Ndugu
Talkandtalk , nafurahi leo unazungumza kiungwana. Baadhi ya majibu kwa maswali yako:
1. Unasema mgogoro wa kisiasa ulimalizwa kisheria baada ya mahakama mbili kuamua kuwa Nkurunziza anaruhusiwa kuongoza:
Kwa hili you are very WRONG,japo kweli mahakama iliamua hivyo lakini what about the coup attempt?? unaongeleaje mgawanyiko jeshini baada ya failed coup serikali ilianza kuwinda wale wote waliokuwa wanasapoti coup d`etat.
JIBU: Hapa ni wewe ndie unayekosea, mgogoro ulikuwa tafsiri sahihi ya mkataba wa Arusha kisheria. Sasa kama mahakama zimeamua kuwa hakuna tatizo, hao wenye matatizo na Nkurunzinza msingi wa hoja zao ni nini? Maana kama kungekuwa na any ruling inayokubaliana na tafsiri yao halafu Nkurunzinza akakataa hapo sawa, otherwise ni magaidi tu.
Kama wangekuwa wanapinga uchaguzi uliompa Nkurunzinza madaraka, maybe wangeeleweka, but they chose to boycott the elections AFTER mahakama ya EAC allowed it! Kama wana msingi wowote ule please tuelezee sisi tusiojua.
Kuhusu the coup, naona wewe umegeuza maneno. Wanaowindwa sio walio support coup, actually wanaowindwa ni wale waliomrejesha Nkurunziza madarakani! Aliyepambana na Niyombere na kumrudisha Nkurunziza madarakani
Lt. Gen. Adolphe Nshimirimana amepigwa roketi na kuuawa, MKUU WA MAJESHI
Gen Prime Niyongabo naye kaponea chupu chupu kuuwawa last month katika tukio ambalo walinzi wake 7 waliuawa! What are you talking about kuhusu walio support coup kulengwa. Jeshi lote sasa hivi liko chini ya Nkurunziza, maafisa wote wanamtii Nkurunzinza. Niyombere na wenzie walisha surrender na wako chini ya Nkurunziza. Hao wanajeshi wanaompinga Nkurunzinza wanaolengwa ni kina nani? You should be asking who is behind these targeted assassinations against government officials ikiwa Niyombere is no longer in the picture.
Mfano wako kuhusu Zanzibar ni irrelevant. Maalim Seif hawezi kuchukua silaha na kuanza kuua maafisa polisi na jeshi wa serikali ya Zanzibar, hawezi kuchukua mabomu na kurusha hovyo mashuleni na masokoni ili kuleta vita vya kikabila. Na hata akiandamana, ataandamana kwa sababu za msingi na zinazoeleweka, hataandamana kwa kutumia slogans alizokuwa anatumia anatumia sultani aliyepinduliwa na karume zisizo na kichwa wala miguu!
2. Unasema Wapinzani walisusia uchaguzi kwasababu wanazozijua wao...hapa tayari unaonesha upande wako, wapinzani walikuwa hawakubaliani na kitendo cha Nkurunziza kutaka kuendelea kuongoza.
3.Mwenyewe unakubali kwamba Nkurunziza alipigiwa kura na wanachama wa chama chake tuu.. mpaka hapa unakubali kwamba issue sio kabila kwani kuna zaidi ya vyama kumi ambavyo viko active kati ya hivyo very few are owned by Tutsi, as such Wahutu wengi pia hawakumpigia Nkurunziza kura.
JIBU: Sababu zao zilishapingwa na mahakama, kwa hiyo tendo la kufanya uchaguzi lilikuwa halali. Vinginevyo toa sababu zingine tofauti na zile ambazo wapinzani walikuwa nazo zilizowafanya kususia uchaguzi. Na zaidi ya hapo tafadhali tupe hypothesis yako juu ya nani aliyekuwa anaua raia wasio na hatia kwa kutupa mabomu vituo vya kura, kwa kupiga risasi wapiga kura etc, ikiwa wapinzani walisusa uchaguzi.
Sindumuja movement... hii umeifanya title ya post yako, nimejaribu kuisearch kumbe ni twitter hashtag ambayo ina tweets 124 kati ya hizo mwenye account kapost more than 80 posts, hashtag yenye 80 followers na 4 likes!!!
Is this a big deal for a country?? hastag with last tweet done in May?? Cmon!
