Single mpya ya CHADEMA hii hapa


Ukisoma haya ndiyo utaona hali halisi ya mtanzania na hasa kichwani kwake. Huyo anayetuandikia hivyo jana usiku hakula kwa maana kwamba hakuwa hata na hela ya kula kalala na njaa. Wazazi wake huko kijijini pia hawajala hata hela ya kununulia mafuta ya taa (ya kibatali) hawana. Amelala kwa kamshumaa ambako kameshaisha hata leo hana cha kuwasha maana nchi iko gizani. Hakuweza hata kuangalia ka-tamthilia kupitia luninga kwa jirani maana nchi iko gizani. Leo asubuhi amefika kijiweni kwake hawezi kufanya kazi bila umeme matokeo yake amekaa ameduwaa na hajui mchana huu atakula nini. Mkombozi wake mafuta ya taa angalao ya kuwashia jiko la mchina sasa hayatanunulika kwa sababu yameongezwa bei kama mafuta ya gari ili kuwakomoa mafisadi wachakachuaji wa dizeli na petrol. Hapo alipo anawaza bei ya maharage, sukari, dagaa, sembe, nakadhalika nakadhalika bila kusahabu kodi ya mwenye chumba, madeni mpaka utosini, ka ada ka kijana na kale kahela ka kamtihani, nakadhalika nakadhalika. Na kamshahara kenyewe anakachukua leo kaishaisha hata kabla ya kufika nyumbani. Yote yaho na mengine anaona badala ya kujitundika aandike hiyo ngonjera hapo juu aimbe na kucheza ili kujisahaulisha na mawazo. Watanzania tumefikishwa mahali patamu kweli kila mtu abebe sehemu yake.
 

Single imepigwa , Magwanda yote yanacheza haya tuendeleee kucheza mzee...................
 

Tunashukuru kwa kutujulisha hayo kwa upande wako, mie sasa kwangu ni kinyume cha hayo. Njoo na ww nikuajiri uache kupata hayo mateso. Fanya kazi acheni kupenda vitu vya bure bure kama sera ya Magwanda
 
ukitaka kujua thamani ya magwanda na kijani we vaa kijani na suruali nyeusi na mwingine avae magwanda wote mtembee mtaani uatona jinsi utakavyo zomewa na raia kukushangaa kweli kweli mpaka utatamani kuvua

Magwanda na hili joto la Dar es salaam si ndio mnaungua ndani kwa ndani, mbona mnajitesa wenyewe !
 
Singo yako imekaa kikuda kama sharo anayepakatwa

Duh, kweli ww ni balaa, kumbe unapakatwa , ndio mchezo wako kumbe ? haya njoo basi tukupe shughuli sie marijali
 

Inauma eeee, imeingia vizuri eeeee, pole pole vumiliaaaaaaa mtoto
 
rangi yake si nyekundu, kwani yafanana na nyasi,
wengi hupenda kuyavaa, yakiwa na kofia zake,
magwanda hayana mvuto, watu wameyakosesha
 
"Mungu katika Jina la Yesu akusamehe Maovu yako yote, na Kukuponya Magonjwa yako yote
(Zaburi 103:3)"


 
salaam ziwarudie watuwa magamba, magamba makubwa kuliko ya mamba, mloshindwa kuvuana magamba, sasa mwawachokoza magwanda, magamba nyie magamba, lazima tuwanyofoemagamba. wanaupeo wa kufikiri magwanda kuliko nyiemagamba, hoja zao zatugusa wananchi masikini, magwanda watetez wetu,tunyonywao na nyie magamba. na kwa uzalendo walionao, twaawapongeza sana magwanda magamba nyie magamba, lazima tuwanyofoemagamba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…