1. Rwanda's involvement in Burundi. The way you put it ni kuwalaumu Watutsi bila kuangalia vyema root course.
Kwa nini Watutsi wakimbilie Rwanda au coordinators kuwa watutsi? Mkimbizi hukimbilia ambapo atakuwa safe. Hata Tanzania bara pakitokea shida ni very simple Maasai kukimnilia Kenya na Mpemba Pemba. Hii ni kwa sababu upande utakaokimbilia unayohakika na usalama wa maisha yako.
Pili Rwanda kuweka vikosi mpakani ni hatua ambayo kwa mtazamo wangu ni sahihi since uwepo wa vita au FDRL Burundi kunastabilize amani ya Rwanda kwenyewe. Wala hili sio geni kidunia.
Pili la kutungua ndege, unakubali ilitunguliwa na askari halali wa serikali ila unahoji mbona hawakuwa na plan ya whatafter. Hili si sahihi, kwa mujibu wa statements ya baadhi ya waliokuwa Peacekeeping mission walikiri after ile bombing vikosi vya serikali vilianza kumove into action. Pia swala la kuwa RPF walikuja instantly kwa kuwa walijua tukio prior to its happening nadhani ni kuignore kuwa since 1990 RPF walikuwa stationed kijeshi na walikuwa wanafanya raids kwenye mpaka wa Rwanda na Uganda.
Suala la warrants za kumkata Kagame by French and Spain nadhani ni unafiki wa kisiasa. Madai ya Nyamwasa hayo nadhani yapo fully biased. Baada ya kuasi nchi ndio anatoa ushahidi, intentions zake ni malicious towards Kagame. Maake ukiangalia vizuri utagundua hata yeye mwenyewe hujifanya hajahusika na RPF bali ni Kagame pekee. Seriously Kagame pekee bila hao majenerali wenzie??
Tatu, kuhusu Niyombare na wengineo ni kielelezo cha failure ya utawala Nkurunzinzah. Ukiona watu wapo ready kukutoa madarakani na unapingwa jitathmini kama unafaa.
Pia nimeona issue ya location ya maandamano. Maandamano ni contagious yanaweza kuanzia ndani ya nyumba yasipodhibitiwa yaweza kusambaa nchi nzima. I think Burundu millitia iliyadhibiti and this is obvious kwani wote tuliona. So you cant expect it to have spread nchi nzima.
Sorry natumia simu sikuweza kujadili points zote kwa pamoja.
Japo nadhani tukubaliane Burundi kuna tatizo Nkurunzinzah wants to be Kagame lakini hana strength wala influence ya kuwa Kagame. Hata Kagame aweza kuwa ana matatizo yake kama issue ya Congo na madini au sakata la Fred Rwigyema but as a leader he is pretty outstanding.
Mwisho help me with this book kama unacho Mimi natafuta kitabu cha Stephen Kinzer: a thousand hills: rwandas rebirth and the man who dreamed it
1. Sijawalaumu watutsi wala wahutu kwa kuchagua wapi wanakimbilia, ninachofanya ni analysis. matokeo ya analysis ni bahati sio deliberate. Facts remain facts. Lakini kama wewe ume observe kuwa suala ni safety issue, je unataka kusema watutsi hawajisikii safe wakiwa Tanzania? Mbona tuliwahifadhi walipopinduliwa mwaka 1958 na baadae kuwapa uraia? Mfalme wao kakaa hapa miaka miwili nadhani. Issue haiwezi kuwa safety pekee.
Pili, kumbuka kuwa mwaka 1993 kwenye machafuko ya burundi ambapo jeshi la kitutsi lilifanya massacres dhidi ya wahutu, wahutu walikimbilia Rwanda. Sasa kama issue ni safety, jiulize je, ni nini kifanye wahutu wengi safari hii wakimbilie TZ na watutsi wengi wakimbilie Rwanda? What makes Rwanda not safe for hutus this time around? Si eitheir wote wangeenda Rwanda au wote wangekuja TZ?
kumbuka i'm not saying kwamba 100% waliokimbilia Rwanda ni watutsi na 100% waliokimbilia bongo ni wahutu, tunaongelea majority.
2. Sheria za kimataifa zinakataza kuweka majeshi mpakani ila kwa masharti maalum. Kuweka majeshi mpakani bila kutaarifu jumuiya ya kimataifa ni 'act of war' dhidi ya yule ambaye umepakana naye. Ndio maana huwezi kukuta kambi za kijeshi mipakani. Kuna umbali fulani wa kimataifa ambapo hakutakiwi kuwa na jeshi from the border. Rwanda haijaweka vikosi vyake mpakani na haiwezi kufanya hivyo officially. Vikosi vilivyopo ni vya hawa waasi.
Na hii ni sababu nyingine kwa nini Rwanda ituhumiwe. Kama kuna vita Uganda na jeshi la Uganda linapambana na vikundi vyenye silaha mpakani mwa Uganda na TZ, Tanzania lazima tungetoa taarifa UN na kuweka jeshi letu mpakani ili kujilinda na kikundi hiki as well. Lakini Rwanda imetulia tuli! Kama yenyewe haihusiki na vikosi hivi, basi na yenyewe ingeogopa na kuweka vikosi vyake mpakani kwa kufuata sheria za kimataifa. Lakini haijafanya hivyo. why? Ni kwa sababu inawajua!
3. Naona na wewe unaongelea kuwa kuna uwapo wa FDLR Burundi. Je una taarifa zozote independent from zile za Rwanda kuhusu jambo hilo. Je unaweza kuthibitisha hata existance ya FDLR anywhere toka wapigwe na FARDC?
