KILA BAO LA MKONO LA CCM KUIBA KURA TUTALIBAINI NA KULIWEKA HADHARANI 👇
Tulishaweka wazi hapa kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeingia mkataba wa siri na mtandao wa simu wa Tigo kutumia mtandao wa Tigo kutuma matokeo ya kura toka kwenye vituo vya kuhesabia kura baada ya upigaji kura kukamilika tarehe 25/10/2015. Vile vile tulisema kampuni hii ya Tigo kada wa CCM Yusuf Manji na Raila Odinga wa Kenya (rafiki wa Magufuli) wana maslahi/hisa ndani yake. Aidha tukasema Manji ana
mkono katika uagizaji wa mashine mbovu za BVR na wataalam wake walizichezea.
Sasa sikia hii kali: Wataalam wa IT wa CCM na Tigo wako kazini hivi sasa wanachezea mfumo wa masafa wa Tigo wa Base Station Control (BSC) ili kwa siku 3 kuanzia tarehe 25 mfumo huo uweze kuzuia mawasiliano ya simu na data kwa wakati fulani fulani na maeneo fulani fulani ya nchi kwa kadri CCM itakavyoona inafaa kulingana na hali ya matokeo ya CCM na ya Ukawa, kubwa ni kuzuia au kuchelewesha matokeo ya Ukawa kufika haraka Center toka maeneo Umoja huo wanapata matokeo mazuri. Hii ni kuwezesha Tume kujumuisha kura zilizochakachuliwa na mfumo mbovu wa Tume wa kutuma na kujumuisha kura, na kisha kutangaza haraka matokeo feki ya Urais kumpa Magufuli ushindi kabla Ukawa hawajajumuisha kura zao zote.
Kumbuka Tume ikishatangaza matokeo ya Urais ndio imetoka.
UKAWA TUWE MACHO!!
Sambaza kwenye groups zingine 👆