Sintofahamu ya idadi ya wadhamini urais

Sintofahamu ya idadi ya wadhamini urais

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2008
Posts
10,942
Reaction score
437
Harakati za wagombea urais kutafuta wadhamini zinazidi kushika kasi na kuchukua sura mpya ya kuvuna idadi kubwa ya wanachama.

Wapo wagombea wanavuna zaidi ya wadhamini makumi maelfu hadi wengineo kufikia wadhamini zaidi ya elfu hamsini.

Watu wanahoji juu ya hiyo idadi kubwa ya wanachama lakini wanasahau ya kuwa CCM ina zaidi ya wanachama milioni sita (6,000,000) ambayo ni wastani ya wanachama laki mbili (200,000) kwa kila mkoani.

Hiyo ni takwimu ya mwaka jana, mwaka huu kuna kundi kubwa la vijana ambao wametimiza vigezo vya kupewa kadi za uanachama wa CCM.

Endapo tu kila mkoa una wastani ya wanachama laki mbili, leo hii utashangaa vipi katika mkoa mmoja mgombea akipata wadhamini elfu hamsini?

Mathalani katika mkoa wa Mbeya nikisikia kuna mgombea kavuna zaidi ya wadhamini 50,000 sintashangaa.

Mkoa wa Mbeya una wilaya tisa na kila wilaya una wastani wa wanachama wasiopungua 10,000.

Mathalani wilaya ya Mbeya mjini pekee ina wanachama wasiopungua 30,000 hapo bado haujaweka idadi ya wanachama katika wilaya zingine 8 za mkoa wa Mbeya. Leo hii utashangaaje kupatikana kwa wadhamini 50,000 kwa mkoa mzima?
 
Asante kwa kuwaelewesha hawa hayawani wasiojua kupima mambo..

50,000 elfu hata nusu hawajafikia idadi ya wadhamini katika mkoa husika.


Watakuja kwa kasi hapa kukupinga...
 
Nimegundua kuwa LOWASSA amawaumiza sana kichwa kwa hiyo wanachokifanya ni kutaka kuaminisha watu ujinga usio na maana

Ni bora umewaelimisha na wajue hayo, waache porojo
 
Ni kweli kwamba wanachama hao wamelipwa?
 
Nimetokea kukupenda suzan lema. Hivi CCM ina wanachama hai wangapi?
 
Last edited by a moderator:
Kitendo Cha Wanachama wa CCM kujitokeza kwa wingi kumdhamini Lowasa imetusaidia sisi Watanzania kujua kumbe CCM ni chama kinachounga mkono vitendo vya UFISADI. Somo zuri sana
 
Kwahiyo hao 50,000 wanamdhamini mmoja wanaruhusiwa kuendelea kudhamini wengine?...
 
LOWASSA ndio chaguo La watanzania jamani

Acha watu waumwe na roho hasa wapinzani wake ana wapiga tu kwa vitendo
 
Nadhani kuna uwezekano wa kuwadhamini watia nia wote 40. Kwa kuwa kudhamini si kama kupiga kura, ili mradi tu nawe umenufaika kama utaratibu wa nipe nikupe ulivyo.
 
Watu washarudisha fomu nyie endeleeni na kampeni ya kununua wadhamini
 
Hivi mdhamini mmoja anaweza kujirudia kudhamini watangaza nia wengine...??
 
Na bado nadhani hio fungakazi ya darsam mtazimia kabsa maana wadhamini tutakua zaidi ya mikoa yoteee , huyo lowassa anawatesa sanaa jamani maana kama kachukua fom pekee yake kila mtu lowassa, hata hao wagombea wengine Hija udkubwa ni lowassa
 
wagombea wote 30+ hawaendi mkoa mmoja.

Mleta mada kami hesabu ya kueleweka.... Assume una wagombea watano wameenda mkoa mmoja wenye average ya wanachama 200,000 na wanne kati ya hao watano kila mmoja kapata hao 50,000, huyo wa tano si keshakosa wadhamini hapo?
 
Wadhamini wanahitajika ni 450 kila mkoa kwa idadi ya mikoa iliyotajwa.

sasa hao 50,000 ni uhuni wa kutaka kulazimisha kwamba bwana EL ndo anapendwa sana.

anachojaribu kufanya ni kulazimisha chama kimuone kuwa ni mtu na chaguo la wanachama.

Anachokifanya ni kukiuka utaratibu na hili ndo limemuondolea sifa kwani amegeuza nia na kuanza kutembea na kampeni.

Subirini tayari wanamvutia pumzi.
 
CCM kila kukicha inapokea wanachama wapya pole yao wanaokosa udhamini,, mwenzao anakubalika anapata wengi wanaanzaa kusema maneno yao ya hovyo ..

EL mbele kwa mbele
 
Asante kwa kuwaelewesha hawa hayawani wasiojua kupima mambo..

50,000 elfu hata nusu hawajafikia idadi ya wadhamini katika mkoa husika.


Watakuja kwa kasi hapa kukupinga...

Sina uhakika iwapo mtu mmoja anaruhusiwa kudhamini mgombea zaidi ya mmoja. Je, katika idadi ya wastani ya wanachama 200,000 kila mkoa, wagombea 38 kila mmoja atadhaminiwa na wanachama wasiozidi 5,265 tu. Endapo mgombea mmoja atakomba wanachama 50,000 ina maana kuna baadhi ya wagombea wanaweza wakakosa wadhamini! Ninaambiwa Chama chao kina hitaji kila mgombea adhaminiwe na wanachama 30. Je kutotimiza idadi hii au kuzidisha idadi hii sio kukiuka utaratibu? Je wanaokiuka utaratibu huu wanapunguza mojawapo ya sifa za kuteuliwa?
 
Back
Top Bottom