uingereza David Beckgham, Emma, Melanie na Geri Halliwell.
Katika Mahojiano hayo, mojawapo ya maswali aliyoulizwa na mwandishi, ni hili la yeye kutoolewa pamoja na kwamba ana mtoto.
Akijibu swali hilo, Geri alisema kwamba hana imani kabisa na maisha ya ndoa, na ndoa kwake sio mojawapo ya agenda zake katika maisha. Alisema katika kizazi hiki familia nyingi zimeshuhudia kuvunjika kwingi kwa ndoa kama ilivyotokea kwa wazazi wake. "Katika makuzi yangu nimeshuhudia ndoa nyingi zikivunjika mpaka nimefikia kuona kwamba ndoa hazina maana kabisa" alisema Geri. ……… Aliendelea kusema kwamba haoni ndoa hata moja ya mfano ambayo anaweza kuitumia kama Dira yake inayoweza kumshawishi kuolewa, ingawa anapenda sana kuwa na watoto wengi.
Hebu wana JF fungukeni, Je anayosema huyu bibie yana ukweli?