Sintofahamu ya idadi ya wadhamini urais

Sintofahamu ya idadi ya wadhamini urais

Kitendo Cha Wanachama wa CCM kujitokeza kwa wingi kumdhamini Lowasa imetusaidia sisi Watanzania kujua kumbe CCM ni chama kinachounga mkono vitendo vya UFISADI. Somo zuri sana
Shetani ana watu wengi kuliko Lowasa
 
suzan lema

Kama Mkoa wa Mbeya kuna Wana CCM 200,000 na 50,000 wamekubali kumdhamini Lowasa je 150,000 wapo wapi???
 
Last edited by a moderator:
Mchakato wa kupata wadhamini ndio CCM itatumia kama kigezo cha kumpa mgombea(Aliyepata mafuriko zaidi mikoani), anayesubiri vigezo vingine (13?) atasubiri sana. Huwezi kuzuia mafuriko kwa mkono.
Kamati Kuu- CC tayari waliotegemewa kuwa "challenging" Wameshachukua fomu za kujiondoa CC (Eti watangaza nia) ili wasiwe na uongozi na EL, hivyo mpango umeshakaa kama ilivyo tarajiwa, EL mwenyewe keshasema ameshamaliza kazi, kuna watu wachache bado hawajamwelewa.
 
Udhamini ni kwa mgombea mmoja tu. Hao 50,000 ni kuhakikisha wengine wanakosa wa kuwadhamini.....

Kama mgombea mmoja ana wadhamini 50,000 na mkoa una CCM kama 200,000 sasa hao wagombea wengine si watakosa wadhamini?
 
Acheni upuuzi, minimun 450 ktk mikoa isiypoungua 15, each mkoa upate minimum 30, kati ya hiyo mikoa 3 iwe ya Zanzibar...!!

Yaani wadhamini wasipungue 450...in other words kuanzia 450 hadi ukiweza DUNIA NZIMA KAMA INAPIGA KURA wakupe udhamini, even to the entire Universe...!!! Hadi tani ya tani yakooo...!!!

Hivi mnadhania kupata wadhamini ni shughuli ndogo eeeehh...!? Nenda ww hata mmoja ukimpata, ukiacha kura yako utaja niambia..!!!

Wadhamini ndio KIGEZO KIKUUUUUUU CHA KUKUBALIKA KWAKOOOOOOOOO.... hamwelewiiiiiiiiiiiiiiii..... aaaaarrrgghh...capucino..!!!
 
Sasa kama hawajirudii mbona kuna watu kila mtangaza nia akipita mkoani kwao ni lazima utawaona tu wapo mstari wa mbele...???

Si kila anayekuwa mstari wa mbele anakuja kudhamini....... Wengine kusikializa tu jamaa anasema nini... Kinachokatazwa ni kudhamini mara mbili na si kufika alipo msaka udhamini..
 
Kama mgombea mmoja ana wadhamini 50,000 na mkoa una CCM kama 200,000 sasa hao wagombea wengine si watakosa wadhamini?
Sawa kabisa, na hiyo ndo nia halisi.. Wapige kelele jamaa atawakosesha wadhamini
 
kwani kuna kosa gani wakilipwa? umemuweka mtu saa tano anakusubiri, je ni kosa kumlipa muda wake alioupoteza kukusubiri?

acheni mawazo ya kifukara.
Acha kupotosha Makatibu wa Mkoa wanatafuta wadhamini kwa kadi zao na kuzirudisha haina haja hata ya kuonana na unayemdhamini hiyo ni Rushwa tu. Akina Bilali hawajetembea hata hiyo mikoa yote zaidi ya kutafutiwa wadhamini na kurudisha fomu hao wanaozunguka kila Mkoa na wilaya wanatafuta kuhonga tu na kampeni hawana lingine
 
Nashangaa sana, kuna haja ya wale wote ambao wanatuhumiwa na ufisadi wasiwe wanaruhusiwa kuingia kwenye kinyang'anyiro
 
wagombea wote 30+ hawaendi mkoa mmoja.

Hakuna utata kwa ukweli kwamba ukimdhamini mgombea mmoja huwezi kumdhamini mwingine, Ila bado kuna shida kwenye idadi ya wanachama wanaotakiwa kumdhamini mgombea katika mikoa hiyo 15,

Je? 450 members ni kwa mikoa yote 15 kwamaana ya 30 kwa kila mkoa? wengi tunadhania hivyo maana hata CCM wenyewe kwenye masharti yao hawakufafanua vizuri. AU hiyo 450 ndio kwa kila mkoa kwa maana ya 450 x 15?

