Wanaharakati wa Tanzani, Wanasheria, Wanasiasa. Kesho ni siku rasmi ya kuanza kudanganywa wananchi wa vijiji vya Kisaki, Ughaugha A, Ughaugha B, Unyamikumbi A, Unyamikumbi na Kisasida kuanza kuombwa watoe ardhi kwa kampuni inayoitwa WIND EAST AFRICA inayotarajia kuhamisha vijiji sita.
Kampuni hiyo ikiwa bado haina eneo Singida, imebebwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida mpaka akatoa matusi kwa wananchi, Serikali yetu kupitia TIC ilitoa Certificate of Insentive kabla kampuni haijapewa eneo, Ewura walitoa leseni ya kuikubalia kampuni hiyo kuanza uzalishaji, na Tanesco walianza Power Purchasing Agreement bila kampuni kuwa na eneo. Ramani ilichorwa na kampuni hiyo licha ya Mkurugenzi wa Manispaa kusema kuwa haina eneo kauli inayopingana na Mkuu wa Mkoa huo.
Pamoja na juhudi za Vilio hivyo hakuna Mwanaharakati aliyeingilia kuwasaidia wanavijiji hawa, wala Mwanasiasa aliyewasaidia hawa wasiojua hata sheria zilizokiukwa
Kampuni hiyo ikiwa bado haina eneo Singida, imebebwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida mpaka akatoa matusi kwa wananchi, Serikali yetu kupitia TIC ilitoa Certificate of Insentive kabla kampuni haijapewa eneo, Ewura walitoa leseni ya kuikubalia kampuni hiyo kuanza uzalishaji, na Tanesco walianza Power Purchasing Agreement bila kampuni kuwa na eneo. Ramani ilichorwa na kampuni hiyo licha ya Mkurugenzi wa Manispaa kusema kuwa haina eneo kauli inayopingana na Mkuu wa Mkoa huo.
Pamoja na juhudi za Vilio hivyo hakuna Mwanaharakati aliyeingilia kuwasaidia wanavijiji hawa, wala Mwanasiasa aliyewasaidia hawa wasiojua hata sheria zilizokiukwa