4. Tuje kwenye ishu ya ndege. Sijakubali kuwa wanajeshi wa serikali ndio waliotungua, read my comment carefully. Nimesema "ikiwa". kwa maana ya 'for the sake of argument lets assume...' Pili, mimi na wewe hatuna haja ya kutegemea statements za yule na yule, mahakama TATU tofauti zimesha mu implicate Kagame na RPA kwenye hiyo ishu ya ndege. Sasa kwa nini tutegemee statements za watu wengine tena? Mahakama hizi ushahidi wake ni mzito kiasi cha kufikia kutoa arrest warrants, unazipingaje kwa kutumia hearsay statements mkuu? Kusingekuwa na siasa za kimataifa kwenye hii ishu, leo hii kagame na kundi lake wangekuwa ndani kwa mashtaka ya ICTR, ufaransa na spain.
Tatu, historia yako iko flawed kidogo. RPA mpaka siku ndege inatunguliwa walikuwa tayari wameshikilia sehemu kubwa ya Rwanda, soma kwa mfano jinsi walivyoua watu zaidi ya 40,000 na kuteka Ruhengeri for example, na vile vile kutokana na mazungumzo ya Arusha, moja ya masharti ilikuwa ni kuruhusu RPA kuweka vikosi vyake katikati ya Kigali wakati mazungumzo yanaendelea. FACT ambayo haipingiki ni kwamba RPA kwa siri, kinyume na sheria, walizidisha kiwango cha silaha na wanajeshi walioruhusiwa na mkataba ule. Sio kweli kwamba RPA walikuwa Uganda mpaka ndege inatunguliwa. They were already there in Rwanda. Kwa hiyo mpaka tukio linatokea wao walikuwa wameshapanga strategies za nini cha kufanya next. Vikosi hivi ndivyo vilivyoanza immediately kushambulia baada ya ndege kutunguliwa.
5. Mahakama za France na Spain hazijatumia ushahidi wa Nyamwasa, hakuna siasa hapo. Nyamwasa ushahidi wake bado anao mwenyewe. Na narudia tena Nyamwasa of course alihusika ndio maana anasema yuko tayari kutoa ushahidi kamilifu ikiwa mahakama yoyote itampa immunity. Hilo hatushindani. Na je vipi kuhusu mashtaka ya ICTR dhidi ya Kagame ambayo yalikuwa yameandaliwa na Carla del ponte? Mahakama tatu haziwezi kufanya vitu kisiasa my friend.
6. Nkurunzinza anaweza kuwa kiongozi wa hovyo. Lakini anakubalika na waburundi walio wengi. Lete ushahidi kuwa majority ya waburundi hawamtaki Nkurunzinza. Niyombere kajaribu na kashindwa na wenzake wa jeshi hilo hilo, are you sure Nkurunzinza hatakiwi kama unavyodai? Kushindwa kwa coup ni kielelezo tosha kuwa Nkurunzinza anakubalika na kwamba wale ambao hawamtaki ni wachache. Sijui kama unajua kuwa Julius Nyerere aliponea kupinduliwa mara 3! Je huo ni ushahidi kuwa watanzania tulikuwa hatumtaki kwa vile kaponea kupinduliwa mara nyingi kuliko Nkurunzinza?
7. Kuhusu location za maandamano kuwa contagious na militia kuzuia sio kweli. Maandamano yanaendelea hadi leo hii, kwenye sehemu za "sindumuja". Sehemu zingine kuko shwari tu.
8. Mtazamo wako juu ya Kagame nauheshimu ila sikubaliani nao, nobody that know Kagame for what he really is angetaka kuwa Kagame. The only people wanaomuona Kagame kuwa ni kiongozi mzuri ni wale ambao either are ignorant of the facts about the man, au wale ambao kula yao inamtegemea Kagame.
Kagame alivamia Rwanda kwa miaka minne akiua wananchi wasio na hatia, Kagame katungua ndege na kusababisha genocide, Kagame kafanya mauaji ya wahutu ndani ya Rwanda (kibeho massacre), kafanya mauaji ya wahutu nchini DRC (mapping report), mauaji ambayo UN yenyewe imeyaita "genocide" kwenye ripoti yake iliyokaliwa kisiasa, Kagame katengeneza vikundi vya kigaidi vya M23, CNDP,...vilivyofanya atrocities za kutisha pale DRC, ushahidi huu umethibitishwa na ripoti za UN, sanctions za US pamoja na UK, Kagame kashiriki mapinduzi ya Uganda, mapinduzi ya Rwanda, mapinduzi ya DRC. Kabla ya Kagame Rwanda ilikuwa ina uhusiano mzuri na mataifa yote. Baada ya Kagame kuingia, kagombana na Kenya, Africa kusini, Ubelgiji, Ufaransa, Tanzania, Uingereza, na nyinginezo nyingi; South Africa, Kenya, Sweden na nchi zingine zilifikia kufukuza diplomats wa Rwanda na kuvunja uhusiano wa kibalozi at some point in time!
Yeye alikuja Rwanda akidai kaja kumaliza mgogoro wa wakimbizi wa Uganda, na kuleta inclusive goverment. Well, leo hii wakimbizi wa Rwanda ni wengi maradufu kuliko wakimbizi wa Habyarimana! Leo raia wa Rwanda kupotea nchini kwao ni jambo la kawaida tu, miili kukutwa inaelea ziwani ni jambo la kawaida tu. Hiyo demokrasia aliyoleta ndio hii ya kujiongezea miaka ya utawala mpaka 2034? Au ile ya kufunga wapinzani wote kwa mashtaka ambayo hata mashahidi wa serikali wakifika mahakamani wanaigeuka serikali (victoire ingabire)?
Tukubaliane kutokukubaliana mkuu. kuhusu hicho kitabu mimi sina, asante.