JIBU: Mimi nazungumzia sindumuja yenye link hii:
https://twitter.com/hashtag/sindumuja hiyo ya mwezi mei ni ya kwako mkuu.
Issue ya history ya Ufalme huwa unapenda kuileta sana, yes it happened lakini kumbuka this was everywhere in Africa,Tanzania inclusive: Ufalme ulikuwa hereditary na Familia za kifalme lived as dictators...issue ni current leaders.
Nyerere angekuwa na idelogies kama zako Tanzania ya sasa isingekuwepo kungekuwepo na
ukabila..angeanza kukumbusha wananchi jinsi walivyonyanyaswa na wafalme.
JIBU: Usemayo ni kweli kabisa. Naona umekubaliana na mimi kuwa hata Nyerere ?angeanza kukumbusha?? tungekuwa na matatizo. Sasa je kuna haja gani ya wapinzani ambao ni watutsi kuanzisha slogan ya #sindumuja fully knowing its implications kwa wahutu regardless of how ?positive? YOU tutsis define it? Huu sio uchokozi wa wazi wazi kukumbushia historia kama ulivyosema? Burundi was more advanced in tribal reconciliantion than Rwanda, look at what this #sindumuja is doing now. How would a Tutsi feel if a political party, majority composed of Hutus use #SinduInyenzi? Halafu wadai wanamlenga Kagame because he has extended his rule? Where is the relationship here?
Zingatia kuwa wahutu wa Burundi wamekandamizwa na watutsi toka uhuru, kila rais aliyechaguliwa toka uhuru aliuawa na jeshi la watutsi kuchukua madaraka kwa mtutu. Nkurunzinza ana uhalali unaothibitishwa na mahakama halafu watutsi wanatumia #sindumuja kutaka atoke bila sababu za kisheria?
Sasa nani atachukua madaraka kama watakuwa tayari wameuawa, kwa msemo wako nikama vile wanajitoa mhanga..
Hapo sikuelewi eti UTENGENEZAJI WA GENOCIDE DHIDI YAKO KWA KUKUSUDIA is it ???????
JIBU: Watutsi wa kawaida sio wanaojitoa mhanga, wao ndio wahanga, wanaowatoa mhanga ni the elite behind #sindumuja. Kama ambavyo when the dust settled ndio ikajulikana kumbe Interahamwe iliyokuwa inafanya genocide against the Tutsis, ilikuwa inaongozwa na MTUTSI afterall! Kwa hiyo sio ajabu kabisa kuwa when its all over ukagundua kumbe ?Imbonerakure? wanaofanya unyanyasaji wa watutsi kiongozi wake ni mtutsi! Right now ripoti zote zinadai wanaofanya mauaji wamevaa nguo za polisi. Lakini polisi wenyewe hawana rekodi zozote za hao watu, na hata mauaji yenyewe ni senseless. Why would a police officer atumwe na Nkurunzinza kwenda kurusha mabomu kwenye neighbourhood ambayo ni stronghold ya CNDD??? Huu ndio ule uongo wa Kagame enzi zile za kudai miili inayoelea mto Kagera ni watutsi waliouawa na interahamwe, mpaka pale watu wetu walipomtolea uvivu na kumkumbusha kuwa jeshi lake la RPA lilikuwa limeshikilia hayo maeneo for a whole year!
Ukweli ni kwamba mauaji yanayoendelea Burundi yanafanywa na pande zote it is tit for tat... in this case as long as Nkurunziza ndiye Rais wa nchi he is answerable.
Yeye hajitofautishi na waasi wa serikali yake, wakiua na yeye anaua, huo sio uongozi kashindwa.
JIBU: Yes majeshi ya Nkurunziza kill, lakini why do they kill? Hilo ndio swali. What reason do these sindumuja have for killing innoncent civilians? Why don?t they target the army only kama vikundi halali vya uasi vinavyofanya? Did ANC kill innoncent white people during the struggle? Here you have tutsi opposition thugs, killing hutu innocent civilians while shouting #sindumuja, what do you expect if not revenge killings? Do they have to burn buildings and destroy properties? Sasa hapo kuna kosa gani kwa polisi wa Nkurunzinza kutumia risasi kupambana na hawa watu?
Mwisho kabisa labda nikuulize wewe, given the situation, what would you have done if you were Nkurunzinza? Na kwa sababu ipi?