Lowassa(CCM)+Lubuva(NEC) = Sioi(MP ARUMERU).
Kwa kombineisheni hii tujiandae kupokea habari mbaya ifikapo hiyo April.
Mtoto wa marehemu jeremiah solomon sumary amechukua fomu ya ugombea ubunge kwa tiketi ya ccm . Kuna uwezakano mkubwa akapitishwa kuwa mgombea wa ccm kupambana na upinzani .
Wakuu heshima kwenu, Nimesoma comments za wengi humu, nimegundua wengi wetu tunatoa comments kiushabiki zaidi ya hali halisi ilivyo. Wengi wetu tunadhani CDM wanachukua jimbo kirahisi safari hii na hii si kweli hata kidogo. kuna thread moja nilichangia kuhusu Jimbo hili mara baada ya kifo cha Mzee Sumari. nitarudia tena hapa.
Yeyote kati ya CDM na CCM anaweza ibuka mshindi ktk jimbo hili kwa sababu zifuatazo: Wakazi wa jimbo hili wamegawanyika katika makundi mawili yaani Wenyeji na wahamiaji. kundi la wenyeji kama wengi tukikumbuka huko nyuma lina misuguano ya muda mrefu kwenye koo zao (rejea ugomvi wa KKKT 1989/1990), na kwa kawaida ya hawa ndugu zetu ni wagumu kusamehe haraka. kwa hiyo mshindi wa ubunge inategemea sana anaungwa mkono na koo zipi.
Kundi la pili ni la wahamiaji na kwa kawaida wengi wao (80%) wataunga mkono CDM na hawa utawapata sana maeneo ya pembezoni mwa barabara kuu. Technically CDM wakicheza vizuri kete zao wanaweza shinda kwa sababu ukoo wa Nassari (iwapo CDM watamteua) ni moja ya koo zisizofungamana na upande wowote kama ilivyokuwa kwa Sumari. Lakini pia kama CCM nao watazingatia uzaifu wa koo hizi wakaja na jina kutoka kwa wasiofungamana na upande wowote then kazi ipo na ni pevu.
Kumbuka Mzee Sumari hakutaka kugombea 2010 kwa sababu za kiafya lakini wazee wa pale walilazimisha na hata kampeni hakushiriki kwa kiwango kikubwa. CDM wanatakiwa kusahihisha makosa yaliyofanyika 2010, CDM mkoa walijikita sana Mjini na nguvu kidogo walizipeleka kwa Nassari, na hata kuna maeneo mengine nadhani ilishindikana kuweka mawakala, na hapo ndipo CCM ilipiga bao ingawa hata kwa kutokuchakuchua bado nina imani CCM wangeshinda kwa kura chache.
Wapiga kura wa Arumeru mashariki (wenyeji) wengi wao ni wazee hasa kina mama, na kama CCM wataleta jina neutral CDM msitarajie kupigiwa kura na kundi hili. ni wagumu sana kubadilika na kuelimika haraka. Ni matumaini yangu kwamba CCM watakuja na the Kaayas, the Palangyos, the Ayos and the likes, na hapo for sure CDM watapiga bao kama kumsukuma mlevi.
Heasabu yako mkuu imenikumbusha mbali sana naona uliwahi kupiga hesabu za intergration vile?maana hiyo formation ni more than danger je hali itakuwaje?nadhani damu itamwagika,maana hiyo kombinesheni ni ushindi wa kulazimisha full charge-Tautology.
Hapo kuna haja ya kujipanga zaidi ya vita.na ndio maana nimeshapost humu nimesema CCM wote wanamilikiwa na EL,anaebisha ajitokeze,hata Nape kama unabisha jitokeze useme humu jukwaani,maana atakaloliamua hakuna wa kubisha,leo hii kujivua gamba kumefutika tena,ni kwa ajili alichoka na jambo hilo,huko NEC ameshapanga safu na sasa anataka kupanga huko Arumeru,hakika CDM tunaahidi kupambana
Nasari kwa upande wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo yupo on line kwa mapambano tena na huu uongozi wa kuridhishana nafsi yangu inaikataa sana na cjui hw mafisadi wanafikiri bado tupo kwenye karne ya 10 Mi cjui.
Na nafikiri hili litakuwa fundisho kwa hawa mafisadi wachumia matumbo yao!
Yeye kwani nao umaarufu na uzoefu gani katika siasa? na je hicho kiti ni kiamba useme lazima mtoto arithishwe kama kiti cha umangi kule kwa akina Mareale Marangu? Ina maana ni Kampuni ya akina sumari inarithishwa kwa mtoto baada ya kifo cha CEO siyo?
Mdogo wangu Nasari wa CDM kaza buti tuko pamoja ktk hii vita nyepesi iliyoko mbele yetu ya kutwaa Jimbo la Arumeru kwani sasa hivi ni zamu yako kupokea kijiti kaa mkao wa kupokea .
Yeye kwani nao umaarufu na uzoefu gani katika siasa? na je hicho kiti ni kiamba useme lazima mtoto arithishwe kama kiti cha umangi kule kwa akina Mareale Marangu? Ina maana ni Kampuni ya akina sumari inarithishwa kwa mtoto baada ya kifo cha CEO siyo?
Mdogo wangu Nasari wa CDM kaza buti tuko pamoja ktk hii vita nyepesi iliyoko mbele yetu ya kutwaa Jimbo la Arumeru kwani sasa hivi ni zamu yako kupokea kijiti kaa mkao wa kupokea .
Ukiondoa kuponzwa na mkewe, he is a man of integrity!.Jamani kama hali ndo hii, mbona sijamsikia mkuu wa kaya mstaafu akimleta mwanae kwenye siasa? au yeye hakuwa na watoto???
Chunga sana ndogo wangu Wameru hawakawii kunyanyua mapanga, hata hivyo tunawatakia mafanikio!!!! CHADEMA HURAAAA!!!
Kuna wakati najiuliza hivi kama huyu SIOI kama angeamua kugombea kwa kupitia CDM, mtizamo wa watu si ungebadilika sana? Tunachotaka sisi akipitishwa asimame yeye kama yeye na si kutumia kivuli cha baba yake kama ilivyokuwa kwa V. Nyerere
pata chimbika kule n nyumban
Jana nilikuwa usa river,wapiga kura wengi waliosikia kuwa mtoto wa marehemu mbunge Sumari, Sioi Sumari na mtoto wa mkuu wa zamani wa jeshi meja Sarakikya,willy sarakikya ni dalili za kuwadharau watu wengine wa jamii hiyo.wamesema ubunge wa meru si ufalme wa kurithishana kwa familia zilizoshiba wakati wowote.