Hebu wajuaji watujuze, pls.
 
Chama cha Mapinduzi kilifungua dirisha lake la watia nia kwa ngazi ya urais. Wanachama wengi wamejitokeza hadi sasa wanakaribia kufikia 40. Miongoni mwao wameshakamilisha zoezi la kutafuta wadhamini wasiopungua 450 kwa mikoa isiyopungua 15 ya Tanzania. Katika mchakato huo, baadhi wametumia fursa hiyo kujiuza toka mkoa mmoja hadi mwingine huku wapambe wao wakisherehesha mikutano ya kusaka saini za wadhamini kwa mikutano mikubwa sana. Na baadhi yao wamefanya na kukamilisha mchakato huo kimya kimya.

Aidha, kwa watia nia wengine miongoni mwa waliojitokeza inaonesha kuwa fursa hii ya kusaka wadhamini waliisubiri kwa kwa shauku kubwa. Ni fursa ambayo ilikusudiwa kujiuza kwa taifa kwa maana kabla ya hapo hawakuwa na wala wasingeipata fursa kama hii. Hii ni fursa adimu ya kuzunguka nchi nzima ukisema makusudio yako ni nini kwa umma. Fursa adimu iliyotumika kuvuka mipaka ya zoezi hata kufikia kuitangulia NEC ya Jaji mstaafu Lubuva.

Inavyoelekea, kuna watia nia hao waliokuwa wamepanga kimkakati kabisa kutumia mchakato huo kuanza kampeni za kuusaka urais mapema. Na kwa mujibu wa Katibu Mwenezi wa CCM ndugu Nape Nnauye mchakato wa kutia nia na kusaka wadhamini sio muda wa kampeni. Hata hivyo, kwa sisi tulio wengi mchakato huu kwa baadhi ya watia nia umegeuzwa muda na msimu wa kampeni kiaina. Kampeni ambazo si kwa wanachama tu, bali sasa ni kwa taifa zima.

Tunapenda kuelewa, kwa mujibu wa kanuni za CCM. Je! Ni sahihi kwa mwenendo kuwa hivi?
 
Chama cha Mapinduzi kilifungua dirisha lake la watia nia kwa ngazi ya urais. Wanachama wengi wamejitokeza hadi sasa wanakaribia kufikia 40. Miongoni mwao wameshakamilisha zoezi la kutafuta wadhamini wasiopungua 450 kwa mikoa isiyopungua 15 ya Tanzania. Katika mchakato huo, baadhi wametumia fursa hiyo kujiuza toka mkoa mmoja hadi mwingine huku wapambe wao wakisherehesha mikutano ya kusaka saini za wadhamini kwa mikutano mikubwa sana. Na baadhi yao wamefanya na kukamilisha mchakato huo kimya kimya.

Aidha, kwa watia nia wengine miongoni mwa waliojitokeza inaonesha kuwa fursa hii ya kusaka wadhamini waliisubiri kwa kwa shauku kubwa. Ni fursa ambayo ilikusudiwa kujiuza kwa taifa kwa maana kabla ya hapo hawakuwa na wala wasingeipata fursa kama hii. Hii ni fursa adimu ya kuzunguka nchi nzima ukisema makusudio yako ni nini kwa umma. Fursa adimu iliyotumika kuvuka mipaka ya zoezi hata kufikia kuitangulia NEC ya Jaji mstaafu Lubuva.

Inavyoelekea, kuna watia nia hao waliokuwa wamepanga kimkakati kabisa kutumia mchakato huo kuanza kampeni za kuusaka urais mapema. Na kwa mujibu wa Katibu Mwenezi wa CCM ndugu Nape Nnauye mchakato wa kutia nia na kusaka wadhamini sio muda wa kampeni. Hata hivyo, kwa sisi tulio wengi mchakato huu kwa baadhi ya watia nia umegeuzwa muda na msimu wa kampeni kiaina. Kampeni ambazo si kwa wanachama tu, bali sasa ni kwa taifa zima.

Tunapenda kuelewa, kwa mujibu wa kanuni za CCM. Je! Ni sahihi kwa mwenendo kuwa hivi?

Tumeanza kampeni
 
Hivi hao wanaotia nia kwanin wapoteze pesa zao kwa kitu wanajua hawapati?...
 
Back
Top Bottom